Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Jamani mimi nimekuwa safarini tangu Alhamisi kwa kazi maalumu iliyonitenga na network, sikuweza hata kuangalia mechi ndio naingia nyumbani asubuhi hii. Naona tumeshindwa kabisa kuifunga defensi ya timu C ya Man United ni defensi ipi tutaiweza kuifunga.
Je tutaweza hizi defensi
  1. Brighton vs Chelsea — Tue, 21 Apr, 22:00
  2. Chelsea vs Leeds (FA Cup Semi-Final) — Sun, 26 Apr, 17:00
  3. Chelsea vs Nottm Forest — 4 May, 17:00
  4. Liverpool vs Chelsea — 9 May, 14:30
  5. Chelsea vs Tottenham — 17 May, TBD
  6. Sunderland vs Chelsea — 24 May, 18:00
Wale wanaoednelea kuifuatilia Chelsea wakidhani itabadili matokeo poleni sana. Sisi sasa hivi tumeanza pre-season. Ligi ilishaisha Enzo na qwenzake walipoamua kutoka kuwachimbua wamiliki huko kwenye mahandaki yao na wakachimuliwa kweli hadi wakaaambukiza wachezaji wetu wazuri kama Palmer na Caicedo kupiga siasa kwenye vyombo vya habari.

Chelsea itamaliza ya 12 na safari yetu ya FA inaishia kwa Leeds Unbited

Chelsea is now the NETFLIX, tukitegemea next season kila msimu
Poleni sana

Chelsea itahitaji mabadiliko makubwa ikiwemo kuwaondoa akina Enzo, Delap, Garnacho. Neto na yale malapulapu ya siku zote akina Tosin, Badiashile.

KOcha pia n i mpumbavu huyu, yeye kaja katikati ya msimu badla ya kuendeleza mfumo wa Enzo maresca ambao wachezaji waliumudu anakuja kubadilisha mbinu na kutest mbinu zake za kijinga kwenye timu ambayo tayari ni mbovu. Kocha huyu hana akili na hata akili ndogo aliyokuwa nayo imeondolewa na hao wamiliki wanaomjaza uongo kichwani
 
Nasikia hamjafunga kwenye last four PL games .....

Shida nni wazee ? Kina Garnacho, Gittens , Pedro wote, Delap , Estevao ina maana wanakula mshahara hewa ?

Ni huzuni 😃
 
Kajamaa Rosemary na miwani yake kanawapa matumaini hewa kila siku .....

Amna kocha mle .... mmewekeza over £2b since hawa matapeli wameichukua timu halafu hakuna lolote..... wanaletwa wachezaji hawajakomaa , kwa kigezo cha kusema future .... pia makocha nao mnaokoteza, uongozi serious huyu Rosemary Hawez pata hata timu championship, achana na EPL..... hajui anachofanya anaotea otea, wachezaji ni kama wamejitakia tamaa.... kapoteza dressing room
 
Kupitia anguko la hili genge kuna mengi la kujifunza hata kwenye maisha ya kawaida ya kila siku

Usiwekeze pesa kwenye kitu usichokuwa na maarifa nacho mtaji utageuka ada ya maarifa. £2B zimeliwa na timu na mawakala kama uyoga kisa matajiri wamevamia kitu wasichokuwa na maarifa na passion nacho

Pili ukiingalia timu licha ya kuwa na average players wengi lakini hao hao average player wanamuona mwalimu ni below average/kilaza wanaingia uwanjani kuhakikisha matokeo yanashinikiza kocha kufukuzwa sababu kocha anyonekana ni swahiba wa SD na wamiliki na vile matapeli wanavyojua kujieleza basi anawapet hao matajiri wa Hollywood

Twende mbele turudi nyuma haya mateso yatakuwa ya muda mrefu kama sport directors wataendelea kuwa hawa wanaoamini kuendesha timu kama Brighton plus ushikaji mwingi wa kubebana kisa utaifa

Mwisho hata wachambuzi wengi pale kwa malikia wana ka ubaguzi fulani treatment wanayompa Rosemary angekuwa kocha kutoka taifa jingine wangempasua vipande vipande wengi kwa matokeo haya wanaona kosa la kocha ni 20% wakati ukweli yule ni mwalimu wa college tu
 
Chelsea ikianza kufanya mabalaa yake usirudi, hatukutaki tena
Wewe unajua mkopo ni kitu gani, hii timu sio yako, mwisho wa msimu, pre-season June tutakuwa wote penda usipende, ukichukia sana meza wembe na Limao itapooza hasira yako
 
Mzee wa essay kapotea na kondoo wake wamepotea.
Leo mabeki ni watano
 
Halafu mnakuja kushinda uzi wa Arsenal. Ila kuna watu wana kipaji cha kukosa utambuzi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom