"P Mkuu P, somo la Karma ni pana sana.
Karma haijitokezi kama watu wanavyotarajia, hujitokeza kwa namna nyingi na tofauti sana.
Mfano 1: Marekani mtu aliua mkewe na kumzika uani. Imepita miaka zaidi ya 20 hakuna aliyejua nini kilitokea.
Nyumba imeuzwa, mnunuzi akaamua kuchimba uani katika kutengeneza na kuimarisha nyumba yake.
Alikutana na mabaki ya marehemu, uchunguzi ukabaini mumewe alimuua. Karma ikajitokeza jamaa kanaswa.
Mkuu Nguruvi 3, kwanza ni kweli karma haijitokezi direct pale kwa pale na sometimes wewe unaweza kutenda maovu na ukafa vizuri bila kufidia, lakini kikaja kulipa kizazi chako hadi cha 4!, 4th generation!.
Kwa huyo mtu aliyeua mkewe, hakuna mtu aliyekuwa ana keep track aliishi maisha gazi hiyo miaka 20, take it from me, his life was a living hell!, sio watu wote wamejaaliwa kuona ndani ya mioyo ya watu, lakini mimi nawafahamu matajiri wengi tuu, wana furaha machoni lakini huzuni moyoni, hata smile zao, cheka zao ni just superficial, wana kila kitu and yet they are living hell!.
Mfano 2. Same Kilimanjaro kuna tukio la mtu aliyepotea baada ya kuchukua mafao yake.
Mkewe alipofariki akataka azikwe eneo X. Wakachimba pale pale mumewe alipozikwa.
Ikabainika aliyetenda unyama ni mwanae miaka zaidi ya 10.
Mama kutaka azikwe eneo X ilikuwa ni 'Karma' ili mwanae inamrudi leo hii.
Hapa nikama tukio la kwanza, hakuna mtu aliye keep track ya maisha ya huyo kijana katika miaka hiyo 10 baada ya kuua baba yake!. He was living hell!.
Hakuna aliyeuliza kwa mama why alichagua azikwe pale?, kupitia life after life, baba kule alipozikwa alimtokea mama ndotoni akamuamsha na kumpeleka kwa astral travel, mama akaona baba alipo, mama akaelekeza nikifa nizikwe pale, baba akamuita mama aje, akaitika, akaenda, wao wakaendelea na mapenzi yao kwenye ulimwengu wa roho.
Wanabodi, Kifo cha Ephraim Kibonde kimeibua simanzi kubwa kwa sababu katika uhai wake hakuwahi kuugua, amekufa ghafla, hivyo watu kubaki na maswali mengi. Katika bandiko la Tribute to Kibonde, kuna mwana JF kaandika maneno haya kumhusu Kibonde. Sikumfahamu zaidi ya kumuona kwenye Mkasi...
Mfano 3; Marekani kuna wimbi la askari kupata matatizo wakiyaita PSTD(Post stress traumatic disorder)
Idadi ya askari wanaojiua kila siku inaongezeka na hata kuwa ''janga''. Je, hii si karma ? Amri halali ndiyo subject hapa.Vitani ni amri halali.
Miaka yangu, ulikuwa ukimaliza A level unakwenda JKT kwa mujibu wa sheria, mimi nilikuwa bingwa wa paredi na shabaha, nikachaguliwa moja kwa moja kujinga na JWTZ straight from JKT, hivyo nikapiga deppo mpya ya JW pale Airwing kabla ya kwenda Cadet Monduli, sasa kwenye somo la mbinu za medani, kuna kitu kinachoitwa "initiative", mkishambuliwa, mkijikuta wenzako wameumia sana, huwezi kusaidia na unatakiwa ku retreat, au atakufa kwa mateso, unatakiwa wewe kuwaalizia bila huruma ili kuwapunguzia mateso, askari wote wanaofanya mauaji ya kikatili hiyo au hata kushuhudia tuu ukatili wa ajabu, ndio huja kupata PSTD, hiyo sio karma bali ni guilt conscious.
Ukiua vitani vifo halali hakuna karma, ila kuna wale wanaovamia kijiji, wana ua wanaume wote, wana rape wanawake kisha kuwaua, kisha wanamalizia kuua vitoto, ili visiteseke, kwenye vita vya Kagera, majeshi yetu pia yalifanya unyama huo Uganda, Generali Ernest Mwita Kiaro, wakati huo akiwa Major General, alikuokoa kitoto kimoja cha Kiganda baada ya wazazi wake kuuliwa na kikosi chake, askari wake wakataka kukimalizia, akatoa amri ya stop, akakichukua kitoto kile na kukipeleka kwake.
Akakipa jina na kutumia ubini wake, amini usiamini, kilikuja kuwa a very rich guy in town, kimemuoa mtoto wa rais, kina roho nzuri hakuna mfano!. Marwa akabarikiwa hadi kuwa CDF na ni darasa la 8 tuu la mkoloni!.
Mnyongaji anatenda kwa amri halali tena mchana kweupe baada ya process nzima ya uhalali kufanyika.
Wanaokabiliwa na adhabu ya kunyongwa kamwe hawalaumu wanaotimiza wajibu.Ni amri halali.
Swali, amri halali mipaka yake ni ipi?
Kuna sababu inaitwa halali, kwa maana imepitia hatua halali, imeelezwa kihalali, imeidhinishwa kihalali.
Hata vitani kuna kitu kinaitwa ''rule of engagement' kwamba, kuna abcd za kufanya na kutofanya.
Uwepo wa 'rule of engagement' unalenga kuhakikisha askari wanatimiza amri halali kama ilivyoelezwa.
Kwahiyo amri halali ina namna zake na mipaka yake si ''open season''
Amri halali ni amri yoyote unayopewa na mkubwa wako, kijeshi usihoji. Kwenye ile idara ya wale jamaa zetu, kuna kitengo kabisa cha covet operations, kinafanya eliminations na kina ma snipers wenye shabaha ajabu, ndio maana nikasema kama wangekuwa ni wale jamaa zetu kwenye tukio la Lissu, wasinge fanya such mercy dirty job!, they have 100 ways plus za kufanya a clean job hata accident look a like na watu wasijue!. Hili nimelieleza vizuri hapa
Wanabodi, Tangu kutokea kwa shambulizi kwa Mhe.Tundu Lissu, ambalo mpaka sasa linaelezwa kufanywa na watu wasiojulikana, kumeibuka shauku kubwa ya watu kutaka kuwabaini hawa watu wanaoitwa ni watu wasiojulikana, ni kina nani?, wanatumwa na nani? na lengo lao ni nini?, kunakopelekea kujengwa kwa...
Mkuu P huku mitaani watu hujitoa katika baadhi ya maamuzi ya Familia au Ndugu yenye utata.
Kauli kubwa unayoisikia ni moja '' wana nawa mikono yao'', kwa maana wanajiepusha na ''karma''
Hoja yangu hapa ni maoni tu ya jumla juu ya Karma. Hailengi kuhusu tukio au watu kwa namna yoyote
Its true watu wengi hujitoa kwa kunawa mikono kuepuka karma, hata Pilato alinawa mikono kabla ya kumhukumu YESU hii haiondoi karma!, pia nilishikwa sikio, kuna mtu alisulubiwa kwasabu ya kunawa mikono kwa tukio la Lissu, naomba msiniulize nani!.
P