tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. Analogia Malenga

    Mwaka 2019 Kamati ya Malalamiko ya TCRA iliitaka Vodacom imlipe mteja Faini ya Tsh. Milioni 1.2 kwa kufanya SIM swap kiholela

    Bahati Mekene alipeleka malalamiko katika kamati ya malalamiko ya TCRA kuhusu Vodacom kufanya swap ya laini yake ambapo ilimletea shida hata kwenye mahusiano yake kwani aliashindwa kuendelea na mpenzi wake baada ya mwenza wake huyo kupiga simu na kupokelewa na mwanaume. Tukio hili lilitokea...
  2. mshale21

    TCRA: Hatujakataza matumizi ya VPN bali ni kusajili na kutoa taarifa ya matumizi ya VPN

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia kwa Mkuu wake wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Rolf Kibaja imesema taarifa kwa Umma iliyotolewa juzi October 13,2023 haijakataza matumizi ya VPN kama baadhi ya Watu wanayopotosha kupitia mitandao ya kijamii. Kibaja ameiambia Ayo TV...
  3. Nobunaga

    TCRA hili la VPN nalo litawashinda kwa sababu hamtaki kuukabili uhalisia wa mambo

    Swali kwa TCRA: Mnajua sababu ya matumizi ya VPN kuwa makubwa nchini? Uhalisia ulivyo: Kwenye teknolojia ukiwabinya sana wananchi pale, wao wanatokea kule kwa sababu ya kukua kwa teknolojia kila siku, kila kitu kina option B. Katika mambo ambayo serikali ilikuwa haijawahi kuwaza basi ni...
  4. ACT Wazalendo

    Macheyeki: Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini

    Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini. Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network)...
  5. G

    TCRA angalieni Airtel wanavyowaibia wateja

    Leo nimepiga simu airtel huduma kwa wateja kupitia namba 100 kama wenyewe wanavyoelekeza. Ajabu hadi dakika 10 zinakwisha, sijaunganishwa na mtoa huduma, napewa tu maelekezo, bonyeza 1, mara bonyeza 6. Baada ya maelekezo hayo, napata sms kuwa nimetumia dakika 10, na kweli dakika 10 hizo...
  6. S

    Je, TCRA wana mamlaka yoyote ya kutunga sheria?

    Naomba kufahamu kwa wajuvi wa sheria hapa JF. TCRA ni taasisi inayosimamia mawasiliano hapa TZ. Je hawa watu wanahusika na kutunga sheria? Mfano ni kuhusu hili suala la VPN
  7. M

    TCRA watakagua simu za Watanzania wote kuwajua wanaotumia VPN?

    Nimeona katazo la Tcra kuzuia matumizi ya Vpn nakusema kuwa kuna faini ya mil 5. Sasa kwa sababu karibu kila Mtanzania mwenye smart foni amedownload VPN na anaitumia kuangalia mambo yake binafsi ya kifaragha . Je, TCRA itawag'amua vipi watu wakiwa na simu zao mkononi. Msaada wa kitalaamu
  8. Cannabis

    TCRA: Ukikutwa unatumia VPN Tanzania, faini milioni 5, kifungo mwaka mmoja

    Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) imewataka wananchi na makampuni kiujumla ambazo kwa asili ya kazi zao hawawezi kuepuka matumizi ya VPN kutoa taarifa juu ya VPN wanazotumia na taarifa muhimu kabla ya Oktoba 30 mwaka huu. Aidha mamlaka hiyo imesema iwapo itabainika umetumia VPN kinyume na kanuni...
  9. MSAGA SUMU

    Chadema tuwahi TCRA kuzuia leseni ya Nape

    Tuna siku 14 pekoe, japo kuwa hatuna sababu ya muhimu twendeni kuizuia hivyohivyo.
  10. Analogia Malenga

    TCRA bado mnaendelea kufanya kosa kwenye jina lenu

    TCRA mimi ni mtumiaji wa takwimu zenu, ila angalieni ripoti zenu nyingi mnakosea jina lenu, badala ya kuwa "Authority" mnajiita "Authory" hii inanipa mashaka kama data mnazotoa ziko sahihi ikiwa jina lenu tu mnakosea. Ripoti ya June 2023, mmejiita "Authory" June 2022, mmejiita "Authory"...
  11. GENTAMYCINE

    TCRA mmebariki huu Upuuzi wa Viongozi wa Timu za Ndondo Cup Kusifia kufanya Ushirikina Mubashara Redioni Clouds FM?

