kodi

  1. Ushauri: Usiagize chochote nje ya nchi bila kujua gharama halisi za kodi na ushuru utakaolipia

    Moja ya changamoto kubwa wanayokutana nayo wateja wetu ni kuagiza bidhaa kwa njia ya mtandao halafu kukutana na kodi/ushuru mkubwa wa kutoa mzigo pale Bandarini, Uwanja wa Ndege au mipakani. Bei za viwandani (supplier) zinazowekwa mitandaoni huwa ni rahisi na zinavutia kuagiza. Mfano bei za...
  2. Ludovic Uttoh: Kama Kodi ni kwa maendeleo ya Nchi kwanini Wabunge hawakatwi wakati nao wanalipwa Mshahara kama wengine?

    CAG Mstaafu, Ludovic Uttoh amesema hakuna sababu za kwanini Wabunge wa #Tanzania hawalipi Kodi licha ya kwamba wana Mishahara kama walivyo Watumishi wengine wanaokatwa Kodi. Uttoh amesema "Siku zote msingi wa Kodi ni Usawa na wala kodi haitakiwi kuwa na Matabaka. Ikiwa tunasema tunalipa Kodi...
  3. Kwa YouTube content creators na wanaomiliki YouTube channel ni kweli U.S imepeitisha sheria ya kodi kwa raia wa nchi zingine pia 30% Tax ?

    Nilokuwa na pitia YouTube kuna channel kadhaa raia wa nchi zingine wanalalamika kuhusiana na kodi ambayo Marekani imepitisha ya 30% kwakuwa YouTube ni kampuni ya "kimarekani". hivyo basi kuqnzia sasa YouTube channel creator watakuwa wanalazimika kulipa kiasi hiko cha kodi kwa asalimia hizo...
  4. Haonga aombe radhi kwa upotoshaji kodi za Mbolea; Rais amesema Corona ndo chanzo cha kupanda bei ya Mbolea

    Leo wakati wa hotuba yake baada ya kuapisha mabalozi Mh Rais alijaribu kuhusiana na kupanda kwa bei ya mbolea nchini , jambo ambalo linaonekana wazi kuwa litaleta athari sana katika suala letu la chakula hapo mwakani. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa kupanda kwa bei ya mbolea nchini kumetokana...
  5. Jerry Silaa: Wabunge tuanze kukatwa kodi kwenye Mishahara yetu

    Mbunge wa Ukonga Jerry Slaa, amesema imefikia hatua Wabunge waanze kulipa kodi kupitia mishahara yao ili wapate uwezo wa kuwaambia Wananchi na wao walipe kodi. Silaa ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliowashirikisha wananchi wa Mzinga Ukonga jijini Dar es Salaam wakati akizungumzia...
  6. D

    Tozo na kodi kubwa zinavyoua Uchumi wa Mataifa yanayoendelea

    Ni wajibu wa kila serikali kuhakikisha wananchi wake wanaishi maisha bora, na ili serikali iwahakikishie wananchi wake maisha bora ni lazima wananchi hao watoe kodi ili serikali ijiendeshe vizuri. Mtu lazima awe anajishuhulisha eidha ameajiriwa au amejiajiri ili aweze kupata kipato cha kujikimu...
  7. Ujio wa kodi mpya ni nini? Serikali inalenga nini kwa umma kuongeza tozo mpya kwa mlipa kodi kupitia miamala ya mitandao?

    KODI (ushuru) ni malipo ambayo kila mtu mwenye shughuli za kuingiza kipato anatozwa na serikali kulingana na kipato chake. Hivyo kodi ni chanzo cha mapato ya serikali ambayo hutumika kugharamia huduma za jamii zinazotolewa na serikali kama ujenzi wa miundombinu, ujenzi wa mahospitali, shule...
  8. Wananchi tuanze rasmi kususia bidhaa na huduma za wasiolipa Kodi.

    Ndugu zangu wananchi wabunge hawalipi Kodi kwenye mishahara yao na ni mikubwa kwelikweli Sasa swali linakuja kwanini upande Basi lake? Kwanini ulale kwenye hoteli yake? Kwanini ununue chochote kwenye duka lake au hardware yake? Tena Bora lingekuwa lile bunge lililochaguliwa na wananchi la kina...
  9. Prof. Kitila: Hatujapunguza kodi kwenye bia za Kawaida

    Waziri wa Viwanda na Biashara, Prof. Kitila Mkumbo amesema serikali imepunguza kodi kwenye bia zinazotumia shayiri ya Tanzania 100% Amesema malalamiko ya kusema zimepunguzwa kwenye bia na kupelekwa kwenye miamala ni kutoelewa Amesema dhumuni la kushusha kodi ni kuwezesha uanzishwaji wa kiwanda...
  10. Serikali fanyeni yafuatayo kupata mapato badala ya kuleta kodi za kuumiza Watanzania

    Mkitaka serikali yetu ipate mapato kama mnavyotaka badala ya kuleta kodi za kuumiza watanzania fanyeni yafuatayo 1. Zuieni leakage ya kodi zinazotozwa kwa wafanya biashara, Bandarini, Kwenye manunuzi ya umeme, maji, usafiri wa reli, kwenye Masoko, n.k 2. Zuieni leakage ya kodi zinazotozwa...
  11. M

    Viongozi wa kisiasa Tanzania kutolipa kodi ni uzalendo?

