Mimi kusema kweli sikuwa na tatizo na awamu iliyopita na hata Posts zangu humu zinaonyesha hivyo mpaka pale nilipogundua wafuasi kindakindaki wa JPM ambao hawana staha na hawaheshimu mawazo ya wengine! Pia wanaamini wao tu ndo wanastahili maendeleo.
Ni Maoni yako,mimi nilikuwa anti awamu ya 5 toka day 1 na ntaendelea kuwa hivyo Kwa sababu Kwa Imani yangu miaka 6, statistics za Uchumi na parameters zote zinaonyesha tumerudi nyuma kulinganisha na hapo awali.
Yaani una execute utopian policies in modern world? Kinachoelezwa kufanyika kwangu ni kidogo kuliko kilichostahili.Sekta ya Real estate ilikufa kabisa, miradi mingi imefanyika chini ya kiwango ikiwemo Bwawa la Nyerere,Udsm hostel,majengo ya serikali nk.
Hakuna mtu aliweza kuibua uozo wala kuhoji,ukithubutu unapotezea as opposed to six phase government.Kila.siku ilikuwa ni mikwaruzano na majirani hususani Kenya,ikapelekea Mazao mengi ya kilimo ku collapse bei zake.
Ndio sababu ya matumizi ya nguvu na propaganda Sana kwa tu vitu tudogo.Imagine Rais anafunga safari ya kwenda kuzindua mradi wa bil.1 Ili afanye propaganda kwa wajinga.
Masheria mengi ya kipumbavu yalitungwa ambayo tunaanza kubadili tena Ili tuu kulinda uozo.
Yule jamaa kawatia watu jela afu wanaenda kunegotiate kwa pesa Ili wakuachie,kupora wafanyabiashara pesa na upuuzi mwingine.Anajua kutumia pesa ila kutafuta hajui.
Mwendazake angeendelea saizi tungeshakuwa Zimbabwe nyingine.Yeye badala arekebishe mapungufu ya JK anaanza kufanya crackdown tena kwa mihemko ya kijinga.
Enzi za Jakaya Tulikuwa tumefika mahala kuamini private sector kwenye kutoa ajira,tuliacha Kazi za serikali tukaenda kujiajiri but zama za Mwendazake ikawa kinyume,ukikosa Kazi ya serikyunajibanza kuwa machinga na worse enough ajira zilikuwa kiduchu Sana kwa kisingizio cha miradi.Kila mtu akawa Machinga kwa kukata tamaa,na hao wakawa wanalipishwa vitambulisho.
Mbona saizi ajira zinatoka na miradi inaenda? Wenye chuki wamekuja na chorus ya wafanyakazi hewa mara sijui anapendelea kwao na nonsense zingine..
Laiti Samia angekumbatia sera za kipuuzi kwenye uchumi ningempinga directly kama nilivyofanya kwa Mwendazake.