Gang Chomba
Platinum Member
- Feb 29, 2008
- 20,734
- 4,869
Habari njema hii, tena amechelewa sana, ameifanya timu icheze bila malengo kwa muda wote aliokaa pale
Ubakize na maneno ya akiba mkuu.
Maneno haya ungeyatoa last season ningekuona shababi kweli.
Ancelotti kaja kwenu kawakuta mnambwela mbwela hamna lolote tangu alipoondoka Jose Mourinho.
Yeye amekuja na akaendelea na timu hiyohiyo aliyoikuta na kisha akapiga kazi na mkabeba makombe mawili EPL na FA.
Msimu huu mmeanza Chelsea wanashinda nusu Dozen tu.
Mabadiliko na Madudu yalianza pale baada ya Kocha msaidizi kutimuliwa na ndipo matokeo mabovu yalipoanza.
Ancelotti alishalaumu kuwa nafasi ya kumchagua kocha msaidizi apewe yeye kwa kuwa huyo ni msaidizi wake yeye na si msaidizi wa Roman.
Lakini hakuna lillofanyiwa kazi na matokeo yake akapewa mtu wa kusaidiana nae kazi ambae hakuwahi kukutana nae hapo awali.
Ancelotti amebeba ndoo ya ulaya mwaka 1989 akiwa mchezaji wa AC Milan na pia akabeba kombe hilohilo akiwa kama kocha wa aC Milan mwaka 2003 na 2007.
Pia ameshafundisha kikosi cha Milan kilicho na nyota wengi zaidi lakini kwa kuwa majukumu yoote alipewa na mmiliki basi aliweza kufanya kazi na Mauro Tassotti ambaye ni mtu aliyecheza nae mpira tangu enzi ya Safina ya Nuhu.
hata Mourinho aliambiwa ampange Shevchenko ambaye yeye alisema kuwa kwa mfumo anaoufundisha haoni nafasi ya Sheva lakini mmiliki alilazimisha tu.
Jiulize JOSE alitimuliwa, then CARLO nae katimuliwa.
Kuna nini hapa?
Mbona makocha wenye uwezo wanaondoka timu hii?