Magaidi
wanachafua Uislamu
Mi ni Mkristo, najua kuwa wako waislamu ambao ni wema sana,
tena baadhi ya Waislamu ni wema kuliko baadhi ya Wakristo.
Namaanisha wako Waislamu wanafanya matendo mema kuliko baadhi ya wanaojiita "sisi ni Wakristo"
Ila haya makundi ya kigaidi yanachafua Uislamu hata yanafanya baadhi yetu tusiwaamini baadhi ya waislamu
Haya magaidi Sera yake kuu ni
Kutawala dunia kwa kutumia miongozo ya Qurani.
Mara nyingi huwateka Wakristo na kuwachinja eti sababu kuu ni kuwamaliza, wasiwepo hapa duniani kwa kusingizia wanabariki matendo maovu kama Ushoga.
Kule Kenya chuo kikuu cha Garisa Al Qaida waliwatenganisha Waislam na Wakristo, kisha wakawapiga risasi na kuwaua Wakristo na kuwaacha Waislam.
Huwa wanawatenganisha kwa kuwaambia wasome sura fupi za Qurani kama Sura Fatiha au wataje nguzo tano za uislam au kwa kukiri kuwa ni dini gani, wakishindwa basi wanawachukulia kama wakristo.
Haya makundi yanachafua sana Uislamu. Wanapochinja wana mwita Mungu kwa jina la Allah.
Wakifulahia ushindi wanapiga Takbir kama wanavyofanya Waislam
Ukiwauliza wanasema wao ndo wanafuata maagizo ya Qurani na Uislamu kwa usahihi, bila woga na wanapigania maadili ya dini hiyo yasivunjwe.
Ninachoshangaa wanawakamata na kuwachinja Wakristo lakini waumini wa dini nyingine kama, Wahindu, Wabudha, Wapagani hawana ugomvi nao, hawa wadhulu kwa namna yoyote.
Adui yao ni Mkristo sababu haijulikani kwani ninavyojua Mkristo hapendi Ushoga, Wizi, Ugonvi, na matendo mabaya kwa ujumla.
Siyo kila jengo linaloitwa kanisa ni nyumba ya ibada ya Wakristo.
Kuna kanisa la Lusifer, Warastafarian, Wamomoni, Wapinga Kristo nk.
Ambayo baadhi ya hayo ndiyo yana fanya vitendo viovu kama kuozesha Mashoga na Wasagaji.
Kanisa la Kristo linafuata Maagizo yaliyofundishwa na Yesu Kristo na ndilo wanalo sali Wakristo, kama Wakatoriki, Walutheli, Wasabato, nk
Siyo kila kanisa, ni la Kristo.
Nina waomba ndugu zangu Waislamu tusiwaendekeze magaidi,
mara kadhaa wanawachinja hata Waislamu wenzao kwa kusema hawaipiganii dini inavyopasika.
Magaidi wanachuki na Wakristo na hawaelezi chanzo cha chuki zao.
Hakuna mahali Ukristo unaruhusu matendo maovu kama Ushoga