    Viongozi wa Tanzania kuanzia Bungeni wamekuwa wakipitisha sheria mbalimbali za kuipatia serikali mapato kupitia kodi. Lakini viongozi mbalimbali wao hawalipi kodi kupitia mishahara yao na posho. Je, viongozi wa aina hii ni wazalendo kwa nchi yao? Je, unaweza kuhimiza wengine wafanye kitu...
  12. Mbali na kuikosoa serikali kuhusu Makato; lakini kiukweli Watanzania kwenye kulipa Kodi tuwagumu sana

    Kwema Wakuu! Kama nilivyoeleza kwenye heading hapo, suala la ulipaji Kodi Kwa sisi Watanzania ni kipengele. Watanzania wengi wetu Kama sio wote hatupendi kulipa Kodi. Hata wanaolipa Kodi ni kutokana na hawana jinsi mazingira yanawabana tu. Ila Kama wangeambiwa kwa hiyari yao nakuhakikishia...
  13. J

    Spika Ndugai: Asiyetaka tozo ya kizalendo atupe njia mbadala ya kupata fedha

    Spika Ndugai amesema wabunge wameshapitisha tozo ya kizalendo kwenye miamala ya simu na sasa ni sheria hivyo asiyeitaka atupe njia mbadala ya kutufikisha 2025 Roho wa Bwana akamshukia mtumishi wake Jerry Slaa mbunge wa Ukonga naye akajibu; Wabunge tuanze kulipa kodi. Labda kama Spika ana swali...
  14. Ni wakati sasa Wabunge kuacha utapeli na kulipa kodi inayolingana na kipato chao

    Wabunge wetu wa TZ wamejadili na kujinasibu niya yao ya kuinua mapato ya Taifa kupitia kodi. Hali inayojionesha kwa miaka mingi, ni tabia yao ya kutozungumzia ulipajhi wao wa kodi, usioendana na kipato halisia walichonacho. Kwa ujumla hili ni Bunge la watu wa misheni touni. Ktk kuhakikisha...
  15. D

    Tupo tayari kulipa kodi ya nchi bila kujali ukubwa wake

    Ndugu zangu habarini ! Poleni kwa changamoto zinazowakabili kutoana na mihangaiko mnayokabiliana nayo. Niende kwenye mada, ndugu zangu Watanzania wapotayari kulipa kodi kwaajili ya maendeleo yao bila kujali kiwango watakachotakiwa kulipa kwa serikali yao. Ila kutokana na madhaifu kadhaa kutoka...
  16. Jedwali la kodi za PAYE 2022 si la kitaalam

    Nimedownload hilo jedwali (INCOME TAX TABLES 2122) kwa link hii Tanzania Revenue Authority - Tax Tables na nimegundua lina mapungufu kadhaa, Kuna mahali ukiweka mshahara kodi inakuja hasi (negative). Na hii imesababishwa na mtengeneza jedwali kutotumia formula inayojumuisha kila tax bracket...
  17. S

    Polisi wafika nyumbani kwa Mbowe kwa upekuzi

    Mama na CCM wamebaki chama dola kwa asilimia 100.
  18. Hivi ukitaka kutoa mapendekezo ya vyanzo vya Kodi kwa Taifa, serikali inasikia kupitia njia ipi?

    Bado ninaamini serikali makini itakuwa na mfumo rahisi na wa wazi kupokea maoni mbalimbali tulionao wananchi juu ya mapendekezo Kodi zitoke wapi na mambo mengine. Hivi kwanini ndugulile akaongezewa kitengo kingine hiyo wizara ya mawasiliano, wakatengeneza data base inayoweza kupokea na kuchuja...
  19. B

    Suluhu kwenye kodi ya kizalendo

    Kimtazamo, kodi hii ni muhimu lakini haitekelezeki. Kodi hii huwezi kuita progressive maana imegusa maisha ya wananchi ambao hata basic needs ni shida. Yaani lower end zile charges ni exorbitant. Nini kifanyike; Tozo zitoe nafuu mpaka 50k TZS na kwenye miamala ya juu yake ziwe ndogo ili ku...
  20. Msingi wa hii dhana kuwa wanasiasa wasilipe kodi, wasishitakiwe inatoka wapi?

    Huwaga nashindwa kuelewa. Mtu kwa kujitoa kuwahudumia wananchi, wengine wanaenda mbali kusema wanawahudumia wanyonge, halafu anaacha kulipa kodi kwa miamala anayolipwa. Mbaya zaidi akikosea kisheria hata akiua, asishitakiwe. Miye napataga kigugumizi kuwatetea hawa watu.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…