Kama serikali, sector zote ni muhimu, utakachokifanya ktk hizo sector lazima pia ukifanye katika sector zingine kwasababu serikali ni mwili mmoja.
Chukua mfano ukiboresha maslahi ya sector ya afya bila kugusia sector za maji na umeme kwa mfano, hizo Hospitali zitafanya kazi?.
Tatizo ni kwamba, serikali inaziangalia sector zote Kama watoto wake, inajaribu kuhakikisha kidogo kinachopatikana kukigawa kwa uwiano ulio mzuri bila kusababisha manung'uniko toka kwa watoto wengine.
Kuhusu kuongezeka kwa gharama za maisha, Kila ongezeko la gharama katika huduma muhimu za jamii inachangia katika kuongezeka kwa gharama za maisha nchini.
Unapoongeza mishahara au marupurupu kwa wafanyakazi wa afya, nani atalipia hilo ongezeko Kama sio wateja wanaotumia hizo huduma?
Mkuu, a reason I said suala la elimu na afya halihitaji siasa kabisa, I understand your positivity, and so am I,
Hizi sekta ni lazima zipewe kipaumbele,
Ukiangalia mishahara ya watumishi wa hIzi sekta kama TANESCO na Mamlaka za Maji za zote za mikoa , ukalinganisha na Wanavyolipwa watumishi wa sekta za afya na elimu ni Mbingu na ardhi, licha ya kuwa watumishi wa afya na elimu wanatumika sana kama punda, plus udharirishaji na matusi juu.
Uwekezaji kwenye sekta za Umeme + Maji ukilinganisha na sekta za afya na elimu ni Mbingu na ardhi,
Hapa sababu kuu ni moja, kwenye Maji na umeme kunazalisha pato, iwe uwekezaji au vyovyote vile wanasiasa wananufaika (Cash Cows) , kuna ulaji huko .
Maana yangu ilikuwa,
1. Serikali iwe serious kuwekeza kwenye elimu, pia zifanyike reforms , maslahi ya wafanyakazi pamoja na mazingira ya kufanyia kazi viboreshwe,
Kusiwe na mtu tena anafeli kisha anaqualify kusomea ualimu akafundishe wengine. Hii pekee inadhihirisha hatupo serious .
Usipokuwa serious na suala la elimu huwezi kuwa serious na chochote .
2. Uwekezaji Sekta ya Afya, isiwe kisiasa, yaani kujenge vituo mobu vya afya na hatuna hata clinical officer hapo, hatuna medical equipments wala medicines, yaani ukiondoa Muhimbili, Ben Mkapa, Aga khan trust me hakuna taasisi nyingine yenye vifaa vya kujitosheleza nchi nzima hii.
How much do we need ( tukiwa na $200m) kwa kuanzia
Tunaweza weka vifaa vya kisasa angalau kwa kiasi kwenye hospitali zetu za mikoa yote 31 (za rufaa)
Kisha tukiwa na wataalam wa kutosha, angalau wenye maslahi ya kujimudu basi we are good to go, later on tunaboresha kwenye eneo la pharmaceutical. Ile pesa ya Covid-19 ilikuwa na uwezo wa kusovu yote haya vizuri kabisa, but where is the money?
Somehow tunaona kuna some will ku train hawa Specialists inaleta mwanga walau tunajua nini cha kufanya,
Mkuu, mshahara wa Medical Doctor aliyehitimu shule ya medicine ya miaka 6 ni around 400$ , hii ni pesa ndogo sana. Ndio unakuta mtu ana practice kama MD kisha ana shmba la matikiti analima pia, malpractice. Graduate aanzie $750
Na graduate mwalimu aanzie $500
This is possible.
Sijajua kama Viongozi wa nchi hii wanajua ni how much billions of $ zinaenda India na ulaya na marekani kwa ajili ya pharmaceuticals, I mean Billions of $ kila mwaka, naijua vema hii sehemu ambayo wengi hawaijui.
Kwani kuna rocket science gani kununua mitambo, kuinstall na kuanza kuzalisha generic molecules ambazo tayari zipo ?
Kazi ya hawa wakemia na wafanasia ni nini ?
Nchi hii ina wafamasia karibu 4000, tunawatumiaje? Kudispense na ku order dawa really?
Bado hatujawa serious