    "Hela tuliyopata tumeenda kununua Mayai Viza, Kuku Mweusi na Udi na kumpelekea Mganga wetu wa Kienyeji na kwa jinsi tunavyoenda Kuwaroga Watatukoma" Shabiki wa Timu Moja inayoshiriki Michuano iliyosifiwa na inayosapotiwa na Rais wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ya Ndondo Cup' kwa Mikoa...
  12. S

    TCRA kuufungia wimbo "Amkeni" wa Ney wa Mitego na kuacha nyimbo za matusi ni uchawa, kujipendekeza na unafiki

    TCRA acheni kutumika vibaya. Mmeufungia wimbo wa Ney Wamitego "Amkeni" kwasababu tu umemparura aliyewateua lkn mmeacha nyimbo kibao za matusi zkiendelee kwenda hewani. .....sijui kutongoza.... .....ikiiingia inateleza.. ....paka mate niteleze.. .....nampatia sukari ananambia ongeza.. n.k, n.k...
  13. Hismastersvoice

    TCRA, hivi kwanini hamtulindi wananchi dhidi ya dhuluma? Badala yake mpo kwa kutukandamiza!

    Nilinunua kifurushi cha wiki cha Airtel nikiwa safarini Marangu Moshi, nilipofika nikakuta Airtel haipatikani hivyo kifurushi kikaisha kwa muda niliokuwepo hapo! TCRA wao wanajionea sawa tu. Nilitika Marangu nikaenda Moshi mjini eneo la KCMC ah! Nako ni shida tu mpaka mwenyeji akuelekeze...
  14. NostradamusEstrademe

    TCRA naomba mchunguze namba hii inanisumbua

    Kuanzia jana napata message kutoka namba 0738264152 inaniambia naomba unitumie hiyo hela kwenye namba hii ya Airtel 0695662564 jina AGNES ALKADO nakusubilia kwa wakala. Naomba fuatilieni tukomeshe usumbufu huu
  15. lufungulo k

    TCRA itoke hadharani kukiri kuwa muziki wa matapeli wa mtandaoni umewashinda

    Sasa imekuwa KERO, KERO KERO jumbe za kitapeli mtandaoni zimekuwa nyinginyingi mno! Hapa nadhani TCRA umefikia wakati watoke hadharani na kukubali kuwa muziki wa matapeli umewashinda. Kama kupata line za simu lazima uwe na namba ya NIDA, iweje tabia hii ya kitapeli izidi kushika kasi? TCRA...
  16. BARD AI

    Ripoti TCRA: Dar yaongoza kwa idadi kubwa ya Watumiaji wa huduma za Simu Tanzania

    Katika kipindi cha miaka 5 kumekuwa na ongezeko la Watumiaji 16,327,131 wa Huduma za Simu Nchini kutoka 47,685,232 mwaka 2019, sawa na 88% ya Idadi ya Watu hadi 64,088,651, sawa na 101.5% ya Idadi Watu Mikoa yenye Idadi kubwa ya Watumiaji wa Huduma za Simu Tanzania Bara ni Dar es Salaam...
  17. J

    AIRTEL Mnatukosea sana Mbeya, poor Quality of service by TCRA Q3 Report

    Airtel mna call drops kubwa sana , ndio maana hata ukipiga simu Mbeya kwa watumiaji wa Airtel hatusikiani . Hii Report ipo kwenye site za TCRA na iko wazi msiseme tunawasagia kunguni. Mmezidiwa hadi na TTCL kweli...
  18. Analogia Malenga

    Mabadiliko ya muonekano wa tovuti ya TCRA yameathiri upatikana wa ripoti za mawasiliano nchini

    TCRA tunaomba mfanye jambo maana leo kuna takwimu nimezifuata lakini kiunga kuelekea kwenye communications statistics hakifikiki Japo muonekano ni mzuri lakini tatizo hili ni kubwa kwa sisi watumiaji wa takwimu kutoka kwenu, Hili nalo mkaliangalie Uzi tayari
  19. Analogia Malenga

    Nimeshtushwa na TCRA kukosea jina lao kwenye ripoti yao

    Nimeshtusha na ripot ya mwezi wa March 2023, ya TCRA ambayo jina lako limekuwa ni Authory badala ya Authority. Yaani hii ni sawa na mtu kujikosea jina lako mwenyewe. Ni aibu
  20. Analogia Malenga

    Kuna shida ya takwimu za TCRA kuhusu matumizi ya GB kwa mitandao ya kijamii

    Nimeangalia matumizi ya GBs kwa robo mbalimbali nchini nimegundua kuna shida kwenye takwimu wanazotoa TCRA. Kwa robo ya mwisho ya mwaka 2022 walionesha kuwa tulitumia jumla ya GB Trilioni 90.1 Kwa robo ya kwanza ya mwaka 2023, data zimebadilika hadi kufikia GB milioni 48 Mimi niombe...
Back
Top Bottom