Kifo cha Bruce kilichangiwa na mambo mengi yote hayakuwa na uhusiano wowote na masuala ya CIA, kitu cha kwanza ni utumiaji wake mkubwa wa cannabis aliwahi kuonywa na Daktari wake alipo patwa na ugonjwa wa kifafa ghafla akiwa kwenye studio yake aki-dub film, alikaa hosptalini kwa muda baadae akaruhusiwa na kupewa mashariti ya kumeza dawa kila siku ili kudhibiti kifafa kisijitokeze tena, akaonywa kwa mara nyingine kwamba asiwe anatumia/vitu bhangi na dawa za kulevya haionyeshi kama alizingatia mashariti ya madaktari wake!!
Kitu kingine Bruce alikuwa anafanya mazoezi ya viuongo ambayo mengine yalikuwa hatarishi mfano: kutumia umeme kustimulate misuli, wakati fulani aliwahi kuhumiza mgongo wake akiwa mazoezini nadhani alikuwa yuko kwenye zoezi la kunyanyua vyuma kama nakumbuka vizuri, injuries alizo sustain madaktari wake walifikiri hataweza tena kusimama vizuri au kwendelea na michezo/mashindano ya Kung-Fung lakini wapi bwana Bruce bounced back, lakini akawa anaendelea kutumia dawa za kupunguza maumivu ya mgongo - tukiweka maanani idadi ya madawa aliyokuwa anameza kila siku - namely: Dawa za kudhiti kifafa, dawa za kupunguza maumivu ya mgongo na uvutaji/ulaji wa aina fulani ya bhangi yote hayo anayameza kila siku - mtu ungetegemea long term abuse ya nadawa hayo yangeleta nadhala gani eventually.
Kitu kingine Bruce alikuwa anapenda wanawake sana, kifo chake kilitokea akiwa nyumba ndogo, sasa tabia hii ni rahisi sana washindani wako kibiashala kuwatumia wanawake kukudhulu, Bruce alijua kwamba Studio yake na Raymond iliyokuwa inajulikana kama Golden Harvest ilikuwa na ushindani mkubwa na Studio za manyangumi wa Hong Hong wa familia ya Run Run Shaw (sijui kama jina nimepepatia) familia hiyo ilikuwa haipendi jinsi Studio za Raymond Chow na Bruce Lee zilivyo kuwa zimekuja juu kibiashara - wote tunajua Wachina walivyo vicious, wanaweza kufanya lolote kuondoa ushindani.
Now a million dollar question - Vitu gani vilichangia kifo cha ghafla Cha Bruce Lee?
* Binafsi nafikiri sababu ya kwanza inaweza kutokana na utumiaji wake wa madawa mengi kwa wakati mmoja, actually wanasena dawa aliyo pewa (Super Asprin) na mpenzi wake kuzuia maumivu ya kichwa ndio ilichangia kufanya ubongo wake uvimbe na kumsababishia kifo.
* Sababu ya pili, mpenzi wake anaweza kuwa ametumiwa na Kampuni ya Studio za Run Run Shaw kumuua Bruce baada ya kulipwa hela ndefu - kwa nini nasema hivyo: alipo hojiwa na Polisi baada ya kifo cha ghafla cha Bruce, mwanamke huyo majibu yake yalikuwa yenye utata sana, walimuhoji kwa nini Bruce alifia nyumbani kwa binti huyo kwenye kitanda chake - akajibu kwamba Bruce alipitia nyumbani kwangu akanambia anaunwa kichwa nikampatia Super Asprin ameze baadae nikampeleka chumba changu cha kulala nikampumzisha, baada ya hapo akwenda kumwangalia hali yake inaedeleaje mpaka masaa nane yakapita - alidai baadae kabisa alikwenda chumbani kwake akajaribu kumwamusha Bruce bila mafanikio, badala ya kuwasaliana ni mke wa Bruce alawasiliana na Raymond Chow ambae alikuwa ni Business partner wa Bruce, binti huyo hakutaka mkewe wa Bruce afahanu ukweli wa kile kilicho jiri - ndio maana alikimbiza mahiti Hospitalini!! Je hili lilikuwa jambo la kawaida kweli - I don't think so?