CIA walimuua Bob Marley?

CIA walimuua Bob Marley?

Ukisoma hili jarida la high times (lipo mtandaoni) utaona kwamba kipindi cha bob jamaica kulikua na vyama viwili vya siasa vyenye nguvu sana JLP na PNP, JLP kilikua na sera za Ki socialist wakati PNP sera zao zilikua za ki capitalist ambazo bob alikua haziungi mkono kwakua zilikua zina nyonya na kukandamiza wanyonge (babylonian system), sera hizi ziliungwa mkono na CIA kwakua ziliwapa fulsa mbalimbali.

Aidhaa bob alikua anaandaa matamasha ya bure jamaica na kufafanua madhara ya sera hizo za ki capitalist kwa njia ya nyimbo. Wajamaica walimpenda na kumuamini sana bob, jambo lililo wakwamisha sana PNP

BOB alinusulika kuuawa (ambush in the night) siku chache kabla ya tamasha lake la bure la smile jamaica lililokua na udhamini wa JLP, hii ilitafsiriwa na PNP kama kukipa kick chama cha JLP.
Gud analysis
 
Ndoto zangu Ni kuja kufanya kazi CIA kwenye kitengo cha uuaji niwe muuaji wa kutegemewa.safi sana CIA big up kazi nzuri inaonekana
 
Kama Dube Aliuawa Kwa Gun Sishanga Kusikia Hili Kwa Bob Marley.

Sina Uhakika Lakn Hata Senzo Naye Inasemekana Aliuawa Vivyo Hivyo

Hapa nadhani story ni tofauti kidogo.....haihusiani na mkasa wa Bob........
 
Bob Marley Alikuwa Mwanaharakati Na Msema Kweli Hasa Kupitia Music.

Kama Dube Aliuawa Kwa Gun Sishanga Kusikia Hili Kwa Bob Marley.

Sina Uhakika Lakn Hata Senzo Naye Inasemekana Aliuawa Vivyo Hivyo.

Wakweli Huuawa Wakati Wanafiki Huvikwa Taji.
hiii story kweli tupu
 
Wakuu heshima kwenu.

Kwa muda wa miaka kama 20 hivi nimekua mshabiki na mfuatiliaji sana wa muziki wa reggae na waimbaji wake. Nimesoma taarifa mbalimbali juu ya waimbaji wa muziki huu hasa Robert Nesta Marley (Bob Marley) lakini leo nimekutana na taarifa iliyo nishtua kidogo juu ya kifo cha muasisi huyo.

Sote tunajua kwamba bob alifariki kwa kansa iliyo sababishwa na uvutaji wake wa bangi uliopindukia , lakini kwa mujibu wa jarida la high times, bangi haikusababisha kansa iliyomuua bob.

Jarida la ripoti kwamba kansa hiyo ilipandikizwa na aliejifanya muandishi wa habari kwa kumpelekea zawadi ya viatu vilivyo kuwa na waya ndani uliowekewa vimelea vya cancer, waya huo mlimchoma bob kidoleni alipokua akijaribisha zawadi hiyo aliyopewa, baadae mwandishi huyo alipochunguzwa aligundulika ana uhusiano na CIA waliofanya jaribio la kumuua bob (ambush in the night)

Bob kwa kujua alisha nasa kwenye mtego wa maadui wake waliokua wanamuwinda usiku na mchana aliamua ku -condense plan zake za muzik ili kufit ndani ya pindi kifupi cha uhai kilichabakia maana alijua hana muda mrefu wa kuishi, jimmy cliff msanii mwenzake anasema, bob alikua anakunywa chai na kula lunch kwapamoja asubuhi na kwenda mazoezi ya muziki siku nzima na hata usiku wa manane, ili kurekodi kila alichotaka kusema kwa njia ya nyimbo, hivyo jimmy cliff anaamini kwa kipindi hicho kifupi bob aliimba na kurekodi kila ujumbe aliotaka kufundisha kabla hajafa.

Pia moja ya madaktari waliokua wanamtibu bob alishangazwa na style yake ya uimbaji na ushikaji wake wa guiter (kama SMG) katika concert yake ya mwisho, hasa jinsi bob alivoimba wimbo wa REDEMPTION SONG,

"....these songs of freedom is all I ever had"

Daktari huyo alihisi maumivu makali (kutokana na kansa) aliyokua nayo bob kwa jinsi alivyokua akishika paji la uso mara kwa mara, baadae daktari huyo alikiri kwamba bob aliandaa concert hiyo maalum kwaajiri ya kuwaaga rasmi washabiki wake na kusisitiza mambo ya msingi ya kisiasa, kwani afya yake haikuruhusu kabisa.

Bob na timu yake walipokua kwenye mechi ya kirafiki kule ufaransa sote twajua aliumia kidoleni na kansa ikaanzia hapo, high times la endelea kuripoti kwamba kidole kile alicho umia ndicho kilicho chomwa na waya uliokua kwenye viatu, na mbaya zaidi akiwa uwanjani kuna daktari asiyefahamika alikuja kumchoma bob sindano (isiyofahamika) kwenye hicho kidole kama tiba. Lakini sindano hiyo inaripowa kuwa ilikua na lengo la kueneza viini vya kansa mwilini mwa bob. Kwa kweli nashindwa kuamini kama kweli CIA walimuua bob makusudi, sijui wadau mnalionaje hili.
amini tu ndo ilivyo! CIA wasikie kwa jirani,kati ya nyimbo zinazoishi na zitaishi siku nyingi zaidi ni nyimbo za reggae(roots)! salute kwako mkuu,leo nakula reggae tu "live concert za bob marley"
 
Hao wote wamekufa na ajali mmoja na madawa ya kulevya.
Hata hayo madawa ya kulevya inasemekana ni mbinu ya CIA kuua wasanii kwa kuwa expose kwenye madawa(cocain na heroin) na kuwa lock toward addiction, bob alikataa matumizi ya hayo madawa na badala yake alitumia sana bangi (herb) ambayo yeye aliamini ni tamaduni ya mwafika na inamsaidia kufanya meditation.
 
amini tu ndo ilivyo! CIA wasikie kwa jirani,kati ya nyimbo zinazoishi na zitaishi siku nyingi zaidi ni nyimbo za reggae(roots)! salute kwako mkuu,leo nakula reggae tu "live concert za bob marley"
Du inaniuma sana, kujua hili kwani kila nilipochek movie ya mazishi ya bob ilikua inaniuma sana
 
Back
Top Bottom