Usifananishe Jubilee na awamu ya tano.
Faida za kiuchumi siyo lazima zipatikane leo, reli ina maisha marefu (zaidi ya miaka 100). Kumbuka zaidi ya 65% ya watanzania ni chini ya miaka 20, hawa wote wakija kuzaa hapata kalika. Population kubwa kwenye nchi yenye miundombinu ya reli ni mlinganyo unaotengeneza uchumi mkubwa. Angalia maendeleo ya haraka ya Marekani (19th c) na majuzi hapa China (2003 -2013), utaona yanaenda sambamba na km za reli walizojenga.
Miundombinu ni kila kitu kaka, Jeff Bezos asingekuwa na 200Billions leo na kuajiri maelfu ya watu, pamoja na kuwezesha biashara nyingi, kama isingekuwa miundombinu madhubuti ya posta ya Marekani (USPS, moja ya kitengo cha kwanza kabisa kuanzishwa). Hivyo faida za ujenzi wa reli unaweza usiione moja kwa moja ila ki ujumla ni maradufu ya gharama za ujenzi.