Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hongera ziende kwa di mateo... team aliitoa kwenye hali mbaya saana!! Lakini kafanikiwa kichukuwa FA na champions lig


Kweli kabisa...kuna commentator alikuwa anasema kwamba AVB atakuwa anajiuliza kwamba huyu dogo alifanya miujiza gani ambayo ilinishinda??
 
halafu mbona hawajarusha vya kumeremete?

Wamerusha viwili tu, wajerumani bana.
 
Mungu ni mkubwa maombi yetu nadhani ameyasikia tumenyanyasika kwa mda mrefu.

ukitaka kujua chelsea inapendwa subili kesho uone watu watakavyo pendeza kwenye pamba za bluee...hahahaaaa...sijui Paw kanuna au kafurahi...weraweraaaaa...
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Paw
ni furaha iliyoje? Huku wakiwa ugenini chelsea wameweza kupata kumbe la ulaya. hongera sana chelsea. Mmwaaaa...!!!

dubu furaha niliyonayo haielezeki! Nilikuwa sina mpango wa kumalima sasa nimepata appetite kwa furaha.
 
Ahsante sana dada yangu,

Nimepata taabu kama ile niliyopata siku Bibi alipokuwa labour kutuletea first born.....Ni kazi ngumu kusubiri ushindi wa namna hii!!!



Babu DC!!

hahahahahah nakuona vile ulikuwa unasimama na kuketi hahahaha hongera kwa kupata ulichokuwa unasubiria mie leo nilikuwa sina upande
 
Inabidi kuwekwe sheria ukikosea kwa kusudi unapigwa bani kama siku 3 hivi

sijui mwenzio mgeni..potelea mbali najua ukweli unauma uzuri sijatukana mtu tofauti na kuwachoma moyo. i'm sorry...!!!
 
halafu mbona hawajarusha vya kumeremete?

Wamerusha viwili tu, wajerumani bana.

Hata wakijifanya kubana...tayari wameshapigwa matobo na hakuna jinsi.....

Walidhani kumtupa nje Barca na kocha wao ilikuwa mchezo!!
 
Chelsea Champions.jpg
congratulations chelsea
champions 2011-2012

 
hahahahahah nakuona vile ulikuwa unasimama na kuketi hahahaha hongera kwa kupata ulichokuwa unasubiria mie leo nilikuwa sina upande


Ahsante dada....nilikuwa kama kuku anayetaka kutaga....


Unakunywa kinywaji gani wewe? Au bado unadozi ya Kloro!!

Babu DC!!
 
siku ya kufa Mbwa basi Pua zote zinaziba.
Chelsea leo wanaingia uwanjani kwa Bayern yaani Alianz Arena wakienda kujaribu kuushangaza Ulimwengu.
Hawana rekodi yoyote na kombe hili, ni moja ya timu ndogo ktk mashindano haya, hawapewi nafasi ya kulichukua kombe hili, na kama yupo Mshabiki anayeweka Pesa nyuma ya Chelsea basi atakuwa anayataka Majanga kwa lazima.

Bayern Bavaria Munchen wakiwa ktk uwanja wao wa nyumbani ambao ni wa kisasa chini ya Nahodha Philip Lahm wako ktk hali nzuri ya kimchezo, wanatambulika kuwa ni moja ya timu kubwa Barani Ulaya wakiwa wamebeba kombe hili mara 4, wanapewa nafasi kubwa ya kunyanyua kombe hili kwani kufika kwao Fainali ni wazi kuwa wengi wenye utimamu kichwani tulikutaraji.
Wakiwakosa Wachezaji wao kama Mgogo Alaba, Batstuber na Gustavo Bayern wameonekana kuto kutetereka tofauti na wapinzani wao ambao kwa kuwakosa Terry, Meireres na Ramirez wameonekana kupwaya na hata baadhi ya washabiki wa Chelsea wameonekana kutokuwa tayari kwa mchezo wa leo.

All in all dobi wa kweli utamjuwa siku akipewa nguo nyeupe...

Hatimae dobi wa ukweli kajulikana! Pole sana mkuu
 
weraweraaa chelsea for Life since those days of coach Glen hoddle when Di Matteo was just a mield fielder, gianluca vialli, Denise 'the menace' Wise, celestine babayaro aisee chelsea tunatisha

weraweraaaa...tumefunika mbaya. hadi mwakani tunabanana tena na hao wakina man u na man city kama kawa. hii ni heshima ya vijiweni bana. kesho mi ndo ntakua muongeaji. umemuona drogba na kile kichwa..ameruka hivi akasukumwa lakini mara goooo....hahahaaaaaa.....!!!
 
dubu furaha niliyonayo haielezeki! Nilikuwa sina mpango wa kumalima sasa nimepata appetite kwa furaha.

hahahahaaaaa....!!!weraweraaaaa....malima mtu aiseee...!!!hii ni starter nzuri sana. hapa ina kuwa kunywa maji tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom