hapo kwa ole kama atashindwa kujijenga muda huu sidhani kama ataweza kuwa mwalimu bora hapo mbeleni akielekea miaka 50, baada ya kustahafu soka alianzia career yake ya ukufunzi pale united reserve team, baadae akaelekea cardiff na molde na zote hizo ni timu ndogo sana kipresha,
kivyoyote bwana huyu alikuwa na muda mzuri sana wa kujijenga professional kwenye hiyo career yake ya ufundishaji huko alikotkea, now yupo united timu inayompa kila kitu anachokihitaji na still ameshindwa kudeliver matokeo bora na soka bora ndani ya uwanja licha ya uzoeefu aliokuwa nao, kibaya zaidi timu anayofundisha inamfanya muda wote awe na presha kubwa sana inayochangizwa na uhitaji wa matokeo bora yatakayoweza kurudisha morali ya ushindani wa makombe.
media zinamuandama, mashabiki wanamuandama, wawekezaji wanamuangalia yeye na huku umri ukiendelea kumtupa kwa sababu ana miaka 48 na bado hajajijengea heshima inayostahili itakayozifanya timu nyenginezo washawishike kuhitaji huduma yake pindi atakapoondoka united.
kama atashindwa man utd huenda itakuwa ndio mwisho wa career yake ya ukufunzi, nani atakayemuhitaji pale pale ulaya kuu(german,england, france, spain).
=========
lampard bado anajificha kwenye kivuli cha uzoefu, baada ya kustahafu soka nakumbuka alitumia muda mwingi sana kufanya kazi ya pundit tofauti na mwenzake steven gerrard aliyeelekeza nguvu kazi kwenye fani ya ukocha.
bahati ya pili alipewa timu ya chelsea wakiwa na ban ya usajili na aliweza kuwapa tiketi ya UEFA msimu huu licha ya kwamba alikuwa akipata matokeo yasioridhisha baadhi ya nyakati, kuwapa nafasi ya UEFA akiwa na wachezaji mfano wa tomori, zouma, mount, abraham, odoi na wengineo ni tiketi nyengine inayomfanya aendelee kuaminiwa na wapiga kelele wa pale darajani.
bahati namba 3 jamaa anafundisha timu ambayo haina presha yeyote kubwa ukiachana na mzuka wa bossi kitambi abramovich, chelsea ameshapoteza mechi mbili mfululizo ila husikii legendary yeyote akimnyooshea kidole super frank, hata media za uingereza zimekuwa haziendeshi mijadala ya mara kwa mara juu yake.
kwa umri wake na cv yake ya kiuchezaji naamini anaweza kupata offer nyengine baada ya kuondoka chelsea, hivyo basi nakubaliana na wewe super frank bado ana nafasi zaidi ya kujijenga.
jana nilibahatika kuangalia mechi ya chelsea
- lampard huongozwa na mazoea: hafanyi sub kwa sababu ya kiufundi bali huongozwa na mazoea, nimepitia forum thread nyingi za chelsea kwa kuanzia hapa mpaka reddit nipate kujifunza angalau dhumuni la kuingizwa abraham baada ya kutolewa giroud lakini hakuna aliyeweza kuja na tactical analysis yeyote.
- timo werner ataendelea kulose possession ovyo kila mechi kama ataendelea kuchezeshwa pembeni, jamaa ni mweupe sana anapokuwa mbali ya goli. kama kocha anawajibika kumtafutia werner eneo sahihi la kiuchezaji, kule germany hakuwahi kuzipata goli 20 kwa kutokea pembeni
- sitaki kumzungumzia kai harvetz, eneo lake sahihi linajulikana....tafuteni mechi dhidi ya crystal palace japokuwa hakuchangia goli lakini alicheza vizuri sana na ulegevu wake
- chelsea wanapocheza na giroud mentality yao kubwa ni mpira wa krosi
- hivyo basi chelsea wanahitaji mchezaji mwenye kuuelewa mchezo pindi wanaposhambulia, majirani zetu man city wanateseka sana kipindi hichi kumkosa mchezaji mwenye sifa hizo, miaka ya nyuma walipokuwa na mchezaji aina hiyo walitusumbua sana kupitia mfumo wao wa midfield wawili wanaoshambulia....namzungumzia mchezaji aina ya david silva au KDB.....kwetu tunao watatu wachezaji aina hiyo lakini mfundishaji anazingua....kule kwetu bruno anaweza kutengeneza open chance hadi 6 kwenye mechi moja kupitia angle tofauti lakini conversion rate ikawa 0