Maoni yangu kuhusu mechi ya Jana.
Nimeona wengi wakilalamika kuhusu viwango vya mount, kai havert na Gallagher na wengine Ziyech, unapokuwa mchambuzi na mzoefu wa kuangalia mechi ni vizuri ukaangalia tatizo la msingi kwanza kabla ujaenda kwenye matokeo nilichoona Jana chelsea ilikosa identity ya uchezaji au kwa jina lingine tunasema pattern style of playing ikafanya chelsea itumie uwezo binafsi ya wachezaji kunapokosekana Muundo sahihi wa uchezaji utafanya hata baadhi ya wachezaji wasionekane hatari mfano mzuri ni Mudryk ule upande wake haukutumika kabisa mipira ilikuwa haifikii.
Tukija kwa hawa wachezaji wanaolalamikiwa kufanya vibaya tuanze Kai huyu jamaa ni bonge la mchezaji ila anachezeshwa sehemu isiyo sahihi hadi leo Kai namtazama kama mchezaji anayeweza kucheza kwenye no 10 ila sio striker sijui kwanini kocha halioni Hili? Mount katengeneza nafasi mbili za wazi Jana lakini watu wanamponda japo hatukuwa na Muundo mzuri wa uchezaji, Gallagher kajituma Sana lakini kuna sehemu anatakiwa awe improved na kocha hasa kwenye kwenye Technical ability, Ziyech japo kaathirika na Muundo mzima wa uchezaji wa jana lakini aliweza kutoa chance nzuri Sana kwa kai lakini haikutumiwa vizuri
NB: Tuna wachezaji wazuri Sana tumewasajili na wote wameonesha Wana kitu chakuoffer kwenye team hivi pata picha Enzo acheze na Kante au Kovacic pale Kati?
Binafsi naona solution ni kumfukuza kocha kabisa hakuna njia nyingine tofauti, Moja ya sababu kuu naona Potter hatufahi chelsea imekaa wiki mbili bila kucheza game yoyote Jana ndio wakaja kucheza unajiuliza hizo wiki mbili mbona ni nyingi walikuwa wanafanya nini? Kiasi ambacho unaona kabisa imecheza kama vile walikosa msimamizi mazoezini.
juan david
lembu
Covax
Cash Money Forever
johsee