ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,054
- 49,739
MAMLAKA ya Usafiri Ardhini (LATRA), imesema inakamilisha upangaji wa viwango vya nauli ya Reli ya Kisasa (SGR), vitakavyokuwa vinatozwa baada ya kuanza rasmi kutoa huduma kwa treni ya mwendokasi kati ya Dar es Salaam na Dodoma.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, Habibu Suluo, tayari Shirika la Reli Tanzania (TRC), lilishapendekeza viwango mbalimbali vya nauli za abiria kwa treni ya SGR na mamlaka hiyo imeitisha maoni ya wadau ili washiriki katika jambo hilo.
Suluo alisema mambo mengi ya kiufundi katika kuanza kwa huduma hiyo ya usafirishaji kwa njia ya reli ya kisasa yamekamilika na sasa wapo katika majaribio yanayotakiwa kufanyika kabla ya kuanza kutoa huduma kwa ajili ya usalama zaidi.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, Habibu Suluo, tayari Shirika la Reli Tanzania (TRC), lilishapendekeza viwango mbalimbali vya nauli za abiria kwa treni ya SGR na mamlaka hiyo imeitisha maoni ya wadau ili washiriki katika jambo hilo.
Suluo alisema mambo mengi ya kiufundi katika kuanza kwa huduma hiyo ya usafirishaji kwa njia ya reli ya kisasa yamekamilika na sasa wapo katika majaribio yanayotakiwa kufanyika kabla ya kuanza kutoa huduma kwa ajili ya usalama zaidi.