Macheyeki: Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
610
1,540
Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini.

Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network) iliyotolewa jana Oktoba 13, 2023. ACT Wazalendo tunaona taarifa hiyo pamoja na vifungu vya kanuni vilivyotajwa ni kandimizi na mwendelezo wa kuzuia wananchi kufurahia haki na uhuru wa kupata habari na kujieleza bila hofu na faragha za watumiaji.

Tunafahamu VPN zinatumiwa na watu binafsi na taasisi kama benki, mashirika katika shughuli zao za kila siku na kwamba kusalimisha itifaki hizo kwa TCRA kunaweza kurahisisha kuingilia faragha na taarifa binafsi za watumiaji kinyume kabisa na sheria za nchi.

Serikali ya CCM imekuwa ikizuia wananchi kupata au kutumia mitandao mbalimbali mara kwa mara bila maelezo yoyote. Wananchi hutumia VPN kuendelea kufikia habari, taarifa na kupata faragha. Mfano mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu Serikali ilifungia mitandao ya kijamii ili kuzuia wananchi kupata taarifa za kiuchaguzi. Hatutaki yajirudie tena.

ACT Wazalendo inashangazwa na kitendo cha Serikali badala ya kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu usalama na Ulinzi wa taarifa za kimtandao kama vile wizi wa taarifa, utapeli na ulaghai wa kimtandao, usiri wa taarifa zinazotembea katika mitandao na kuzuia udukuzi wa aina yoyote. Serikali inakuja na tamko la ajabu linalolenga kurudisha nyuma hatua na kurahisisha udukuzi wa taarifa. Hii haikubaliki na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

Hivyo, ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kusitisha mara moja kanuni hizo kandamizi na kuacha wananchi, taasisi na mashirika waendelee kuvinjari haki ya faragha, kupata na kutoa habari kama ilivyotolewa na katiba ya nchi.

Mwisho, tunatoa wito kwa wadau wote kushikamana ili kulinda uhuru wa kupata habari nchini kwa kupinga katazo hili haramu na kutaka kanuni zifanyiwe marekebisho.

Imetolewa na;
Ndg. Philbert Simon Macheyeki,
Waziri Kivuli wa Habari na TEHAMA,
ACT Wazalendo.
14 Oktoba, 2023.
 
Mambo mengine ni kujiongezea majukumu wasiyoyaweza! TCRA mpaka leo imeshindwa kudhibiti utapeli mitandaoni wale wa tuma kwenye namba hii tuma ya kutolea nk leo waje kudhibiti VPN private network virtual! Unaizuiaje kwa mfano? Watasimamisha kila mwenye simu kuikagua au watafanyaje? Wataalamu tujuzeni.
 
Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network) iliyotolewa jana Oktoba 13, 2023.

ACT Wazalendo tunaona taarifa hiyo pamoja na vifungu vya kanuni vilivyotajwa ni kandimizi na mwendelezo wa kuzuia wananchi kufurahia haki na uhuru wa kupata habari na kujieleza bila hofu na faragha za watumiaji.

Tunafahamu VPN zinatumiwa na watu binafsi na taasisi kama benki, mashirika katika shughuli zao za kila siku na kwamba kusalimisha itifaki hizo kwa TCRA kunaweza kurahisisha kuingilia faragha na taarifa binafsi za watumiaji kinyume kabisa na sheria za nchi.

Serikali ya CCM imekuwa ikizuia wananchi kupata au kutumia mitandao mbalimbali mara kwa mara bila maelezo yoyote. Wananchi hutumia VPN kuendelea kufikia habari, taarifa na kupata faragha. Mfano mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu Serikali ilifungia mitandao ya kijamii ili kuzuia wananchi kupata taarifa za kiuchaguzi. Hatutaki yajirudie tena.

ACT Wazalendo inashangazwa na kitendo cha Serikali badala ya kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu usalama na Ulinzi wa taarifa za kimtandao kama vile wizi wa taarifa, utapeli na ulaghai wa kimtandao, usiri wa taarifa zinazotembea katika mitandao na kuzuia udukuzi wa aina yoyote.

Serikali inakuja na tamko la ajabu linalolenga kurudisha nyuma hatua na kurahisisha udukuzi wa taarifa. Hii haikubaliki na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

Hivyo, ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kusitisha mara moja kanuni hizo kandamizi na kuacha wananchi, taasisi na mashirika waendelee kuvinjari haki ya faragha, kupata na kutoa habari kama ilivyotolewa na katiba ya nchi.

Mwisho, tunatoa wito kwa wadau wote kushikamana ili kulinda uhuru wa kupata habari nchini kwa kupinga katazo hili haramu na kutaka kanuni zifanyiwe marekebisho.
 

