tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. JanguKamaJangu

    Laini zisizohakikiwa kuzimwa Januari 31, 2023

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema ikifika Januari 31, 2023 namba za simu ambazo hazitakuwa zimehakikiwa zitazuiliwa kupokea na kutoa huduma za Mawasiliano. Taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa TCRA imesisitiza kuwa kila mtumiaji wa huduma za Mawasiliano anapaswa kutekeleza na kukamilisha...
  2. kavulata

    TCRA lindeni walaji wa habari

    Vyombo vya habari redio na tv havipaswi kuwa na ratiba za vipindi vyao zinazoonyesha muda na siku? Kama zipo ratiba ni nani anapaswa kuhakikisha kuwa ratiba hizi zinafuatwa na vyombo vya habari ili kuwalinda wasikilizaji na watazamaji wa vipindi vyao? Mfano, Redio inasema watakuwa na taarifa ya...
  3. T

    Wale mliofungiwa NIDA zenu (Blacklist) na TCRA kusajili line mpya njooni hapa mtoe shuhuda zenu na jinsi mlivyopata solution

    Mimi ni kiongozi wa timu za usajili wa line mpya. Hivi karibuni kumetokea wimbi la wateja wengi wanaotaka kusajili line mpya na vitambulisho havijajaa lakini wanaambiwa (nin blacklisted). Je wewe ni mmoja wao? Na je ulitumia njia gani kuondoa tatizo hilo? Karibu utuelezee ili na wengine wenye...
  4. BARD AI

    TCRA: Usikubali kuingiza Alama za Vidole mara mbili wakati wa kusajili Line

    MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imeeleza wahalifu wa mitandao ya simu maarufu kama 'Tuma kwa namba hii' wanavyosajili laini kinyemela kwa kutumia vitambulisho na alama za vidole vya watu, bila wahusika kugundua. Imesema uhalifu huo hufanywa na mawakala wanaosajili laini za simu mteja...
  5. Capo_di_Tutti_Capi

    Ni kwanini TCRA haisimamii na ku-regulate bei za huduma za mitandao?

    Habari ya asubuhi wana JF. Nimeleta hoja hii mbele yenu, kupata maoni kutoka kwenu. Hii ni kutokana na kubadilika kwa bei za vifurushi mara kwa mara bila kutolewa sababu za kubadilika kwa gharama za huduma hizo. Kwanini hakuna chombo kama EWURA!? Kinachofanyika kwenye mafuta kifanywe na huku...
  6. Njowepo

    TCRA saidieni kwenye hili la vifurushi, hali tete

    Hii mitandao ya simu kila leo wanapunguza package zao ila kwa bei ile ile. Mfano Vodacom kwa mwezi wa Nov na Oct kwa malipo ya Tshs 50,000 nimekuta wamepunguza 3GB na dk 200. wamepunguzakama ifuatavyo; ~ 50,000 Nov Package unapata :1200minutes 500sms 20GB. ~ 50,000 Oct Package nilipata...
  7. NetMaster

    Serikali ndio ya kulalamikiwa, Mitandao ya simu inafidia gharama zinazoongezwa na Serikali kwa kupandisha bei vifurushi

    Nimekuwa nikiona sehemu nyingi watu wanalalamikia mitandao ya simu kuongeza bei za vifurushi, hii sio sawa, tunalalamikia 2 badala ya kulalamimikia chanzo cha 1+1. Ni kama vile gharama za mafuta zikipanda basi nauli nazo zinapanda, si haki kuwalaumu wafanya biashara wenye mabasi. Ndivyo ilivyo...
  8. Bujibuji Simba Nyamaume

    Mfalme Zumaridi kama umeshindwa kuongoza kanisa, pisha mchungaji mwingine

    Duh.... Hapana Mfalme Zumaridi aache visingizio sasa. Kama ameshindwa kuongoza kanisa si aseme tu. Anashindwaje kuwakaripia wapiga vyombo kwa kuongeza sauti hadi inakuwa kero kwa waumini? Sisi ndio tunatoa sadaka, lakini hatuoni sadaka zetu zinafanya kazi gani. Yeye kila siku yuko kwenye...
  9. BARD AI

    Thamani ya miamala ya Simu yapungua nchini

    Wakati idadi ya watumiaji wa huduma za fedha kwa simu za mkononi ikizidi kuongezeka, thamani ya miamala wanayoifanya inapungua kila uchao. Ripoti ya robo mwaka inayoishia Septemba 2022 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaonyesha idadi ya miamala imeongezeka kutoka zaidi ya milioni...
  10. N

    Haki Itendeke; Hili la Mbowe TCRA wafungieni gazeti la Mwananchi kama mlivyofanya kwa Kwanza TV

    Kwanza tv ya maria sarungi iliandika Gwajima apata ajali, ikala rungu la TCRA , soma sababu zake na uniambie kwa nini mwananchi wasile rungu kwa jinsi walivyoandika habari ya mbowe kushinda huko ccm HAKI ITENDEKE, ACHENI DOUBLE STANDARD kilichofanya kwanza tv ikala rungu hiki hapa, bwana Joseph...
  11. ACT Wazalendo

