Unafananishaje ya Makongoro Nyerere na Kikwete!?
Makongoro Nyerere alikua mbunge mwaka gani!?
Tuje kwa Ridhwani,unaamini hakukuwa na mtu wa kushindana na Ridhwani humo humo CCM!?
Haijaishia hapo mama yake na yeye amewania nafasi hiyo hiyo kama ilivyo awali.
Matokeo yake unaingiza watu wapuuzi kwenye serikali na wanafanya upuuzi kisa wamejiwekea legacy humo ndani.
Huyo Bill Clinton uliyemtaja familia yake ilifanya kama hivi!?
Je huyo Nyerere uliyemtaja alifanya kama hivi baba kumpigia debe mkewe na mtoto wake waingie uongozini wakati mmoja!?
Mkubali mkatae hiki chama ni saratani hapa nchini.
Huku Kigamboni wamechagua hadi mabeki tatu kuwania udiwani na wengine serikali ndogo pia.
Kisa tu wanawahonga pesa wajumbe wanaopiga kura za maoni.
Na unategemea hawa ndio watufikishe MAHALI!?