Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

Dunia ina mambo mengi ya kushangaza

UNa hoja nzito ila kuna sehem unachanganya kidogo, unachanganya kati ya mazingaombwe na uchawi kamili

Hicho unachokiona wewe na kukikosoa hayo ni mazingaombwe ambayo mara nyingi yanatumia akili tu ila uchawi wenyewe upo ni vile tu bado hujaingia kwenye 18

All in all mlango mkubwa wa uchawi ni hofu, hofu ndio njia ya kwanza kabisa ambayo inaingiza roho wabaya mwilini japo pia kutokuwa na hofu haimaanishi eti uchawi haukuwezi kabisa yapo mambo kadhaa ya kujikinga na hizo roho
anza kwanza kutoa darasa uchawi ni nini ili watu wajadili vizuri
 
Anyway wewe unataka uchawi upi? Ule wa quran(sio mgumu kama inavyodhaniwa kwasababu inatumia maneno ambayo yamezoeleka)

Ama unataka ule wa kale? Japo huu ni mgumu kiasi inaweza kukuchukua kuanzia miez 6 mpaka kukamilika
huu wa kwenye uzi wako ndo uuweke mezani mkuu
 
😂😂😂

Wewe utakuw aunaishi mjini tu!

Kuna beki tatu wetu mmoja alikuwa anamlea bibi yetu(rip) alikuwa mganga, aisee mambo aliyokuwa anatusimlia ni balaa… kwanza aliambiwa akiacha uganga hatozaa, walijuaje kama hatozaa kweli? Mpaka kwaho anahangaikaga huyo mama hana mtoto yuko 40s sasa, alishaend ahospital za kila namna hana ugonjwa wala nini, dawa za kienyeji, akaamua kuokoa anakesha kwenye maombi, akarudi tena kwa waganga, akabadili wanaume lakini hola!
Watanzania wote karibia 95% wanaamini haya mambo ya Ushirikana, uchawi, majini na uganga iwe wa vijijini au mjini.
Story yako kwanza tu unaanza mambo mliyokuwa 'mnasimuliwa' na beki tatu aliyekuwa anamlea bibi yenu, Tuanze hapa kwanza, kwa nini ninyi wajukuu na wazazi wenu hamkuwahi kuyahushudia hayo mambo ya bibi yenu na wazazi wenu hawakuwahi kushudia mambo ya mama yao??
Jambo la pili, mbona kuna wanawake wengi tu wenye matatizo ya uzazi ambao hawajawahi kuhusishwa na uchawi? Vipi kama huyo beki tatu alikuwa na matatizo ya uzazi tayari na bibi yenu alikuwa ameshajua mapema? Vipi kama ni coincidence tu kwamba bibi yenu alimwambia hayo maneno na huyo beki tatu alikuwa na tatizo la kutokuzaa?
 
Uchawi upo ndugu zangu na sio jambo la kushabikia lengo la huu uzi sio kujionesha kujua kitu fulani lengo langu kuu ni kufungua uwepo wa muumba kwasababu wengi huamini njia za mkato pekee na wakati njia ya muumba ndio njia sahihi
 
Sijawahi kusikia story ya uchawi au miujiza isiyo na matobo mengi ya kutosha mpaka najiuliza mtu anawezaje kuamini ujinga wa jinsi hii wa wazi kabisa. Hata hivyo pia ubongo unaweza kutengeneza hallucinations, illusions na false realities kwa sababu nyingi mbalimbali ikiwemo madawa ya kulevya, njaa, ugonjwa, ndoto, hofu, PTSD, uchovu, magic tricks n.k
Shida hapo wewe mwenyewe unajadili vitu vya kusikia, ingekuwa vizuri kama ungekuwa unatoa maoni yako baada kushuhudia hivyo vitu vyenye kuaminika kuwa ni uchawi hapo ingekuwa poa.
 
Shida hapo wewe mwenyewe unajadili vitu vya kusikia, ingekuwa vizuri kama ungekuwa unatoa maoni yako baada kushuhudia hivyo vitu vyenye kuaminika kuwa ni uchawi hapo ingekuwa poa.
Ila waungwana mnapenda ligi sana
Yeye amesema amesikia halafu umemkatalia unataka akuambia alivyoviona, mimi nimeviona nimewasimulia mnasema ni uongo, kwa style hiyo kwako ni ngumu sana kupata haya maarifa labda mpaka yakutokee mwenyew ndio utaamini
 
Uchawi ungekuwepo kweli na ungekuwa unafanya kazi kweli, Africa ingekuwa bara tajiri sana.