    Macheyeki: BASATA iifungulie Mara Moja Wimbo wa Ney wa Mitego

    JUZI Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA,) ilivitaka vyombo vya Habari vya kielektronic hususan redio Tv na mitandao ya kijamii kutoutumia wimbo wa msanii wa Kizazi Kipya Emanuel Elibariki(Ney wa Mitego) walioutaja kwa jina la Tozo, wakieleza kuwa wamepokea taarifa kutoka baraza la Sanaa la...
  12. BARD AI

    TCRA yapiga marufuku wimbo wa Nay wa Mitego uitwao "Tozo"

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA imetoa agizo hilo kwa vyombo vyote vya Utangazaji nchini baada ya kupokea taarifa kutoka Baraza la Sanaa la Taifa BASATA. Kwa mujibu wa barua ya TCRA imesema baada ya BASATA kuhakiki wimbo huo imebaini kuwa maudhui yake hayafai kutumika katika jamii na...
  13. BARD AI

    TCRA: 80% ya tamthilia zinazorushwa kwenye TV ni za nje

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevihimiza vyombo vya habari kuangalia uwezekano wa kutoa nafasi kwa tamthiliya, muziki na michezo zenye maudhui ya ndani ili kulinda utamaduni na nembo ya Taifa. Akizungumza kwenye mkutano wa wadau mbalimbali wa vyombo vya habari, sanaa na michezo...
  14. Suley2019

    Maxence Melo: TCRA sikilizeni pande zote kabla ya maamuzi. Sheria na Sera za Nchi zilenge kuchochea Uchumi wa Kidigitali

    Baadhi ya masuala aliyoongelea Mkurugenzi mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo, katika warsha ya kukuza maudhui ya ndani yaliyofanyika TCRA. Kukosoana si kubaya Ukosoaji uwe wa pande mbili, kama kamati inavyokosoa watengeneza maudhui na wao pia wakubali kukosolewa, lakini kukosolewa huku kuwe...
  15. The Sheriff

    TCRA ina 'task force' ya kuwashughulikia wenye televisheni za online ambazo hazijasajiliwa

    Engineer Kisaka ameyasema hayo leo Septemba 16, 2022 wakati wa Warsha ya Kuhamasisha Uandaaji, na Uzalishaji wa Maudhui ya Ndani iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambapo Waziri wa Habari na Mawasiliano. "…lazima tumsikilize kila mmoja anasemaje. Muafaka uliofikiwa ni kuwa...
  16. BARD AI

    TCRA yaipiga faini ya Tsh. Milioni 2 ZamaMpya TV (DarMpya), Maudhui ya Afande Sele kuhusu Tozo yatajwa

    Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA)imeiamuru ZamaMpya TV Online kulipa faini Shilingi Milioni Mbili (2,000,000) ndani ya siku 21 kufuatia kuchapisha hisiyo na midhania ya habari. Taarifa hiyo ilihusu maudhui ya Selemani Msindi (Afande Sele) ambayo yanatuhumiwa kuwa ya...
  17. J

    TCRA imeendesha kikao Kazi na Wadau wa sekta ya Mawasiliano Kanda ya Kati

    TCRA imeendesha kikao Kazi na Wadau wa sekta ya Mawasiliano Kanda ya Kati Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari, ameongoza kikao kazi baina ya TCRA na Wadau wa Sekta ya Mawasiliano Kanda ya Kati, kilichofanyika Mkoani Tabora, katika ukumbi wa Isike...
  18. BARD AI

    Maxence Melo: Bei za vifurushi vya internet ni ghali, na huduma ni mbovu. TCRA watetea kupanda kwa bei

    Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums, Maxence Melo amesema kupanda kwa Bei ya Data hakukuwa na utaratibu mzuri na pia huduma imekuwa mbovu kwa gharama kubwa zaidi, jambo ambalo linaua ndoto za wabunifu wengi wanaotumia Mtandao. Melo amesema hayo wakati akijibu utetezi wa Bei Mpya za Vifurushi...
  19. Jidu La Mabambasi

    Ujumbe kwa TCRA: DStv wanarusha vipindi vya kuhamasisha ushoga kwa watoto?

    TCRA Please take note. Kuna ujumbe wa malalamiko kuwa kuna vipindi wanavyovipenda watoto vya NICKELODEON, vinavyorushwa na DsTV, vimeleta taharuki kwa wazazi. TCRA kama mhusika tafadhali chukua hatua. Ujumbe: Dear Parents/Guardians. This is to bring to your notice that the cartoon channel...
  20. sky soldier

    MB 1 iliuzwa senti 65, sasa tunakamuliwa shilingi 1 na senti 77, elfu 2 ilitupa GB 3 lakini sasa ni gb 1. Kenya na Zambia wametupindua

    Ndani ya muda mfupi kabisa gharama za internet zimepanda mara 2.7 yani tatu kasoro. Ni mwaka jana tu hapo kabla ya mabadiliko machunu ya vifurushi tulikuwa tunaweza kununua mb moja kwa senti 65 (shilingi 0.65) lakini sasa ni takribani shilingi 1.8. Hii elfu 2 tunayotumia kwa sasa kununua gb 1...
Back
Top Bottom