Ni kweli mkuu, ila sio kwa Sasa, lazima tuwe na vipaumbele kulingana na "limited resources" tulizonazo, hatuwezi kufanya vyote kwa wakati mmoja.
Hivi Sasa nchi yetu hatuna sababu ya kutumia pesa nyingi kuwekeza kwenye Jeshi eti kwasababu Uganda na Kenya wanatumia zaidi ya $1.2B katika Jeshi, mipaka Yao haipo salama Sana ukilinganisha na Tanzania.
Kwasasa, tunaweza kudhibiti usalama wa ndani kwa kutumia polisi, hivi Sasa kwa amani, Tanzania ni nchi ya 7 Afrika na 54 duniani kwa amani na usalama, Kenya duniani ni namba 125 na Afrika ipo chini Sana.
Hivi Sasa Kenya Amani ni tatizo kubwa, wanahitaji kuweka ni kipaumbele cha kwanza katika bajeti zao, huku kwetu usalama sio tatizo Sana kwa Sasa, tunayo matatizo ambayo yanahitaji "immediate action", huko ndio tunapaswa kuelekeza nguvu zetu, CCTV ni sawa, lakini sio huo mfumo mzima, Bora tuwekee katika kudhibiti ajali kwasababu ni tatizo kubwa kwa Sasa.
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app