Attachments

  • ACT_kupinga_Zuio_VPN_nchini.docx
    129.2 KB · Views: 2
Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini.

Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network) iliyotolewa jana Oktoba 13, 2023. ACT Wazalendo tunaona taarifa hiyo pamoja na vifungu vya kanuni vilivyotajwa ni kandimizi na mwendelezo wa kuzuia wananchi kufurahia haki na uhuru wa kupata habari na kujieleza bila hofu na faragha za watumiaji.

Tunafahamu VPN zinatumiwa na watu binafsi na taasisi kama benki, mashirika katika shughuli zao za kila siku na kwamba kusalimisha itifaki hizo kwa TCRA kunaweza kurahisisha kuingilia faragha na taarifa binafsi za watumiaji kinyume kabisa na sheria za nchi.

Serikali ya CCM imekuwa ikizuia wananchi kupata au kutumia mitandao mbalimbali mara kwa mara bila maelezo yoyote. Wananchi hutumia VPN kuendelea kufikia habari, taarifa na kupata faragha. Mfano mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu Serikali ilifungia mitandao ya kijamii ili kuzuia wananchi kupata taarifa za kiuchaguzi. Hatutaki yajirudie tena.

ACT Wazalendo inashangazwa na kitendo cha Serikali badala ya kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu usalama na Ulinzi wa taarifa za kimtandao kama vile wizi wa taarifa, utapeli na ulaghai wa kimtandao, usiri wa taarifa zinazotembea katika mitandao na kuzuia udukuzi wa aina yoyote. Serikali inakuja na tamko la ajabu linalolenga kurudisha nyuma hatua na kurahisisha udukuzi wa taarifa. Hii haikubaliki na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

Hivyo, ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kusitisha mara moja kanuni hizo kandamizi na kuacha wananchi, taasisi na mashirika waendelee kuvinjari haki ya faragha, kupata na kutoa habari kama ilivyotolewa na katiba ya nchi.

Mwisho, tunatoa wito kwa wadau wote kushikamana ili kulinda uhuru wa kupata habari nchini kwa kupinga katazo hili haramu na kutaka kanuni zifanyiwe marekebisho.

Imetolewa na;
Ndg. Philbert Simon Macheyeki,
Waziri Kivuli wa Habari na TEHAMA,
ACT Wazalendo.
14 Oktoba, 2023.
SSH ni dikteta uchwara.
 
Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini.

Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network) iliyotolewa jana Oktoba 13, 2023. ACT Wazalendo tunaona taarifa hiyo pamoja na vifungu vya kanuni vilivyotajwa ni kandimizi na mwendelezo wa kuzuia wananchi kufurahia haki na uhuru wa kupata habari na kujieleza bila hofu na faragha za watumiaji.

Tunafahamu VPN zinatumiwa na watu binafsi na taasisi kama benki, mashirika katika shughuli zao za kila siku na kwamba kusalimisha itifaki hizo kwa TCRA kunaweza kurahisisha kuingilia faragha na taarifa binafsi za watumiaji kinyume kabisa na sheria za nchi.

Serikali ya CCM imekuwa ikizuia wananchi kupata au kutumia mitandao mbalimbali mara kwa mara bila maelezo yoyote. Wananchi hutumia VPN kuendelea kufikia habari, taarifa na kupata faragha. Mfano mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu Serikali ilifungia mitandao ya kijamii ili kuzuia wananchi kupata taarifa za kiuchaguzi. Hatutaki yajirudie tena.

ACT Wazalendo inashangazwa na kitendo cha Serikali badala ya kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu usalama na Ulinzi wa taarifa za kimtandao kama vile wizi wa taarifa, utapeli na ulaghai wa kimtandao, usiri wa taarifa zinazotembea katika mitandao na kuzuia udukuzi wa aina yoyote. Serikali inakuja na tamko la ajabu linalolenga kurudisha nyuma hatua na kurahisisha udukuzi wa taarifa. Hii haikubaliki na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

Hivyo, ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kusitisha mara moja kanuni hizo kandamizi na kuacha wananchi, taasisi na mashirika waendelee kuvinjari haki ya faragha, kupata na kutoa habari kama ilivyotolewa na katiba ya nchi.

Mwisho, tunatoa wito kwa wadau wote kushikamana ili kulinda uhuru wa kupata habari nchini kwa kupinga katazo hili haramu na kutaka kanuni zifanyiwe marekebisho.

