Wacha mimi nimeenda. Tutaonana siku nyingine. Huwa nakubali kwamba Tanzania imepiga hatua kubwa sana kwenye maendeleo ikiwemo ujenzi wa madaraja, barabara, reli ya SGR ya umeme na JNHPP. Tanzania sio nchi ndogo na sio nchi ya kupuuzwa hata kidogo. Hususan miradi ya JNHPP na SGR zikikamilika basi Tanzania mtakuwa mbali sana kwa sababu miradi hizi zitasisimua (stimulate) uchumi wenu sana. Hapa JPM alikuwa anawaza long-term kwa maana miradi hizi mtapata manufaa yao baadaye. Nchi yenu inakuwa kwa kasi mno na itaendelea kukua kwa kasi. Lakini sioni ni kwa nini nyie Wabongo mjifanye kwamba hamuoni ukubwa wa uchumi wa Kenya ilhali watu wengi Africa wanaweza kuiona, hata wazungu wanaokuja kuweka headquarters ya kila kitu Kenya na sio Tanzania wanajua hilo. Hakuna tatizo mkikubali kwamba uchumi wa Kenya ni mkubwa, hamtapungukiwa na chochote. Vile vile mimi nasifia uchumi wenu kwa sababu uchumi wenu pia ni mkubwa na unakuwa kwa haraka sanaa. Mimi kwa kuwasifu sijapungukiwa na chochote. Hamna haja ya nyie kuamini kwamba Kenya ina uchumi mdogo wakati hata data ambazo zinatolewa na taasisi ambazo zipo independent kama World Bank, Imf, UN, Afdb, WEF, CIA, OECD zote zinasema kwamba Kenya ndio nchi yenye uchumi mkubwa ukanda huu. Hizi taasisi zote zimehongwa na serikali ya Kenya kueneza uongo huu? Kwani serikali ya Kenya ina pesa nyingi sana vipi ya kuhonga taasisi zote hizi?