Wananchi wa Morogoro hususani wafanyabiashara wa Morogoro eneo la Msamvu leo waliungana na wanachadema kupokea salamu za Tundu Lissu. Makamu wa mwenyekiti Chadema na Mgonbea Urasi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi Mkuu 2020 alisimama kwa muda na kusalimiana na mamia ya wafanyabiashara eneo la Stendi kuu ya Msamvu. Akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi bila ya viongozi wenzake wa kitaifa aliwaambia wananchi wa Morogoro kuwa naelekea nyumbani Ikungi kuwaonesha makovu ya risasi na kunywa maziwa nyumbani Ikungi. Aliwaahidi kurudi na kufanya ziara mkoani humo. Aidha mgonbea ubunge wa Morogoro mjini wa uchaguzi wa mwaka 2020 na mtangazaji wa zamani wa ITV Devota Minja ndiye aliyekuwa mwrnyeji wake. Picha zitafuata.