Kulwa Jilala

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
3,510
7,755
Jumanne, Agosti 22, 2023

Benki kuu ya Tanzania BoT imesema akiba ya fedha za Kigeni hadi jana ilikuwa Dola za Marekani bilioni 5.41 ambacho kinatosha kuagiza bidhaa za nje kwa miezi minne na siku 27.

Dar es Salaam. Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imesema akiba ya fedha za Kigeni hadi jana ilikuwa Dola za Marekani bilioni 5.41; kiasi ambacho kinatosha kuagiza bidhaa za nje kwa miezi minne na siku 27.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 22, 2023; Mkurugenzi Utafiti na Sera wa benki hiyo, Suleiman Misango, amesema upungufu uliopo sasa wa fedha za kigeni ni himilivu kwakuwa akiba ipo ya kutosha.

Tangu vita vya Ukraine (Machi 2022 hadi Agosti 21, 2023), BoT imeuza Dola 5.18.5 milioni katika soko la fedha na kuanzia Julai Mosi hadi jana BoT ilikuwa imeuza zaidi ya Dola milioni 100 ikiwa ni ongezeko kubwa kuliko zaidi ya Dola milioni 62 zilizouzwa Julai hadi Septemba 2022.

Juni 8, 2023; Gavana wa BoT, Emmanuel Tutuba alinukuliwa akisema hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa zinaifanya Tanzania kuwa salama dhidi ya changamoto ya upungufu wa sarafu za kigeni ulioathiri nchi nyingi.

Miongoni mwa mataifa yaliyoathirika na upungufu wa dola ni Ghana, Misri, Zimbabwe, Nigeria na Kenya, ambayo baadhi yanafikiria kuweka kando matumizi ya dola katika biashara zake.

Hivi karibuni wakati wa mdahalo wa wadau wa sekta binafsi barani Afrika uliofanyika jijini Nairobi, Rais wa Kenya, William Ruto alitoa wito kwa mataifa ya Afrika kuwa na mfumo wao wa malipo na kuweka kando matumizi ya dola.

Akizungumza na Mwananchi Digital, Tutuba alisema licha ya akiba ya fedha za kigeni kupungua nchini, hakuna changamoto hadi sasa.

Alisema Tanzania kila siku inauza hadi wastani wa dola milioni mbili, kiwango ambacho hakifikiwi na nchi yoyote katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Hadi Mei, mwaka huu, Tanzania ilikuwa na akiba ya fedha za kigeni ya Dola bilioni 4.88 zinazotosha kuagiza bidhaa na huduma kwa miezi minne na nusu, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita
 
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imesema ina akiba ya kutosha ya Dola za Kimarekani ambazo ni Milioni 5,441 zinatosheleza nchi kuagiza bidhaa na huduma nje ya nchi kwa miezi 4.9.

BOT imeyasema hayo ikiwa ni baada ya kuwepo kwa upungufu wa Dola za Kimarekani duniani ambao umechangiwa na athari za Uviko - 19, athari za vita ya Russia na Ukraine, mabadiliko ya Tabianchi, utekelezaji wa sera ya fedha ya kupunguza ukwasi katika nchi mbalimbali pamoja na ongezeko la mfumuko wa bei.

Akizungumza mkoani Dar es Salaam katika mkutano na wadau kutoka sekta ya benki, wahariri wa habari na wauzaji wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni nchini.

Mkurugenzi wa Sera na Tafiti za Kiuchumi kutoka BOT Selemani Misango amesema, hali ya upatikanaji wa fedha za kigeni nchini imeendeea kuwa himilivu na inatarajia kuendelea kutumia akiba hiyo kuongeza ukwasi katika soko la fedha za kigeni nchini.

Amesema katika kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2023 mpaka Agosti 21, 2023 BOT imeweza kuingiza Dola Milioni 100.5 za Kimarekani ikilinganishwa na Dola Milioni 62 katika kipindi cha Julai mpaka Septemba, 2022.

Chanzo: TBC
 
Haya sasa tena maajabu mengine ya Mussa!

Tanzania iliyokataa uwepo wa corona kijima kijima, yenyewe na corona wapi na wapi?

F4JMTr9aYAACNhH.jpeg


Corona ipi sasa wakati hii mambo haikupata kuwapo pande za kwetu?

Wenyewe huku si tukijikita kwenye utalii wa nyungu Kwa raha zetu?

IMG_20211211_082805_567.jpg


Magwiji wale wale, leo kama si wao vile na wala hawakuwahi kuwa hapa:

Unafiki mkubwa!
 
Haya sasa tena maajabu mengine ya Mussa!

Tanzania iliyokataa uwepo wa corona kijima kijima, yenyewe na corona wapi na wapi?

View attachment 2725911

Corona ipi sasa wakati hii mambo haikupata kuwapo pande za kwetu?

Wenyewe huku si tukijikita kwenye utalii wa nyungu Kwa raha zetu?

View attachment 2725914

Magwiji wale wale, leo kama si wao vile na wala hawakuwahi kuwa hapa:

Unafiki mkubwa!
Kutapatapa hakuishi kwa anayekata roho.

Chaguzi zimekaribia, hofu ni kuu
 
Back
Top Bottom