Imetolewa na;
Ndg. Philbert Simon Macheyeki,
Waziri Kivuli wa Habari na TEHAMA,
ACT Wazalendo.
14 Oktoba, 2023.
Hii zuiazuia hazina maana sana, katika mazingira ya technology haiwezekani, ni vema wajifunze kuwa wa kweli itawaweka huru. Vinginevyo inatia shaka na mambo yanayoendelea ikiwa ni pamoja na tuhuma.
 
Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini.

Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network) iliyotolewa jana Oktoba 13, 2023. ACT Wazalendo tunaona taarifa hiyo pamoja na vifungu vya kanuni vilivyotajwa ni kandimizi na mwendelezo wa kuzuia wananchi kufurahia haki na uhuru wa kupata habari na kujieleza bila hofu na faragha za watumiaji.

Tunafahamu VPN zinatumiwa na watu binafsi na taasisi kama benki, mashirika katika shughuli zao za kila siku na kwamba kusalimisha itifaki hizo kwa TCRA kunaweza kurahisisha kuingilia faragha na taarifa binafsi za watumiaji kinyume kabisa na sheria za nchi.

Serikali ya CCM imekuwa ikizuia wananchi kupata au kutumia mitandao mbalimbali mara kwa mara bila maelezo yoyote. Wananchi hutumia VPN kuendelea kufikia habari, taarifa na kupata faragha. Mfano mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu Serikali ilifungia mitandao ya kijamii ili kuzuia wananchi kupata taarifa za kiuchaguzi. Hatutaki yajirudie tena.

ACT Wazalendo inashangazwa na kitendo cha Serikali badala ya kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu usalama na Ulinzi wa taarifa za kimtandao kama vile wizi wa taarifa, utapeli na ulaghai wa kimtandao, usiri wa taarifa zinazotembea katika mitandao na kuzuia udukuzi wa aina yoyote. Serikali inakuja na tamko la ajabu linalolenga kurudisha nyuma hatua na kurahisisha udukuzi wa taarifa. Hii haikubaliki na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

Hivyo, ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kusitisha mara moja kanuni hizo kandamizi na kuacha wananchi, taasisi na mashirika waendelee kuvinjari haki ya faragha, kupata na kutoa habari kama ilivyotolewa na katiba ya nchi.

Mwisho, tunatoa wito kwa wadau wote kushikamana ili kulinda uhuru wa kupata habari nchini kwa kupinga katazo hili haramu na kutaka kanuni zifanyiwe marekebisho.

Imetolewa na;
Ndg. Philbert Simon Macheyeki,
Waziri Kivuli wa Habari na TEHAMA,
ACT Wazalendo.
14 Oktoba, 2023.
ACT inafahamika tangu mwanzo, wanapenda sana Xvideos. ningeshangaa wangekaa kimya...
 
HOngera ACT WAZALENDO , chadema nyie mnasemaje au bodo mko kwenye ops 255?
 
Badala ya kufanya kila njia mifumo ya Serikali isomane wao wanakimbizana na VPN wapiga chabo wa Porn Mitandaoni.
 
Wanaotumia VPN bila kibali faini Sh5 milioni, kifungo mwaka mmoja

10 hours ago — TCRA imeeleza kuwa kosa kwa anayetumia VPN bila kibali faini yake ni Sh5 milioni au kifungo kisichopungua miezi 12 au vyote kwa ......

Habari zaidi :

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA


TAARIFA KWA UMMA KUTOA TAARIFA JUU YA MATUMIZI YA HUDUMA YA MTANDAO BINAFSI
(VIRTUAL PRIVATE NETWORK - VPN)


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa kwa Sheria
ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya Mwaka 2003, kwa lengo la kusimamia Sekta
ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta nchini Tanzania.

KWA KUZINGATIA Kanuni ya 16(2) ya Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kuhusu Maudhui Mtandaoni za mwaka 2020; mtu hatatoa, hatamiliki au hatasambaza teknolojia, programu, programu tumizi au kitu chochote kinachoendana na ambacho kinaruhusu au kumsaidia mtumiaji kupata maudhui yaliyokatazwa; na
KWA KUZINGATIA Kanuni ya 19(b) ya Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kuhusu Maudhui Mtandaoni za mwaka 2020; katika utekelezaji wa majukumu yake ya udhibiti
wa maudhui mtandaoni, TCRA ina mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya ukiukaji wa Kanuni
ikiwemo kuzuia upatikanaji wa maudhui yaliyokatazwa; na
KWA KUWA, TCRA imebaini upatikanaji wa maudhui yaliyokatazwa kwa kupitia matumizi ya mtandao binafsi (VPN) kinyume cha Kanuni;
HIVYO BASI, TCRA inautaarifu Umma kwa ujumla, watu binafsi na makampuni ambayo kwa
asili ya majukumu na kazi zao, matumizi ya mtandao binafsi (VPN) hayazuiliki, kutoa taarifa
kwa TCRA juu ya VPN wanazotumia na taarifa zote muhimu ikiwemo anuani ya itifaki ya mtandao (IP Address) kabla au mnamo tarehe 30 Oktoba, 2023 kupitia

TCRA itaendelea kuchukua hatua za kiudhibiti dhidi ya matumizi ya mtandao binafsi (VPN) yasiyo halali ikiwemo kuzuia upatikanaji wa VPN ambazo hazijatolewa taarifa au kusajiliwa.

