Album ya Bob Marley One Love yashinda tuzo za Grammy 2025

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
76,095
159,977
images-8.jpg

ALBAMU ya reggae ya mfalme wa muziki wa reggae, hayati Bob Marley, ‘One Love’, imetunukiwa Tuzo ya Albamu Bora ya Reggae katika Tuzo za Grammy za 67, zilizofanyika usiku wa jana huko Los Angeles. Albamu hiyo ilizinduliwa Februari 2024 na Island Records, ikiwa na nyimbo 10 maarufu za Marley, ikiwa ni pamoja na ‘Natural Mystic’, ‘Exodus’, ‘Waiting in Vain’, ‘Redemption Song’, na ‘One Love’.

Miongoni mwa wasanii walioshirikiana kwenye albamu hii ni mjukuu wa Marley, Skip Marley, Daniel Caesar, Kacey Musgraves, Wizkid, Jesse Reyez, Leon Bridges, na Bloody Civilian. Albamu ilishinda dhidi ya uteuzi mwingine mkali, ikiwa ni pamoja na ‘Evolution’ ya The Wailers na ‘Never Gets Late Here’ ya Shenseea.

Ingawa Bob Marley hakuwahi kushinda Grammy wakati wa uhai wake, urithi wake umeheshimiwa kwa njia hii baada ya kifo chake, akiwa ametunukiwa Tuzo ya Mafanikio ya Maisha ya Grammy mwaka 2001 na tuzo kadhaa za Albamu Bora ya Reggae.
 
Vipi hawa wetu kina roma mkatoliki hukuwaona ukimbini wala kwenye nyimbo za utangulizi!
 
Ina maana huko nyuma hawakuona uzuri wake?
Huko nyuma 2024 ? Hio ni repeat kwahio Album iliyoshinda ni iliyofanyika upya..., Ni kama Killing Me Softly (Fugees ilifanya wengi waupende wimbo) au I will Alywas Love You (ni Whitney ndio ulimpatia Sifa) lakini hizo nyimbo sio kwamba zilikuwa hazijapigwa kabla....

In short ndio maana binafsi huwa siangalii Tuzo bali kazi husika... And on that token his message is still valid and will always be valid.... (Pia muziki wake kuwa political and against the establishment mara nyingine huenda ikawa ni ngumu kupata hizo official recognition)

I'm singin'
When the cat's away
The mice will play
Political violence fill ya city, yeah!
Don't involve rasta in your say say
I'm sayin'
Rasta don't work for no CIA

Bless my eyes this morning
Jah sun is on the rise once again
The way earthly things are going
Anything can happen
You see men sailing on their ego trips
Blast off on their spaceships
Million miles from reality
No care for you, no care for me

 
Back
Top Bottom