Bungeni Dodoma: Rais Magufuli avunja Bunge la 11. Asema ajira 6,032,299 zimetengenezwa, Viwanda vipya 8,477 vimeanzishwa

Bora livunjwe warudi majimboni angalau na sisi raia tupate hizo rushwa ndogo ndogo kama pilau, pesa za ugoro,kofia na mengineyo maana tumezi 'miss' kwa muda mrefu.
Nishajiandaa na kadi za vyama nijilie rushwa ndogo ndogi
 
Wanajamiiforums ,tumekita kambi tangu alfajri maeneo ya bunge hapa Dodoma hapa mambo ni mengi kila mtu yuko bize wewe mwana jf utapata kila kitu hapa hapa na kama unaswali uliza pia .

UTANGULIZI

Kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ibara ya 65 (1,2) inampa nguvu rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ya kulivunja bunge kwa kulihutubia ambapo inatarajiwa muda mfupi ujao leo 16/6/2020 mh rais John Pombe Joseph Magufuli atalivunja bunge la kumi na moja ,itakubukwa kuwa mnamo tarehe 20/11/2015 rais John Pombe Magufuli alilizindua bunge hili la 11 hapa Dodoma kwa mara ya kwanza kama ibara ya 91 (1) ilivyomtaka na hii itakuwa mara yake ya pili kulihutubia na kulivunja pia,hii inamaanisha muda wa bunge la kumi na moja utakuwa umeisha kama ibara ya 65 (2)inavyotamka na kutoa wasaa wa nchi yetu kuelekea katika uchaguzi mkuu wa rais,wabunge na madiwani .

MASPIKA

Job Ndugai anakuwa spika wa sita mzalendo baada ya ukoloni wengine ni

1.Chief Adam Sap Mkwawa 1964-1973

2.Erasto A.M.many'ingu 19731975

3.pius msekwa 1975-2005

4.Samweli sita 2005-2010

5.Anna Makinda 2010-2015

6.Job Ndugai 2015-2020 ambaye ubunge wake unakoma leo na ameshatangaza kuondoka

MAMBO MUHIMU KWA BUNGE LA KUMI NA MOJA

Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania limekuwa chombo kikuu cha kikuungano kinacho jumuisha wabunge 393 ,watanzania bara wakiwa 322 na wanzibari wakiwa 71 .wabunge wanawake kwa ujumla wakiwa 145 na wanaume 248 kwa wabunge wote waliomo katika bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania.

C.C.Mimekuwa na wabunge 287, chadema 63, C.U.F 32 ,ACT WAZALENDO1 na NCCR MAGEUZI 1 ukiachilia hamahama ya wabunge.wabunge wa majimbo walikuwa 264.viti maalum 113 .wabunge wawakilisha wa Zanzibar 5.wabunge wa rais 10 na mwamasheria mkuu wa serkali 1.

Aidha mbunge aliyeuliza maswali mengi ni George Malima lugereje wa jimbo la mpwapwa mawasli 103 na michango 59 huku wizara iliyopokea maswali mengi ni wizara ya TAMISEMI na waziri wake Suleiman Jafo kuwa waziri aliyejibu maswali mengi zaidi,mbunge Dk mary Nagu ndio mbunge alihudumu bungeni muda mrefu kwa vipindi vinne mtawalia huku mbunge George mkuchika akiwa ndio mbunge mwenye umri mkubwa zaidiwa miaka 72 ,mbunge Halima Bulembo yeye ndio mbunge mwenye umri mdogo wa miaka 28 kwali aliingia bungeni akiwa na miaka 23 tu.

Bunge hili la kumi na moja limekamilisha kuchambua na kupitisha bajeti tano za serkali na miswada 82 ya sheria na hasa zile za hati za dharula zilizoletwa na serkali
Kama sehemu ya ya majukumu ya kikatiba ya bunge hili.

BAADHI YA PANDA SHUKA ZA BUNGE LA 11

Kumekuwa na panda shuka za msuguano wa bunge hili na taasisi nyingine katika masuala mbalimbali

1.tarehe 7/sept/2017lilitoke tukio la mbunge Tundu lisu kushambuliwa na risasi ambapo wabunge wengi hasa wa upinzani walizua sintofahamu kuhusu usalama wao na familia zako na kutaka majibu ya kina ya serkali na kuzua mkwaruzano

2.Poul Makonda( RC. Dar es salaam) kuwatuhumu wabunge kuhusika na biashara ya madawa ya kulevya ambapo wabunge walionesha hasira na kutaka serkali imwonye

3.Poul Makonda (RC.Dar es salaamu) kuwatuhumu wabunge kuwa wanasinzia tu bungeni na ikapelekea kuitwa mbele ya kamati ya bunge kuhojiwa

4.wabunge wa upinzania kuwekwa vizuizini kwa miezi kadha na kuzua hofu ya uonevu mfano Godless lema,Freeman mbowe,lijualikali,Halima mdee ,Joseph Mbilinyi na nk.

