Arusha: Wanne wadaiwa kufariki dunia baada ya Noah kusombwa na maji ikijaribu kuvuka barabara iliyofunikwa na maji

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358

KIA 3.jpg

Hii ni ile noah iliyozama ilikuwa na watu sita wawili wamepona, watatu wamepatikana wamefariki, mtoto mmoja hajaonekana sijui kapelekwa na maji hadi wapi

=======

Watu wanne wamepoteza Maisha na wengine wawili kunusurika kufa baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya NOAH T 499 DMY kusombwa na waji katika eneo la Malalula Kata ya King'ori wilayani Arumeru wakitokea Arusha kuelekea Kilimanjaro.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Emmanuela Kaganda amewaambia waandishi wa habari waliofika katika eneo hilo kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa mbili na dakika arobaini asubuhi wakati dereva wa gari hilo Naimani Metili ambae ndio baba akiwa na abiria watano wakielekea katika mahafali ya mtoto wao Moshi.
 
Kuna watu akili zao sijui vipi?
We una familia nzima ndani ya gari unalidumbukiza kwenye maji kasi unaiona,
Si hata angewashusha au kusubiri mkondo wa maji upungue?
Sasa familia nzima ishakufa watu sita.
ndugu km kawaida wataanza kugombea Mali tu.
Mlikua mnawai wapi?
Si mngesubiri, au nenda wewe jemedari na gari yako
Utumbukie humo,
unabwaga familia nzima ndani ya maji.
Inasikitisha sana
Habari iko TBC Jioni hii
 
Inasikitisha mno kwa ajali kama hii ambayo ingeweza kuzuilika,ila RPC &RTO wa mkoa huu hii ajali ni uzembe wenu, why hamkuweka kizuizi pale ili kuhakikisha hakuna gari inayopita pale?,why hamkutuma traffic officer's ili waweke road block pale?,na msinijibu kuwa hakuna officer's wa kutosha, juzi kati nilihesabu check points kati ya Dar na Moro, na maafisa wanaozisimamia, 15checkbpoints, 30officials!! hii ni craze
 
Walikuwa wanaenda kweny mahafali ya ndugu yao wa kidato cha sita huko Kilimanjaro kwa kweli roho imeniuma sana.
Wangeghairi tu yale maji unaona kabisa yalikua na nguvu kiasi huwezi kuvuka pale.
Anyway mungu awalaze wanapostahili.
 
Back
Top Bottom