Sama boy 255 Wacha niongeze kidogo kwamba Kenya imewapiga kwenye idadi ya abiria wanaopitia kwenye airports. Kenya ina service sector kubwa kushinda yenu. Kwa mfano Kenya ina makampuni kubwa kushinda zenu hata tukiangalia banks, banks za Kenya ni kubwa ajabu ukizilinganisha na banks za TZ ambazo ni ndogo sana. KCB, EQUITY na Co-operative banks zina more capital kushinda banks zenu zote na ukumbuke kwamba Kenya ina banks 44 ilhali banks tatu zetu zina more capital kushinda zenu zote. Tukija kwenye telecomm sector, Safaricom pekee ina bigger valuation kushinda kampuni zenu zote za telecomm. Hizi data nipo tayari kumwaga huku. Yaani kampuni za kininafsi za Kenya ni kubwa sana ukizilinganisha na zenu. Kwenye kuexport tea, flowers, coffee, textiles na vegetables tumewapiga. Kenya tunaconsume more electricity na more petroleum products kuwashinda. Kenya tunaimport more goods kuwashinda kumaanisha tunaconsume more goods kuwashinda. Kwa mfano Kenya inaimport goods worth 14 billion dollars kila mwaka wakati nyie mnaimport goods worth 9 billion dollars kila mwaka.
Hizi data zote zinaonyesha kwamba uchumi wa Kenya ni mkubwa kushinda wenu. Service sector ni zaidi ya 50% ya uchumi wa Kenya kwa hivyo Kenya ni service driven economy wakati nyie ni agriculture and mining driven economy. Sie mining industry yetu ni ndogo sana. Yaani kuna mambo mumetupiga lakini sie pia tumewapiga vibaya sana kwenye mambo mengine, hususan private sector yetu ambayo inawafunika vibaya sana. Kumbuka Kenya ndio nchi ya pili kwenye kuinvest hapo Tanzania na top three kwa kuinvest Uganda. Sasa hivi makampuni ya Kenya yanaivest Ethiopia ikiwemo Safaricom na Kengen. Mabenki za Kenya zipo katika nchi zaidi ya saba ukanda huu. Sasa sijui mnaidharau Kenya kwa nini. Hata kwenye diplomasia, Kenya ina embassies zaidi ya mia moja na kuna baadhi ya hizi embassies ambazo hazipo Tanzania. UN global headquarters ya UNEP na UN habitat ipo Kenya. World Bank na IMF regional headquarters ipo Kenya. Google, microsoft, IBM, Oracle regional headquarters zipo Kenya. Al-jazeera, BBC, Xinhua, CGTN regional au African headquarters zipo Kenya. Ikumbukwe Kenya ina skyscrapers nyingi above 100 metres kushinda Tanzania. Hata tu kwenye picha zinazowekwa humu ni wazi kwamba Kenya ina apartments nyingi kushinda Tanzania. Kenya ina watu wengi wanaofanya kazi Marekani na nchi za ulaya kushinda Tanzania. N.k. Niendelee au niwachie hapo?