Tuache siasa, ajira zipo za kutosha Tanzania kwa wanaojua Kiingereza kwa ufasaha

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Members, Msipende kusikiliza maneno ya sisi wanasiasa kuwa lugha ya Kiswahili ni bora na elimu ya shule za kata ni bora sana.

Hakuna mwana siasa wa zama hizi ambaye mtoto wake anasoma shule ya kata au anasoma masomo ya msingi kwa lugha ya Kiswahili.

Usahili au Interview za sasa anayejua kujieleza kwa Kiingereza kwa ufasaha zaidi ndiye anayepata ajira kwenye Makampuni na mashirika binafsi.

Sekta binafsi zinahitaji watu wanaojua lugha kwa ufasaha ya Kiingereza.

Nilifika ofisi moja hapa Tanzania, hakuna mfanyakazi wa kitanzania anayoongea kiswahili, Wote wanatumia kiingereza fasaha kuanzia mlinzi nje mpaka wahudumu ndani.

Watoto wa watu wenye uwezo na waliosoma shule za kimataifa za kiingereza ndio Wanao kwenda kuongoza sekta zote nchi hii, Na hao watoto wengi ni wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wakubwa, Wakurugenzi wa taasisi na Mashirika au wale wafanyakazi wa serikali wenye mishahara mikubwa.

Vijana wa sasa wanakosa ajira kwa kushindwa kujieleza kwa Kiingereza fasaha kwenye Usahili wa mahojiano au Oral interview.

Vijana tumieni simu zenu kujiimarisha uwezo wa kuongea Kiingereza Fasaha, Degree bila kuongea Kiingereza kwa ufasaha ajira ni ngumu kupata sekta binafsi na hata taasisi baadhi za Serikali.

Kiingereza cha kufikiria maneno kama oooh, you know sir, Infact Sir. OK no problem..... The... The.... and.... OK you know... know huwezi kupata ajira kwa sasa.

Mtoto wa kihindi Tanzania wa darasa la tano anajieleza vizuri kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.

Mtoto wa chekechea Feza na Class three IST anajieleza kwa ufasaha kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.

Zamani watu walisoma shule za Serikali na waliongea Kiingereza kwa ufasaha lakini sio kwa walimu wa sasa na shule zilizopo sasa.

Shule za Tanzania hasa za serikali na baadhi sekta binafsi walimu wenyewe tu hawajui kiingereza, Je hao wanafunzi watajua Kiingereza?

Jitihada binafsi zinahitajika kwa wahitimu wa sasa kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha.

Kila siku ajira zinatangazwa za Kitaifa na kimataifa, Lakini vijana wetu wanaogopa na hata wakiomba hawawezi kufurukuta na watoto wa nchi jirani za Kenya na Uganda.

Hata sisi wakinga siku hizi familia zetu zinasoma shule za kisasa na vyuo vya kisasa nje ya nchi.

Fuatilieni scholarship vizuri muone watoto wa viongozi wanavyohangaika kuwaombea watoto wao.

Fuatilieni mashirika makubwa ya kimataifa mtawakuta watoto wa viongozi wa kisiasa huko WHO, UNICEF, WORLD BANK, UNESCO, UNHCR, CITI BANK na Bank zote za Kimataifa wapo watoto wao wanaoongea Kiingereza kwa ufasaha.

Ofisi nyingi na Bank kubwa kubwa Dar Salaam hakuna mfanyakazi wa kitanzania anaongea kiswahili ni Kiingereza tu kilichonyooka labda waamue kukuongelesha kwa Kiswahili.

Lini ulisikia watu wenye account Citi Bank, Standard chartered Bank hawajui Kiingereza, kuanzia wateja wa Bank hizo mpaka waajiriwa wanaongea wengi lugha vizuri ya Kiingereza. Hizo Bank ndani watanzania walioajiriwa wanaongea Kiingereza kwa ufasaha kama wazungu, usiyejua Kiingereza hupati kazi sehemu hizo.

Endeleeni kusema elimu ni uelewa wakati ulichokielewa huwezi kukielezea kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.
 
Watanganyika hawa wasiojua tofauti ya R na L wala matumizi ya herufu H are doomed to fail. Lugha yao tu hawawezi ndio iwe yai! Mtu kahitimu chuo kabisa anaandika ela, akuna, apana, ongera, Kalibu nk. Kifupi hatujui Kiswahili wala kimombo.
 