Kila mwafrika angetajirika kupitia huo uchawi.

Uchawi siku zote una aminiwa na watu wajinga na watu duni maskini.
Unaijua "Wizards forum"? Inamilikiwa na watu gani na member wake ni watu gani Kama sio wazungu??

Nitajie nchi Inayochapisha vitabu vya uchawi kushinda marekani na Uingereza
 
Najiuliza huo uchawi ni mifuko ya cement na kokoto hadi utake ujenga barabara na viwanda? Sijaelewa kwanini uchawi umehusisha na ujenzi wa barabara na viwanda, nauliza kwa sababu najua kila kitu kina mahali pake ndio maana nivutiwa kutaka kujua kwanini umeuweka huo uchawi kwenye masuala ya ujenzi?
binafsi siufahamu, ila mara ya mwisho humu jamvini wadau walituambia ni kama sayansi isiyofata kanuni za kawaida zilizozoeleka, atkeast kwa navyokumbuka ni hivyo, sasa ili kubalance mzani ungetupiga fafanuzi kidogo ili tuone namna ya kuendelea maana bila hivyo tutaenda na story tunazozisikia tu huku mtaani yule jamaa utajiri wake wa kichawi --- sasa kama kuna utajiri wa kichawi maana yake tunaweza pata fedha tukanunua cement , kokoto, tukaajiri wataalamu tukajenga barabara , madaraja, viwanda, mahospitali na kila aina ya mahitaji yetu.


sasa ili kubalnce mambo tupate muongozo wa pamoja kwanza uchawi ni nini , unapigaje kazi, na katika mazingira yapi. maana isije kua sisi hatuelewi uchawi, na hata wanaotuambia huu uchawi nao wakawa hawaelewi wanachosema
 
Watanzania wote karibia 95% wanaamini haya mambo ya Ushirikana, uchawi, majini na uganga iwe wa vijijini au mjini.
Story yako kwanza tu unaanza mambo mliyokuwa 'mnasimuliwa' na beki tatu aliyekuwa anamlea bibi yenu, Tuanze hapa kwanza, kwa nini ninyi wajukuu na wazazi wenu hamkuwahi kuyahushudia hayo mambo ya bibi yenu na wazazi wenu hawakuwahi kushudia mambo ya mama yao??
Jambo la pili, mbona kuna wanawake wengi tu wenye matatizo ya uzazi ambao hawajawahi kuhusishwa na uchawi? Vipi kama huyo beki tatu alikuwa na matatizo ya uzazi tayari na bibi yenu alikuwa ameshajua mapema? Vipi kama ni coincidence tu kwamba bibi yenu alimwambia hayo maneno na huyo beki tatu alikuwa na tatizo la kutokuzaa?
Bibi yetu alikuwa mzee sana hajiwezi hayo mambo katika nayo kijiji kingine!

Hayo mambo yapo nimeshuhudia mama mmoja kaenda kw amganga akapate utajiri kakaa huko kama mwezi karudi huku kakosea mashara akajila kidole chake akishia kuwekwa c-1 mwezi mzima maana aliwehuka akakimbia uchi uko mitaani, baadaye alikuja kukaa sawa ila ilikuwa ni kasheshe za kishirikina!
 
Ngoja aje kujibu hilo swali la uchawi ni nini ili pia tuweze kujua ni kwa vp huo uchawi ungekuwepo kweli afrika ingekuwa tajiri.
Mnapenda ligi tu ila uchawi upo zaidi kiroho na sio kwa kanuni za asili, naweza kuweka maelezo marefu hapa ila kwa aina yako ya maswali unaonekana hutaki kujifunza ila unataka kubishana

Kama wewe huamini mambo ya kiroho itakuwa ngumu sana kwako kuamini nguvu zilizo kinyume na sheria za asili
 
Ila waungwana mnapenda ligi sana
Yeye amesema amesikia halafu umemkatalia unataka akuambia alivyoviona, mimi nimeviona nimewasimulia mnasema ni uongo, kwa style hiyo kwako ni ngumu sana kupata haya maarifa labda mpaka yakutokee mwenyew ndio utaamini
Mbona hakuna hata kitu ulichoshuhudia ulichosimulia ?!
 
Kuna sehem nimesema mambo yangu yalikuwa hayaendi sawa jambo lililopelekea kwenda kwa waganga na tatzo lilikuwa linatatuliwa ila nilikuja kujua ile haikuwa njia sahihi
Mambo gani ?
Uzazi, Pesa, biashara, ugonjwa, mahusiano, ajira, kesi ?
 
Back
Top Bottom