Kwa miaka mitano GDP iliongezeka zaid ukilinganisha na miaka yote ya nyuma, najua ww mafiii ulikuw hujui,2005 ilikuwa 18+ bill, kikwete akapeka 47 billions (10yrs),JPM 65(5yrs)....do the math
Ni Maoni yako,mimi nilikuwa anti awamu ya 5 toka day 1 na ntaendelea kuwa hivyo Kwa sababu Kwa Imani yangu miaka 6, statistics za Uchumi na parameters zote zinaonyesha tumerudi nyuma kulinganisha na hapo awali.
Yaani una execute utopian policies in modern world? Kinachoelezwa kufanyika kwangu ni kidogo kuliko kilichostahili.Sekta ya Real estate ilikufa kabisa, miradi mingi imefanyika chini ya kiwango ikiwemo Bwawa la Nyerere,Udsm hostel,majengo ya serikali nk.
Hakuna mtu aliweza kuibua uozo wala kuhoji,ukithubutu unapotezea as opposed to six phase government.Kila.siku ilikuwa ni mikwaruzano na majirani hususani Kenya,ikapelekea Mazao mengi ya kilimo ku collapse bei zake.
Ndio sababu ya matumizi ya nguvu na propaganda Sana kwa tu vitu tudogo.Imagine Rais anafunga safari ya kwenda kuzindua mradi wa bil.1 Ili afanye propaganda kwa wajinga.
Masheria mengi ya kipumbavu yalitungwa ambayo tunaanza kubadili tena Ili tuu kulinda uozo.
Yule jamaa kawatia watu jela afu wanaenda kunegotiate kwa pesa Ili wakuachie,kupora wafanyabiashara pesa na upuuzi mwingine.Anajua kutumia pesa ila kutafuta hajui.
Mwendazake angeendelea saizi tungeshakuwa Zimbabwe nyingine.Yeye badala arekebishe mapungufu ya JK anaanza kufanya crackdown tena kwa mihemko ya kijinga.
Enzi za Jakaya Tulikuwa tumefika mahala kuamini private sector kwenye kutoa ajira,tuliacha Kazi za serikali tukaenda kujiajiri but zama za Mwendazake ikawa kinyume,ukikosa Kazi ya serikyunajibanza kuwa machinga na worse enough ajira zilikuwa kiduchu Sana kwa kisingizio cha miradi.Kila mtu akawa Machinga kwa kukata tamaa,na hao wakawa wanalipishwa vitambulisho.
Mbona saizi ajira zinatoka na miradi inaenda? Wenye chuki wamekuja na chorus ya wafanyakazi hewa mara sijui anapendelea kwao na nonsense zingine..
Laiti Samia angekumbatia sera za kipuuzi kwenye uchumi ningempinga directly kama nilivyofanya kwa Mwendazake.
Yani ww hutaa kaaa kuacha kuwa mafiiiii



daima
Ni kweli kipindi cha JPM sector ya real estate ili shuka , na sababu kubwa zikiwa ni kupungua kwa ufisadi na kukemewa kwa wawekezaji wa kigen juu ya kufanya vitu kihuni, pia kufwatilia kwa kodi wakati watu walikuw wanaishi kijanja janja ili liliua biashara nyingi,
Lakini hayo hayakuzui uchumi wa Tz sababu hii nchi sio nchi ya kutegemea private sector kwa kiasi kikubwa kutokana na kuwepo na abandonce ya natural resorces such as minerals ( uraniun, titanium, helium, diamond, gold ,iron, to list a few),ges ,vyanzo vya maji mito, maziwa, bahari, Tourism,strategic location hivi vitu vinategemea zaidi kuwepo kwa serikali mahiri ili vitu kuweza kusonga mfano, JPM alivyo tumia excuse ya kuibiwa madin kuweza kubadili sheria za madini nikitu kitakacho isaidia sana hii nchi ila sio kwa mpuzi kama ww,
Kiuchumi kuna njia mbili za kucontrol economy which is fiscal policy(goverment)and monetary policy(bank(BOT)), hizi sera mbili serikali ndio inachagua ni ipi bora kutokana na hali ya uchumi kwa wakat husik.Serikal ya awamu ya tano ilitumia sana fiscal policy na pia JPM aliamini zaidi utajiri ulipo nchin kuliko kwenda kuwakomba mabeberu kitu kilicho pelekea mikwaruzo ya mara kwa mara, mfano yulinyimwa mikopo kadhaa pia kufanyiwa nakisi za uongo ili tu kutushusha ili turudi kuwa lilia ila mzee alikuw naroho ya paka.
Pamoja na setback alizopata toka njee bado alikuw na ushawishi wake uliongezeka sio tu ndani bali mpaka njee juu ya determination yake kwenye kazi mfano alikuwa ni rais wa visions kubwa kubwa wakati wote mfano ni aina ya miradi aliyo ianzisha ilio onekana impossible kama bwawa la Nyerere,mradi wa electrified SGR( wengi tulion analeta uwazim)nw kufufua reli ya zaman,kufufua shirika la ndege tulikuw loughing stock pia upanuzi na ujenzi wa viwanja vipya,kuamisha makao makuu ya serikali, ujenzi wa meli maziw yote,upanuzi wa bandari na kujenga mpya,sector ya Afya ndio alizid kufanya kufuru kwa kuongeza referal hospitals Mtwara, Mbeya na Dodoma huku vituo vya afya pia ,kufanikiw kurudisha ushawishi wa Tz kwenye jumuhiya za SADC na EAC kitu kilicho pelekea kuongezeka kwa ushirikiano ndani ya jumuiya hizi na faida moja wapo ni kupata bomba la mafuta,sector ya elimu alifanya vyema hasa kwa sera ya elimu bure na kuongeza madawati na madarasa
Pamoja na mazuri mengi bado kulikuw na madhaifu wakati wa uongozi wa JPM hasa kwenye upande wa siasa tukio kama la kushambuliwa kwa Lissu, kudhohofik kwa upinzani lakin nikiweka kwenye mizan ni dhahiri uongozi wake ulikuwaa na matokeo chanya zaidi kuliko madhaifu yake.