BAWACHA: Rais Samia asiwatambue Wabunge 19 wa Viti Maalum waliofukuzwa uanachama CHADEMA

Hili suala halina ugumu wowote ila kama yeye atamlinda Ndugai kwkw wote ni CCM. Na CCM ndiyo iliwapa zawadi hao covid-19.
Kikatiba wabunge wote pamoja na Ndugai mwenyewe wapo pale kutokana na uchaguzi mkuu wa 2020 uliokuwa wa mabavu. Mbaya zaidi ni kwamba SSH nae ni mnufaika wa mbinu zilizowaweka wenzake bungeni.
Hawezi kuwasaliti.

Tangu chadema imeanza kushiriki uchaguzi je ni lini uchaguzi haukuwa na mabavu?

Na mbona mlikuwa hamsusi?
 
siyo kweli bunge lina jitegemea na taasisi ya rais inajitegemea huwezi rais ukaanza kumpangia bunge mambo ya kufanya utakuwa umenajisi bunge muacheni mama msimvunjishe sheria
na yule kichaa wenu meko alikuwa analifanyeje bunge la ....NDUGAYe....
 
Hili suala halina ugumu wowote ila kama yeye atamlinda Ndugai kwkw wote ni CCM. Na CCM ndiyo iliwapa zawadi hao covid-19.
Kikatiba wabunge wote pamoja na Ndugai mwenyewe wapo pale kutokana na uchaguzi mkuu wa 2020 uliokuwa wa mabavu. Mbaya zaidi ni kwamba SSH nae ni mnufaika wa mbinu zilizowaweka wenzake bungeni.
Hawezi kuwasaliti.
Hivi kwa mazingira ya Tanzania kipindi cha Mwendazake unadhani Chadema wangeenda kufungua kesi haki ingetendeka?

Hapa duniani kuna kitu kinaitwa KARMA ndio kipo na nilazima ifanye kazi. Naimani Rais wa sasa Mama Samia ni Mungu pekee ndio kamweka hapo alipo kwa makusudi flani, na siku zote kusudi la Mungu ni lazima litimie. Kila mtu kashuhudia uvunjifu wa wazi wa katiba juu ya wabunge 19 pale bungeni, na hili sio jambo dogo na nilazima litatuliwe la sivyo Karma itafanya kazi yake.

Mh. Rais Mama Samia leo tunapaswa tumuombee kwa Mungu ili atende sawasawa na mapenzi ya Mungu ili kuepusha Karma.

Tukutaneni Dodoma bungeni saa 10 jioni
That's correct by 100%

Hebu tujiulize hivi si huyu huyu Spika Ndugai aliyetekeleza kuwafukuza ubunge wale wabunge wa viti maalum wa CUF, mara tu alipopata habari kuwa wamevuliwa uanachama na CUF ya Profesa Lipumba??

Sasa ni kitu gani kinampa kigugumizi kutekeleza hivyo kwa suala la akina Halima Mdee, wakati mazingira yanafanana??

Au ndiyo tuseme kuwa sheria zetu zina "double standards" zikifanywa na CUF ya Profesa Lipumba, linatekelezwa na likifanywa na Chadema ya Mbowe, halitekelezeki??
 
Ndiyo maana akamuita Spika Ndugai katika kikao cha "siri" pale Ikulu ya Chamwino Dodoma

Wananchi tutaifuatilia hiyo hotuba kwa makini sana na iwapo ataipitisha hotuba yake bila kugusia suala hili la wabunge wa viti maalum wa Chadema, basi tutajua ndiyo wale wale wanaCCM, na hakuna jipya!
Rais ni mwana ccm kweli kweli usiwe na shaka na hilo,hakuna urais nje ya ccm
 
Mama alishasema hajaja kutengua mambo ya hayati Magufuli,bali kuyatimiza, yeye leo anaenda kuhutubia bunge,haendi kuchunguza uhalali wa wabunge waliopo ndani ya bunge.
 
Katika mkutano huo, Catherine Ruge amesema:

Tumeona kwenye vyombo vingi vya habari kuwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassani anaenda kulihutubia Bunge tarehe 22 -04-2021 kwa mara ya kwanza tangu alipoapishwa kwa rais wa JMT kufuatia kifo cha mtangulizi wake, Dkt. John Magufuli.

Kuelekea tukio hilo, sisi BAWACHA tuna jambo mahususi amabalo tungependa kuliwasilisha kwa Mh. Rais.

Jambo hilo ni uwepo wa wanaoitwa Wabunge 19 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rais Samia Suluhu Hassan akiwa anakwenda kulihutubia Bunge hapo kesho, sisi wanawake wa CHADEMA tungependa atambue, katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuna watu wanaoitwa Wabunge 19 ambao wapo katika hilo bunge analotaraji kuhutubia, kinyume na katiba...

Hata hivyo, hao Wabunge 19 hawajakidhi vigezo kwa mujibu wa Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwakuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameapa kuilinda katiba ya JMT na amekuwa akieleza hivyo mara kadhaa kwenye hotuba zake ambazo amekuwa akizitoa baada ya kuwa ameapishwa.

...atakuwa amevunja katiba kwa kuwaruhusu hao wanaoitwa Wabunge 19 kuhudhuria vikao vya bunge na kushiriki shughuli mbalimbali za bunge.


----- MAONI YANGU ----

BAWACHA hawaelewi maana ya kutofautisha mihimili​

Nimesikiliza maongezi ya Bawacha walivyokuwa wanaongea na waandishi wa habari Dodoma yaani inaonekana wazi kuwa hawajui ni nini wanataka au ninini wafanye.

Unapomwambia Rais anapoenda bungeni asiwatambue au aende kuongelea suala la hao wabunge ni kumkosea adabu mheshimiwa Rais.

Yaani mnamtaka avunje katiba hadharani ili baadae mje tena muanze kusema kavunja katiba; hivyo atakuwa anaingilia mhimili mwingine, hiyo haiwezekani.

tafuteni agenda nyingine siyo kumuingiza mama kwenye mifarakano ya taasisi yenu.

Asante
Kwa nini Naibu spika anawakumbatia?
 
Back
Top Bottom