Mkuu bora umeongea wewe,ila kuna chawa wa mama huko watalipinga hili.Nililalamika sana hapa kuhusu Masoud kipanya kutopata support kubwa ya serikali kwenye uzinduzi wa gari lake. Hata kama ni kampuni yake binafsi, lakini akiwezeshwa atatoa ajira na kodi serikali itapata.
Elon Musk makampuni yake hayatengenezi faida, yapo kwa hisani ya ruzuku. Sasa wanashindwa nini kumwezesha Mtanzania aliyeonesha nia na uwezo? Masoud ndiye alikuwa mtu sahihi wa kwenda naye Korea ili ajifunze jinsi ya kuendesha kampuni ya magari.
Tulikua tuna mambo mengi ya kimkakati ya kujifunza kwa S.Korea tofauti na filamu.
Angalia filamu ina contribute asilimia ngapi ya mapato halafu uone tulistahili kuweka mkazo mkubwa vile badala ya kutizama mambo nyeti kwanza!?
Ama kweli tumekosa rais mwenye maono.Nahisi hata WaKorea wenyewe wametucheka sanaaaa tena saaanaaaa.