Aya yoyote unayoiona katika Qur'an,imeandikwa kwa sababu maalumu na na wakati maalumu.Hiyo aya haihusiani na sasa,hiyo iliandikwa wakati hao walikuwa maadui wa kuwapiga waislamu na kuwavamia waislamu,sasa kulikuwa na waislamu,ambao sio waislamu wa kweli wakipeleka siri za waislamu kwa hao watu.
Ni sawa sisi Tanzania wakati wa Idi Amini,Uganda alikuwa adui wetu,kipindi chote cha utawala wake,alipoangushwa katika utawala wake,maandishi yanayohusina na uadui wa Uganda kwa Tanzania,hata kama yapo,lakini sasa sisi sio tena maadui na Uganda.Kwa sababu kipindi kimepita cha uadui huo,haupo tena.Tumia akili unaposoma maandiko yoyote.Ujuwe kwa nini andiko hilo liko,ni kama andiko la Yesu
"Asiye na upanga,auze koti anunue mmoja".
Andiko hili ukilisoma juu juu,utaona Yesu ni mtu chinja chinja,anaamrisha wafuwasi wake,wauze makoti wanunue silaha.Na kazi ya silaha ni uwaribifu na uchijanji,kumbe sivyo.