TCRA inapenda kuukumbusha Umma kuwa, utoaji, umiliki au usambazaji wa teknolojia,
programu, programu tumizi au kitu chochote kinachoendana na ambacho kinaruhusu au
kumsaidia mtumiaji kupata maudhui yaliyokatazwa ni kosa la jinai, linaloadhibiwa baada ya
kutiwa hatiani, kwa faini ya shilingi za Kitanzania zisizopungua milioni tano au kifungo kisichopungua miezi kumi na mbili au vyote kwa pamoja.

IMETOLEWA NA
Mkurugenzi Mkuu,
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,
20 Barabara ya Sam Nujoma,
S. L. P 474,
14414 DAR ES SALAAM.
Simu: +255 22 241 2011-2
Nukushi: +255 22 2412009
Barua pepe: dg@tcra.go.tz
13 Oktoba, 2023
 
Ni maandalizi ya wizi wa uchaguzi wa serikali za mitaani hapo mwakani na uchaguzi mkuu
 
Zuio la TCRA Matumizi ya VPN linakandamiza uhuru wa habari Nchini.

Chama cha ACT Wazalendo kupitia Wizara Kivuli ya Habari na Mawasiliano tunapinga vikali taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania -TCRA ya kukataza matumizi ya Mtandao binafsi maarufu kama VPN (Virtual Private Network) iliyotolewa jana Oktoba 13, 2023. ACT Wazalendo tunaona taarifa hiyo pamoja na vifungu vya kanuni vilivyotajwa ni kandimizi na mwendelezo wa kuzuia wananchi kufurahia haki na uhuru wa kupata habari na kujieleza bila hofu na faragha za watumiaji.

Tunafahamu VPN zinatumiwa na watu binafsi na taasisi kama benki, mashirika katika shughuli zao za kila siku na kwamba kusalimisha itifaki hizo kwa TCRA kunaweza kurahisisha kuingilia faragha na taarifa binafsi za watumiaji kinyume kabisa na sheria za nchi.

Serikali ya CCM imekuwa ikizuia wananchi kupata au kutumia mitandao mbalimbali mara kwa mara bila maelezo yoyote. Wananchi hutumia VPN kuendelea kufikia habari, taarifa na kupata faragha. Mfano mwaka 2020 wakati wa Uchaguzi Mkuu Serikali ilifungia mitandao ya kijamii ili kuzuia wananchi kupata taarifa za kiuchaguzi. Hatutaki yajirudie tena.

ACT Wazalendo inashangazwa na kitendo cha Serikali badala ya kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu usalama na Ulinzi wa taarifa za kimtandao kama vile wizi wa taarifa, utapeli na ulaghai wa kimtandao, usiri wa taarifa zinazotembea katika mitandao na kuzuia udukuzi wa aina yoyote. Serikali inakuja na tamko la ajabu linalolenga kurudisha nyuma hatua na kurahisisha udukuzi wa taarifa. Hii haikubaliki na inapaswa kupingwa kwa nguvu zote.

Hivyo, ACT Wazalendo tunaitaka Serikali kusitisha mara moja kanuni hizo kandamizi na kuacha wananchi, taasisi na mashirika waendelee kuvinjari haki ya faragha, kupata na kutoa habari kama ilivyotolewa na katiba ya nchi.

Mwisho, tunatoa wito kwa wadau wote kushikamana ili kulinda uhuru wa kupata habari nchini kwa kupinga katazo hili haramu na kutaka kanuni zifanyiwe marekebisho.

Imetolewa na;
Ndg. Philbert Simon Macheyeki,
Waziri Kivuli wa Habari na TEHAMA,
ACT Wazalendo.
14 Oktoba, 2023.
wanajiandaa kwa ajili ya kampeni/uchaguzi 2025. wamesahau kwamba wameshachelewa. though kwa upande mwingine, nawapongeza, kucontrol mitandao baadhi kama ya ngono kumepunguza sana uovu. sasaivi mtandao wa ngono hupati. vizuri sana jambo hili.
 
Back
Top Bottom