5.Hama hama ya wabunge wa upinzani kihistoria bunge la kumi na moja ndio limetia fora wa wabunge wengi kuhama vyama vyao vya awali na kujiunga na ccm

6.Hoja ya CAG ,baada ya CAG mstafu kutoa hoja yake wakati akihojiwa na redio ya umoja wa mataifa kuwa bunge ni dhaifu kuisimamia serkali uongozi wa bunge na baadhi ya wabunge walikuja juu kutaka aitwe na ahojiwe na hili lilifanyika ba baadae akaoneshwa mlango wa kutokea

7.kufukunzwa kwa wabunge kutumika umma kwa sababu za utoro bunge hili linalomaliza muda wake lilifukuza wabunge wawali kazi mbunge Joshua Nasari na Tindu lisu kwa kile kilichotajwa kuwa ni utoro

8.Spika kuugua kwa muda mrefu na kuzua taharuki ,baada ya spika wa bunge la kimi na moja kulazwa nchini India na kudaiwa kutumia pesa nyingi hapa nchini na hasa bungeni kulikuwa na hofu.

9.Itakumbukwa wakati wa bunge hili kuanza siku ya kwanza ya hotuba ya rais wabunge wa upinzani waliondoka bungeni kwa madai ya kutoridhika na matokeo ya urais Zanzibar chini ya mwavuli wa ukawa hivyo kususia hotuba ya rais

10.Madai ya kuumizwa kwa kiongozi ya kambi rasmi ya upinzani bungeni ambapo pande mbili bado zinarushiana maneno kama ni kweli alishambuliwa na wengine wakisema ameanguka kwa kuzidiwa na pombe

11.ishu ya mbunge Cecil mwambe aliyekiacha chama chake cha chadema na kuendela kuhudumu ambapo jamii ya watanzania ilishangaa kwani katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 71 (1,2,) inatamka kuwa ubunge wake utakuwa umekoma baada ya kuhama chama.

12.Kutokuoneshwa bunge live ,hili lilizua kizaazaa bungeni na mitaani watu wakitaka bunge lioneshwa life.

13. Ishu ya corona ambapo wabunge wa upinzani waliamua kuondoka kwa madai serkali haikuchukua hatua za kuzuia

14.ishu ya escrow ambapo mwanasheria mkuu wa serkali aliondoka bungeni kwa aibu

15.mwenyekiti wa chama cha wananchi C.U.F professor lipumba kuwafuta ubunge wabunge 8 kwa wakati mmoja na kuwafanya wakose sifa za kuwa wabunge

MAFANIKIO YA BUNGE LA KUMI NA MOJA.

Hata hivyo kumekuwa na mazuri ya bunge hili la kumi na moja


1.ujenzi wa shule ya wasichana kwa kutumia michango ya wabunge na wahisani ambapo shule hii imepewa jina la bunge

2.kushirikiana kwa karibu ya serkali kwa ukaribu na kufanikisha kusimamia miradi ya kimkakati ya serkali

3.kusomamia malipo ya wabunge watoro wa vikao ,bunge hili la kumi na moja limeonesha umakini wa kusimamia malipo hewa ya pesa za walipakodi

4.kupunguza urasimu wa habari na kupitisha miswada haraka ili kwenda na kasi ye serkali

5.Kulinda hadhi ya bunge ,bunge hili la kumi na moja halikubali kuyumbishwa kwani limekuwa likiwaita na kuwahoji wote walolionekana kupingana na mwenendo wa kanuni na sheria za kibunge.

6.kutetea wabuge walioonekana kuonewa na vyama vyao mfano cecil mwambe na lijualokali

7.kuunda mfumo bora wa kidijitali ilikuwawezesha wabunge kupata taarifa za kinachoendelea bungeni hata kama hawapo bungeni

8.kuihoji serkali juu ya matumizi ya pesa za umma hasa zile za kwenye miradi ya kimkakati

9.kuishauri serkali juu ya hoja zilizowekwa mezani

10.kuungana wakati wa matatizo kama vifo vya wabunge wenzao na waiopata matatizo ya kuugua na kilazwa

WAGENI WAALIKWA

Wageni mbalimbali wamewasili hapa mjini dodoma tangu majuzi na wengine wanaendea kufika ,wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama tayari wamekwisha kufika ,mawaziri wakuu wastafu na mabalozi wa nchi marafiki bila kuwa sahau mabalozi wa mashirika mbalimbali ya kimataifa au waaakilishi wao viogozi ni wengi.
Wa kuu mikoa wenyeviti wa vyama vya siasa viogozi wa dini madhehebu mbalimbali

Ulinzi umeimarishwa mara dufu gari za dolia usiku mzima na alfajiri hii askari kila sehemu hasa maeneo ya bunge na ikulu ,usafi pia umefanyika kwa kiwango cha kuridhisha tofauti na siku nyingine za kawaida

Television karibu zote zita kuwa hewani nawaona wawakilishi/wanahabari wao mapema sana kuna vyombo vya nje kama CRI .DW .BBC na ndani ya nchi TBC1,channel ten,ITV.star Tv.clouds tv.EATV watu wa online tv ,blogs ,magazeti na n.k

Nipo hapa bungeni unaweza ukaweka swali hapa


Karibuni


USSR
Kwenye list ya maspika umekosea sequence kidogo.

