Tony sidhani kama unaufahamu mzuri wa haya mambo. Unaposema kuwa python ni ngumu kuliko C++ unamaanisha nini?
Python ni very high level programming language kuliko C++, ikimaanisha kuwa imerahisishwa sana. Concepts kama pointers ambazo zipo kwenye C na C++ huwa hazipo kwenye python. Kwa lugha rahisi python ni kama gari yenye automatic gear wakati C na C++ ni ile yenye manual gear.
Zamani ni subjective. Sisi wengine tulianza na C, na mpaka leo C inatumika sana, hiyo simu yako microchips zake zina run C.
Kinadharia unaweza kuprogram kitu chochote kwa language yoyote (Turing computability) lakini kuna baadhi ya language zinafaa zaidi kwa masuala fulani (mf. web vs automotive)
Python huwa na limitations inapokuja kwenye microcontrollers programming ambapo memory iliyopo kwenye chip huwa ni ndogo sana. Kwa kutumia C++ na hasa C unaweza kutumia memory hiyo ndogo kwa ufanisi zaidi.
C++ ilikuwepo kabla ya C-sharp bro.