Hii ni kweli kabisa, huwa si wa kubezwa kirahisi. Wapinzani wanahitaji kujipa muda wa kutafakari kabla kumuattack katika kila jambo analolisimamia. Wapinzani wamekuwa wakurupukaji muno mwishowe wananchi wameanza kuwaona ni wapuuzi.Huyu jamaa usikurupuke naye mwanzo kwa sababu ana hulka ya kuibuka na ushindi mwishoni hiki kitu hata wapinzani hawajikielewa wanakuwa wepesi kumuattack mwanzo badala ya kusubiri kwanza.
Jamaa alichukua form ya urais hakuwa hata na uhakika wa 10% kwamba atakuja kuwa raisi, majina yalikuwa membe na lowassa. Nyota yake inayong'aa mwishoni ilianza kufanya kazi hapa, hata January Makamba alikuwa na nafasi kubwa kushinda Magu lakini kilichotokea anajua Mungu tu.
Lakini wengine tulikuwa tunamuombea sana achukue form kwenye uchaguzi wa 2015. Nakumbuka mzee wangu alikuwa anapenda kuniuliza ni mtu gani ni sahihi kwa nafasi ya Urais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kabla ya 2015 mara zote nilikuwa namjibu ni Magufuli. Alikuwa ananishangaa sana, alikuwa anasema huyo ni mzuri sana lakini hawezi maana hana pesa na hana mtandao. Nilikuwa namwambia ya Mungu ni mengi lakini alewa ni huyo huyo.
Kwa upande wa Zanzibar nilikuwa namwambia ni pa gumu mno na uchaguzi utaharibika. Na kweli baada ya uchaguzi Magufuli alikuwa Rais na Zanzibar uchaguzi uliharibika. Mzee wangu mpaka leo hii huwa hanielewielewi. Kwa mfumo wa kabila letu huwa anasema nilifaa kuwa mganga wa kienyeji.
Sent using Jamii Forums mobile app



tunahitaji vitu bab kubwa because we deserve 