(1) Abulkarim Karimjee -Mpaka 1962
(2) Adam Sapi Mkwawa- 1962- 1973
(3) Erasto Mang'enya- 1973- 1975 (Sikumbuki ni nini kilichomfanya Mkwawa aache gap hili)
(4) Adam Sapi Mkwawa - 1975- 1994
(5) Pius Msekwa - 1994- 2005
(6) Samwel Sita - 2005-2010
(7) Anna Makinda- 2010-2015
(8) Job Ndungai - 2015-2020
 
Kama mojawapo ya kazi ya wabunge ni kuishauri na kuikosoa serikali pale panapo hitajika kufanya hivyo, sasa imegeuka kinyume na sasa baadhi ya wabunge hasa wana ccm ni kuitetea serikali
Bunge la hovyo sana kuwai kutokea hapa Tz. Sioni umuhimu wa kuwepo Bunge hapa kwenye nchi ya Yesu.
 
Cdm ni chama makini sana hawapo tayari kutumiwa kama rubber stamp kupitisha sheria mbovu, ambazo zitakuja kuwaumiza watanzania.
Chadema watatoka bungeni,halafu wataa canteen,kumsikiliza Rais
 
Bunge la Ndugaye limeshindwa kuisimamia serikali na badala yake limekuwa ni mtetezi wa serikali
Bunge linapaswa kutafakari kama limeisimia serikali ambao ndo wajibu wake mkuu au limekuwa sehemu ya serikali katika kipindi cha miaka hii mitano
 
Spika wa pili ni Erasto Mang'wenya. Mtoa Uzi fanya ku-edit hapo ili kuweka kumbukumbu sawa.
Mang'enya (siyo Mang'wenya labda ni typo tu) alikuwa spika kwa muda mfupi sana kama nilivyoonyesha hapo juu, utumishi wake mwingi ulikuwa serikalini. Asingekuwa Spika wa kwanza kwa vile wakati Bunge letu la kwanza linaaza yeye alikuwa mwakilishi kudumu kwenye Umoja wa mataifa
 
Msafara wa spika umekweisha ingia ,spika job ndugai anaingia kwenye eneo la bunge kama mwenyeji kumsubilia mgeni rasmi Jonh pombe magufuli
 
Kwahiyo likiwa na wapinzani wachache Ndiyo uchumi wa Tanzania utapanda kwa asilimia angalau 8%?
Thread yako inatoa kumbukumbu nzuri ya matukio.

Hili litakuwa ni bunge la mwisho lenye wabunge wengi wa upinzani.

Hali halisi inaonyesha bunge lijalo litakuwa na wabunge wachache sana wa upinzani huku likiongozwa na KUB mpya!
 
Kwa uzoefu wangu japo si sheria mara nyingi ma Rais waliopita huwa katikati ya muhula huenda Bungeni kuhutubia kuonesha muelekeo wa Serikal yake lakin inekuwa tofauti kwa mwamba huyu.

Kila la Kheir Mwamba, Jabali, The Great Dr John J P Magufuli mtaani tunamwita Rooselevelt wa Bongo kwa kutuvusha kwny zahma ya corona
Umesahau kabisa kuwa mficha maradhi siku zote kifo ndio umuumbua, endeleeni kuchezeshwa ngoma ya madogori
 
Ukiambiwa nyinyi ni zaidi ya wana futuhi mnarusha ngumi hewani.

Mlipo kuwa mnaruhusu mfumo wa multi party system mlilazimishwa? Au hamkujua kuwa huo mfumo alimaanisha kuwa kutakuwa na vyama vya upinzani?
Wingi wao haujasaidia chochote bora tuwe na Wabunge wa chama kimoja tu chama tawala
 
Kwa akili za watawala wanadhani upinzani ni Mbowe na Lissu au zile kombati zao
uzuri ni kwamba upinzani unafutwa kibabe (sio kidemokrasia) hivyo upinzani halisi bado upo sana!.
watawala wanajidanyanya/mnawadanganya na kweli wamedanganyika!.
 
Ikiwezekana asiishie tu kwenye kulivunja hilo bunge! Alibomoe kabisa na hilo jengo lake maana ndani ya awamu hii ya tano, hilo bunge limeinufaisha zaidi ccm na viongozi wake kuliko sisi wananchi.
 
Back
Top Bottom