ALICHOKIZUNGUMZA MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA BANDARI TANZANIA (TPA)PLASDUCE MBOSSA, KWENYE MAHOJIANO NA TBC
“Bandari ya DSM iko kwenye hatua ya kufanyiwa maboresho, na utaratibu wa kutafuta kampuni kuendesha bandari ni utaratibu wa kawaida na tulikua na kampuni inaitwa TICS ambayo mkataba wake umeisha Disemba 2022, na sasa tumeanza hatua nyingine za kuboresha zaidi"
"TPA bado haijasaini Mkataba na kampuni yeyote, Mkataba uliosainiwa ni kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai ni kuhusu ushirikiano kwenye masuala ya bandari kuhusu tehama, mafunzo ya uendelezaji na uendeshaji wa bandari, baada ya hapo ndiyo kutakua na mikataba ya utekelezaji"
“Kinachoongelewa sasa mtandaoni ni mikataba ya utekelezaji ambayo bado haijadiliwa na wala haijasainiwa, kwa mtu anayesema kuna mwekezaji kapewa miaka 100, atakua anatatizo kidogo hakuna nyaraka yeyote iliyosema tumesaini miaka 100."
"Kilichosainiwa ni Framework Agreament baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai halafu baadaye kutakua na mikataba ya utekeleza kati ya Serikali na Kampuni ambao Mkataba wa Uwekezaji, halafu kutakua na mikataba ya uendeshaji kwa hiyo sasa hivi ni mapema sana kusema atakaa miaka mingapi au atapewa eneo gani"
“Sisi tuna gati 12 na kila gati Kwa wastani tunakua na Meli 10, lakini kila wakati tunakua na meli zaidi ya 20 zinazosubiri na huwa wanatuchaji gharama za kusubiri unaweza kulipa mpaka Dola 3000, sasa lazima tuchukue hatua za kumaliza tatizo kwa kutafuta mwekezaji ambaye anaweza kumaliza hali hii"
“Kampuni ambayo itapewa nafasi ya kuendesha lazima itakua na na uzoefu wa kufanya hii kazi, iwe na mahusiano mazuri bandari kavu za nchi za jirani lakini muhimu zaidi iwe na mahusiano mazuri na Makampuni mengi ya Meli Duniani"
SOURCE: TBC - ARIDHIO
“Bandari ya DSM iko kwenye hatua ya kufanyiwa maboresho, na utaratibu wa kutafuta kampuni kuendesha bandari ni utaratibu wa kawaida na tulikua na kampuni inaitwa TICS ambayo mkataba wake umeisha Disemba 2022, na sasa tumeanza hatua nyingine za kuboresha zaidi"
"TPA bado haijasaini Mkataba na kampuni yeyote, Mkataba uliosainiwa ni kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai ni kuhusu ushirikiano kwenye masuala ya bandari kuhusu tehama, mafunzo ya uendelezaji na uendeshaji wa bandari, baada ya hapo ndiyo kutakua na mikataba ya utekelezaji"
“Kinachoongelewa sasa mtandaoni ni mikataba ya utekelezaji ambayo bado haijadiliwa na wala haijasainiwa, kwa mtu anayesema kuna mwekezaji kapewa miaka 100, atakua anatatizo kidogo hakuna nyaraka yeyote iliyosema tumesaini miaka 100."
"Kilichosainiwa ni Framework Agreament baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai halafu baadaye kutakua na mikataba ya utekeleza kati ya Serikali na Kampuni ambao Mkataba wa Uwekezaji, halafu kutakua na mikataba ya uendeshaji kwa hiyo sasa hivi ni mapema sana kusema atakaa miaka mingapi au atapewa eneo gani"
“Sisi tuna gati 12 na kila gati Kwa wastani tunakua na Meli 10, lakini kila wakati tunakua na meli zaidi ya 20 zinazosubiri na huwa wanatuchaji gharama za kusubiri unaweza kulipa mpaka Dola 3000, sasa lazima tuchukue hatua za kumaliza tatizo kwa kutafuta mwekezaji ambaye anaweza kumaliza hali hii"
“Kampuni ambayo itapewa nafasi ya kuendesha lazima itakua na na uzoefu wa kufanya hii kazi, iwe na mahusiano mazuri bandari kavu za nchi za jirani lakini muhimu zaidi iwe na mahusiano mazuri na Makampuni mengi ya Meli Duniani"
SOURCE: TBC - ARIDHIO