Kumbe hujui kuwa Darfur ina mafuta mengi na hiyo ya kuua watu weusi ilikuwa ni njia ya kuwahamisha wakazi hao ili kupisha uchimbaji. kipindi hicho, China National Petroleum Company (CNPC) ndiyo walikuwa wawekezaji wakuu wa nje kwa serikali ya Sudan. Ile ilikuwa ni proxy war kati ya China na Marekani huku ikihusisha serikali ya Chad.
Ndiyo, visima vingi vya mafuta viko sudani ya kusini, huku mashirika ya mafuta ya magharibi yakiwa na umiliki. Mwamba huo wa mafuta unaambaa mpaka Hoima ambako ndiko bomba letu la mafuta litaanzia.
Rais wa Somalia Mohamed Barre aliondolewe (1991), huyu alikuwa ni mjamaa na ni mwaka huo huo USSR ilisambaratika.
Zenawi wa Ethiopia naye aliingia maradakani 1991, na kama ulikuwa hufahamu serikali zote duniani zilizoingia madarakani 1991 zilikuwa supported na west (pamoja na ya Yeltin). Hawa wa Tigrinya (kabila dogo la Ethiopia) ndio walioitawala Ethiopia kwa miaka 30, wakipata support kutoka magharibi. Walijipendelea sehemu zote za serekali na kusababisha kabila kubwa la Oromo kutaka kujitenga.
Rais wa sasa Abiy alipoingia sera yake ilikuwa ni kuiunganisha nchi, Watigrinya wakataka kuiangusha serikali yake lakini kwa masaada wa China na Turkey waliweza kushinda.
Dah, wakati mwingine sielewi kama unatania au la.
Congo toka kuuawa kwa Lumumba imekuwa haitawaliki ili madini yaendelee kutoroshwa. Hivi umesahau muda si mrefu gari la UN lilidondoka na kumwaga madini? Sasa UN na madini wapi na wapi?
Mkuu, haya mawazo ya kuyaona mataifa makubwa ndiyo yenye kuongoza Kila kitu hapa Africa ni mawazo ya kujidhalilisha Sana.
Kwahiyo wewe Kila kitu sisi waafrika hatuna uwezo wa kujisimamia, lazima wageni ndio wawe wanahusika?.
Burundi na Rwanda wamekua na tofauti za kikabila hata kabla ya kuja kwa wakoloni, hapa Tanzania kulikuepo na vita vya kikabila hata kabla ya 1884, Soma historia ya kuja kwa wangoni, Mkwawa, Chifu Mirambo na wengine wengi.
Wazungu walipokuja walikuta tayari tunapigana, walichofanya ni kutumia hizo tofauti zetu kuweza kututawala kwa urahisi zaidi.
Baada ya kupata Uhuru na wazungu kuondoka, nchi nyingi zilirudi katika tofauti zao za kikabila walizokua nazo kabla ya kuja kwa wageni.
Viongozi wengi wa Afrika walitumia tofauti hizo kama walivyofanya wazungu kuweza kupata madaraka na kujilimbikizia Mali, hawakutaka kuunganisha raia wao kwa kuogopa kupoteza vyeo, mfano ni Kenya, Malawi, Rwanda, Burundi na nchi zingine nyingi.
Vita vingi hapa Africa ni migogoro ya ukabila, na siku hizi dini hasa dini ya kiislam, lakini chini yake wanataka madaraka na Mali. Enzi za "Cold war" ndio kulikua na "influencers", na lengo lao kuu halikua Mali, bali ni "Geopolitical influence".
Vita vya Ethiopia, havina mkono wa taifa lolote la nje, Soma historia ya Ethiopia vizuri. Mfalme Hailes Selas alipoingia madarakani, aliifanya Lugha ya kabila lake "Amharic", kuwa ndio Lugha ya Ethiopia, kabila la Oromo ambao ndio wengi, walikasirishwa na kitendo hicho wakaanza uasi dhidi ya serikali, wakaungana na makabila madogo likiwemo "Tigrey", wakampindua, Mangistu akachukua nchi, bado waoromo wakaendelea na uasi Hadi Leo.
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app