Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Naona hamu ya dunia tufungwe imetimia at least bado tunaongoza ligi vijana walipambana spurs walikuwa bora
Jifariji tu, next game Vs Leicester city then Liverpool, zote unapigwa bikra ishatolewa
 
Kwao wapi kaka?, Chelsea wako London na Totenham wapo London, kama mechi ya Kwanza walifungiwa London hata hii watafungiwa London
Bahati mbaya leo haikuchezwa london, ilichezwa mwezini
 
Kaka mchezo utakua mgumu sn mkuu. Kwanza hawa Spurs msimu ule wa majuzi walituharibia mpango wetu ambao tulikua tunataka tumalize ligi bila kufungwa, na hawa Jamaa wakatufunga.... Nakumbuka ule mchezo ulichezwa tarehe moja January na ilikua game yetu ya kwanza ya mzunguko wa pili hawa Jamaa wakatufunga.


Sasa safari hii tunakutana nao tukiwa tunataka kuvunja record za watu kwa kucheza michezo 14 kwa kushinda mfululizo.

Wao Spurs hawataki hii record ivunjiwe kwao nimeona kwa namna moja au ingine wachezaji na kocha wao wamekua wakijitahidi na wakifanya kila linalowezekana kuhakikisha wanamsimamisha chelsea.



Mchezo utakua ni mgumu sn kwasababu karibu waingereza hasa mashabiki wa timu zinazoifata chelsea wanataka chelsea isimamishwe ili kuipunguza kasi ya kutengeneza mazingira ya kua bingwa mapema.

Nimeona maandalizi kwa timu zote huku kila timu ikiwa haina majeruhi ata mmoja. Pia nimeona namna walivyojaribu mbinu hasa Spurs ktk mchezo wao uliopita kwa kufata mfumo wa chelsea na tayari Conte ameshaliongelea hilo. Na ata dawa atakua kaiandaa vzr.


Chelsea wanapaswa kua makini sn na wasifanye makosa ya kijinga kabisa. Spurs wakipoteza mpira hua wanautafuta kwa nguvu sn, sasa ni wakati wa chelsea kumiliki mpira sn na kupiga pass za uhakika fupi fupi na ndefu.


Nataka nione battle ya Wanyama na Dembele kwa Spurs huku kwetu Matic na Kante. Na Moses na Rose na Walker na Alonso. Huko kwa Delle Alli na Ericksen na Kane hakuna shida sn kwasababu Luiz na Cahil na Azpelicuiter watahakikisha hawaleti mazara. Wakati huo huo Spurs watakua na kz kuwazuia Hazard na Pedro na Costa.


Bado Conte anachanganyikiwa ampange nani amuache nani kati ya Faby na Matic.
Kweli kwa dele ali hakuna shida
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom