Ikumbukwe kwamba sababu kubwa ya WB kukataa kutoa pesa ya kujenga SGR ya Tanzania ni kwasababu ya kuwepo kwa reli ya zamani, wao walisema ni bora kuiboresha reli ya zamani iwe ya kisasa na kuweka umeme kuliko kuwa na reli mbili zinazokwenda sehemu moja.
Hivi kweli kabisa kwa akili ya kawaida tujenge tena SGR parallel na hii iliyopo ya TANGA arusha, wakati hii iliyopo tukiweka umeme na kuiboresha kama tulivyofanya hii ya Central corridor na kununua train za kisasa za umeme inatosha?, hata huko Ulaya na Marekani pia wengi hawajaeneza mitandao ya SGR, kwa utajiri gani tuliona Tanzania wa kujenga mtandao wa reli hata katika njia ambazo tayari reli zipo?.
Tuacheni kuwa "over ambitious", SGR ijengwe kule ambako hakuna reli tunaanza upya, lakini kule ambako tayari kuna reli, tuboreshe na kuweka umeme na kununua trains za kisasa.
Sent from my TECNO-L8 using
JamiiForums mobile app