Tony254
JF-Expert Member
- May 11, 2017
- 16,016
- 16,434
coodip1 Hizi gari zinazojiendesha (self-driving cars) huwa zinafanya vizuri sana kwenye expressways kwa sababu hakuna kusimama kwenye junction ili kupisha gari zingine kupita na hakuna bumps, sasa computer inaendesha gari wewe ukiwa umelala usingizi wa pono au ukiwa kwenye online business meeting katika kiti cha nyuma huku computer inaendesha gari. Ila computer haitaweza kuendesha gari safely katika barabara zetu za Kiafrika ambako kunahitaji umakini mwingi kwa maana hapa Kenya usipokuwa makini unaona chokoraa amevuka barabara bila kuangalia, sasa inabidi dereva akanyage breki, au unakuta matatu hapa Kenya zina tabia ya kuchange lanes kiholela bila kujali, sasa inabidi dereva awe makini ili kuzuia kugongana na matatu. Sasa computer sidhani kama itaweza kudeal na hizi unexpected scenarios virahisi, binadamu yuko vizuri kwa kureact haraka hata kwa mambo mapya ila computer lazima ifanyiwe training kutumia AI ili ipate experience ya jinsi ya kunavigate chaotic African roads. Lakini expressway haina hizi chaos eti mtu wa mkokoteni anajaribu kuvuka barabara na mambo mengi ya maajabu yanayoweza kuichanganya computer, expressway iko fully barricaded from the other roads. Hata bumps hakuna kwa hivyo computer haina haja ya kupunguza mwendo katika safari nzima. Nairobi expressway ndio barabara nzuri ukanda huu kwa kutest self-driving cars kwa maana haina distractions nyingi kama bumps, junctions, wavuta mkokoteni, bodaboda anayebadilisha leni viholela holela, matatu zinazobebea abiria njiani, wavuka njia wasiokuwa makini na kadhalika.