Bukyanagandi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2009
- 11,626
- 18,223
hivi kwann JOHN F KENNEDY aliuwawa na CIA ?
Kuna madai ya kila sampuli, kuna wanao dai CIA ilihusika, kuna wanao dai kundi la Mafia ndio walihusika kutokana na mdogo wake ambaye alikuwa mwanasheria mkuu wa Serikali ya Kennedy kupanga kuwatia kizuizini mapapa hao wa kuhuza madawa ya kulevya, kuna wanao dai kwamba Kennedy kupenda penda wanawake kulimfanya awe na uadui na kundi la mafia wakimgombania mrembo Marilyn Monroe, wengine wanasema kwa kuwa Kennedy alijaribu mara nyingi kumuua Fidel Castrol ilifika wakati Fidel akachoshwa na upuuzi huo akahamua kushirikiana na KGB wakawakodi ma marksmen majasusi ili wamumalize Kennedy, wapo wanao sema makamu wa Raisi wa Kennedy Mr. L.Johnson ndiye muhusika mkuu wa kifo cha Rais Kennedy.
Binafsi sina shaka kwamba Makamu wa Raisi Mr. L.Johnson ndiye alisuka mipango ya kumuua Kennedy akishirikiana na matajiri wenye viwanda vya kuhunda silaha kweye jimbo lake la Texas aliko pigwa risasi Kennedy, matajiri hao walifikia decision ya kumuua kutokana na msimamo wake wa kutaka kisitisha vita huko Vietnam, wenye viwanda wakaona anataka kuwaharibia biashara ya kuhuza silaha afadhili wamuwahi mapema.
Mkewe Kennedy alikuja gundua mhusika mkuu wa mauuaji ya mumewe hakiwa bado yupo Dallas Texas, wanasema wakati mwili wa Kennedy unasafirishwa kwa ndege kutoka Texas kuja Washington DC, ndani ya ndege walikuwemo makamu wa Rais L.Johnson na mke wa Kennedy among others, wanasema mama huyo alipata ujasiri akasimama akamfuata Johnson alipo kuwa amekaa akamwambia bila ya kumungunya maneno kwamba ana uhakika ndiye anahusika na kifo cha mumewe, wanasema Johnson alinamisha kichwa chini hakujibu kitu!
Kazi ya kumuua Kennedy walipewa marksmen zaidi ya mmoja ambao walikuwa hawajuani, walifanya hivyo kuhakikisha kwamba si rahisi wote waka miss target, kati yao mmoja wao alikuwa bingwa sana wa kulenga shabaha, aliwahi kuhusika kwenye operation kama hizo miaka ya nyuma akitumiwa na CIA alipo kuwa jeshini, ndio alikuja kukili juzi juzi hapa kabla hajafa kwamba ndiye alifanikiwa kumpiga risasi ya kichwani Kennedy akitumia risasi maalum (dum dum bullet) ambazo ulipuka zikigusa mfupa au kitu kigumu, cha ajabu mlenga shabaha huyo alijificha nyuma ya overgrown shrubs karibu na jengo la glassknoll huku akilindwa na Polisi (FBI), baada ya kumpiga risasi Kennedy akafungia silaha yake kwenye briefcase na kuondoka zake bila ya kubughudhiwa na mtu!!
Madai ya kusema muuaji alikuwa ni Mr.Oswald si kweli huyo alikuwa ni chambo tu, hata silaha walio dai walimkuta nayo kwenye jengo la ghorofa sita ilikuwa planted tu na FBI ndio maana silaha ilipo pelekwa kwenye mahabara kwa uchunguzi ikagundulika haikuwahi kutumika siku za karibuni, hata firing mechanism zake zilikuwa na walaki mkubwa, hivyo ni dhahili FBI ilikuwa imepania kumbambikizia kesi Oswald.