Nyoosha maelezo sema ajira zipo kwa watoto wa vipopa ie wabunge, wafanyabiashara, wakurugenzi etc lakini sio watoto wa walalahoi
Pamoja na hilo la lugha, Ila kiukweli watafuta ajira ni wengi kuliko ajira zenyewe.

Miaka yangu 8 mtaani na degree, nimeona mengi Sana. Lugha sawa hatupo vizuri lakini ukweli ulionyooka ni nafasi za ajira ni chache kuliko wahitaji. Usijidanganye kuwa Kila mwenye English nzuri anapata ajira.

Sasa hivi watu wengi mno wanaajiriwa Kwa simu.

Mtu anaulizwa 'kuna nafasi ya kazi kwenye kampuni, je una muda au upo busy'.
 
Umeandika kishabiki zaidi,
Kuna tofauti kubwa ya lugha na uelewa,
Kwa kuwa kazi nyingi zinatafutwa kwa lugha na si uelewa hapo tatizo!!

Lugha Ni swala la mawasiliano tu, mpime mtu kwenye utendaji na vitendo!!

Wachina hawajui kiswahili Wala kingereza lkn wamejaa Africa na wanafanya kazi sababu ujuzi upo tu!!

Elimu yetu bado yakiukoloni na mawazi yakiukoloni km haya ya lugha ndo tatizo kwa elimu yetu!!

Tuwajenge watoto ktk elimu sahihi, elimu ya vitendo na ufanisi swala la lugha Ni sehem tu ya mawasiliano!!
 
Kuna uhusiano gani kati ya kujua ngeli na kupata ajira?

Kuna chances za kazi zinazozalishwa kupitia sekta ya viwanda au huduma kwa private sector kunapelekea hata public sector kutokua.

Lazima private sector awe muajiri mkubwa ili kupanua tax base,na kutoka hapo ni rahisi public sector kuongeza wigo wa ajira kwani public in most cases ni service sector ili kui-facilitate private sector ikue.

Muandishi pengine urekebishe msingi wa dhana yako; kama muajiri anatafuta civil engineer haina uhusiano na lugha; wachina, wakorea au Indians wangapi wako hapa kwenye civil works na wala hata ngeli yao haijanyooka kama yetu.

Sina maana tusijiboreshe kwenye communication skills, Ila lazima msingi wa wizara ya ajira iwe na watu wenye IQ ya kuzalisha ajira kwa kushirikishana na Wizara ya biashara, uwekezaji na hazina kama facilitor wa availability of investment funds.
Unfortunate hazina inafocus kwenye tozo na kodi bila kuwe sehemu ya mchakato wa facilitation on investment financial instrument ili uzalishaji ukiwa mkubwa, kodi na tozo zitakuja inevitably. Ng'ombe apewe malisho ya kutosha ili maziwa yapatikane.
 
Kuna uhusiano gani kati ya kujua ngeli na kupata ajira?

Kuna chances za kazi zinazozalishwa kupitia sekta ya viwanda au huduma kwa private sector kunapelekea hata public sector kutokua.

Lazima private sector awe muajiri mkubwa ili kupanua tax base,na kutoka hapo ni rahisi public sector kuongeza wigo wa ajira kwani public in most cases ni service sector ili kui-facilitate private sector ikue.

Muandishi pengine urekebishe msingi wa dhana yako; kama muajiri anatafuta civil engineer haina uhusiano na lugha; wachina, wakorea au Indians wangapi wako hapa kwenye civil works na wala hata ngeli yao haijanyooka kama yetu.

Sina maana tusijiboreshe kwenye communication skills, Ila lazima msingi wa wizara ya ajira iwe na watu wenye IQ ya kuzalisha ajira kwa kushirikishana na Wizara ya biashara, uwekezaji na hazina kama facilitor wa availability of investment funds.
Unfortunate hazina inafocus kwenye tozo na kodi bila kuwe sehemu ya mchakato wa facilitation on investment financial instrument ili uzalishaji ukiwa mkubwa, kodi na tozo zitakuja inevitably. Ng'ombe apewe malisho ya kutosha ili maziwa yapatikane.
Unaongelea ulaya au hapa Tanzania, Achana na theory za darasani hizo zinawapotezea muda na wakati

Uwanja wa mapambano haupo hivyo Tanzania

Kuwa injinia sio kigezo cha kushindwa kuongea lugha kwa ufasaha

Misingi mibovu ndio maana unaitwa engineer wa miaka 4 huku huelewi lugha uliyosomea darasani

Kazi nyingi za engineering zinafanywa na Technician
 
Back
Top Bottom