Ilianza rasmi kipindi cha mh. jpm (r.i.p) ambapo kiswahili kilitamalaki kufikia kutumika kisawasawa afrika.
Juzi hapa tena mh. Mwigulu alipokuwa anasoma bajeti, alikipromoti tena kwa kusema usaili fulani (nimesahau eneo rasmi alilolitaja) utakuwa unafanyika kwa kiswahili sasa na si kiingereza...
Watanzania wote tumeiona Loyal Tour ikichezwa kwa lugha ya kiingereza na sio kiswahili.
Tunaitangaza nchi yetu na vivutio vya utalii kwa lugha ya kiingereza kwa nini lugha hii isiwe haki ya raia? Wasanii wetu wachekeshaji hawaendi Nigeria wala Ghana kisa language barrier. Sasa umefika wakati...
Wakuu habari zenu.
Nimepita kwenye status moja ya mdada nikakutana na hiyo clip ya Royal Tour kukiwa na maongezi kati ya Rais Samia na huyo mzungu.
Kuna kipande Rais Samia anamwambia huyo mzungu kuwa THIS IS BEGINNING OF BEAUTIFUL FRIENDSHIP. Nimejiuliza mara 2 kuhusu hiko Kiingereza je kipo...
Akiwa anasoma, kuna afadhali kidogo.
Lakini akiwa anaongea kutoka kichwani ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa], anapata shida sana.
Yaani Magu na Hangaya walichaguana wote wakiwa weupe kwenye hiyo lugha pendwa.
Muangalie na msikilize kwenye video hapo chini. Yale ambayo hayajaandikwa...
Nyota wa Bongo flavour Diamond Platnumz amepata taabu sana mitandaoni kwa siku kadhaa sasa kutokana na kiingereza chake kwenye filamu ya #YoungFamousAndAfrican.
Mdau mmoja amesema kuwa wengi hapa Afrika hususan Afrika Mashariki bado fikra zetu zinatawaliwa na wakoloni.
Kiingereza sio kipimo...
Members, Msipende kusikiliza maneno ya sisi wanasiasa kuwa lugha ya Kiswahili ni bora na elimu ya shule za kata ni bora sana.
Hakuna mwana siasa wa zama hizi ambaye mtoto wake anasoma shule ya kata au anasoma masomo ya msingi kwa lugha ya Kiswahili.
Usahili au Interview za sasa anayejua...
Jambo lakimaskini na kifukara la wanasiasa hafifu kifikra nikufikia hatua yakusifia lugha.
Nilichukizwa na Kiswahili kutumika kisiasa awamu ya Tano na watu wenye madaraka kuacha kushughulika na matatizo ya wananchi nakufungua mjadala wa kiswahili.Wasiojua kiswahili wakatuamunisha kutumia...
Kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kuelimika na kujua kiingereza hapa nchini kwetu. Kwasabb lugha yetu ya kufundishia ni kiingereza.
Hivyo ili mtu aweze kuipata elimu kwa kiwango kikubwa lazima aifahamu vema lugha ya kiingereza maana ndiyo iliyobeba taarifa zote zinazotakiwa na mwanafunzi...
Nitafurahi sana nikipata audio Clip ambayo itazidi dk 5 Rais wetu Mpendwa akichana mistari kwa kiingereza katika mahojiano au maelezo flani sehemu yoyote. Iwe imenyooka haijaungwa ungwa.
Nitafurahi sana. Tuachane na haya madai ya watu kuwa yeye huwa mara nyingi anasoma tu. Tunataka kuwaonesha...
Kiingereza cha watanzania wengi kinawasaidia na kinaishia kwenye kuandika status, kuelewa kilichoandikwa kwa kiingereza mfano magazetini na pale kinapotumika kuongea kwa kufatiliza maneno ambayo yameshaandikwa kwa mpangilio kwamfano kutoa hotuba kwa kufatiliza speech iliyochapishwa kwenye...
Sensa inakuja hivi karibuni,
Moja kati ya takwimu ninazotaka kusikia ni takwimu za lugha.
Je, Watanzania wangapi wanaweza kuongea lugha za asili?
Je, Watanzania wangapi waliopo wana zungumza Kiswahili kama lugha ya pili? Yani si lugha waliyoanza kuongea kama lugha yao ya kwanza.
Je...
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu imeibuka na mfumo mpya wa kujulisha umma Serikali inayoyafanya kwa njia ya Kiingereza. Hii imeminya umma usiojua Kiingereza kutojua yanayoendelea nchini
Tabia kama hii naona ni bora Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais. Zuhura Yunus atambue kuwa kwa sasa...
Hiki kitu nimeshuhudia kuna mtoto wa ndugu yangu anasoma shule flani ya msingi darasa la nne, ni shule ya mtaala wa kiingereza ila walimu ni wa hapa kwetu, huwa anafaulu vizuri tu lakini kuna maswali aliniletea nimsaidie ya social studies (maarifa ya jamii) sasa nikawa namweleza swali...
Hadi dakika za mwisho za kujiuzulu kwa Ndugai wana CCM wengi hawakujua wawe upande upi wa Spika au wa Rais. Ndio maana hadi sasa wabunge wengi wa CCM bado wapo kimya. Kwa upande wa upinzani hasa Chadema wao walichokuwa wanafanya ni kuchochea kuni, kuna waliokuwa wanampaka mafuta Ndugai kwa...
Elimu yetu inajengwa kwa msingi wa lugha ya Kiswahili baadaye inachanganywa na lugha ya Kiingereza.
Wakuu naomba tusaidiane, hii sentensi inamaana gani? Yaani nikiwa naama kwamba wewe umeilewaje?
Kama tunapenda maendeleo ya kiuchumi kupitia elimu yetu tunapaswa kufanya jambo katika elimu yetu...
Jana Mhe .Rais Samia alizindua Kitabu cha muongozo kwa Majaji na Mahakimu kinachohusu jinsi ya utoaji wa Haki za wanawake na watoto ktk kesi za mirathi ndoa na talaka n.k.
Sisi wananchi tunashukuru kwa hatua hiyo lakini tumeshangaa sana kuona kitabu hicho kuandikwa kwa lugha ya kizungu wakati...
Watumishi wa afya 290 kati ya 300 nchini Kenya wamefeli mtihani wa Kiingereza ambao ungewawezesha kupata kazi katika shirika la afya la Uingereza (NHS).
Julai 2021 Kenya iliingia makubaliano na Uingereza ambayo yatatoa fursa za ajira kwa wauguzi (wa Kenya) ambao hawana ajira.
Kuna Mzazi (Masikini au Mnyonge) Mwenzangu Chumba cha Pili tu nimetoka kumuamlia asimchape mwanae kwakuwa hajui Kiingereza huku akimwambia kuwa ni bora Afeli masomo yote ila siyo Kiingereza ambacho kwake ndiyo Ishara Kuu ya Mtu Msomi.
Cha kushangaza sasa huyu huyu Mwanae asiyejua vyema...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.