GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Members, Msipende kusikiliza maneno ya sisi wanasiasa kuwa lugha ya Kiswahili ni bora na elimu ya shule za kata ni bora sana.
Hakuna mwana siasa wa zama hizi ambaye mtoto wake anasoma shule ya kata au anasoma masomo ya msingi kwa lugha ya Kiswahili.
Usahili au Interview za sasa anayejua kujieleza kwa Kiingereza kwa ufasaha zaidi ndiye anayepata ajira kwenye Makampuni na mashirika binafsi.
Sekta binafsi zinahitaji watu wanaojua lugha kwa ufasaha ya Kiingereza.
Nilifika ofisi moja hapa Tanzania, hakuna mfanyakazi wa kitanzania anayoongea kiswahili, Wote wanatumia kiingereza fasaha kuanzia mlinzi nje mpaka wahudumu ndani.
Watoto wa watu wenye uwezo na waliosoma shule za kimataifa za kiingereza ndio Wanao kwenda kuongoza sekta zote nchi hii, Na hao watoto wengi ni wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wakubwa, Wakurugenzi wa taasisi na Mashirika au wale wafanyakazi wa serikali wenye mishahara mikubwa.
Vijana wa sasa wanakosa ajira kwa kushindwa kujieleza kwa Kiingereza fasaha kwenye Usahili wa mahojiano au Oral interview.
Vijana tumieni simu zenu kujiimarisha uwezo wa kuongea Kiingereza Fasaha, Degree bila kuongea Kiingereza kwa ufasaha ajira ni ngumu kupata sekta binafsi na hata taasisi baadhi za Serikali.
Kiingereza cha kufikiria maneno kama oooh, you know sir, Infact Sir. OK no problem..... The... The.... and.... OK you know... know huwezi kupata ajira kwa sasa.
Mtoto wa kihindi Tanzania wa darasa la tano anajieleza vizuri kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.
Mtoto wa chekechea Feza na Class three IST anajieleza kwa ufasaha kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.
Zamani watu walisoma shule za Serikali na waliongea Kiingereza kwa ufasaha lakini sio kwa walimu wa sasa na shule zilizopo sasa.
Shule za Tanzania hasa za serikali na baadhi sekta binafsi walimu wenyewe tu hawajui kiingereza, Je hao wanafunzi watajua Kiingereza?
Jitihada binafsi zinahitajika kwa wahitimu wa sasa kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha.
Kila siku ajira zinatangazwa za Kitaifa na kimataifa, Lakini vijana wetu wanaogopa na hata wakiomba hawawezi kufurukuta na watoto wa nchi jirani za Kenya na Uganda.
Hata sisi wakinga siku hizi familia zetu zinasoma shule za kisasa na vyuo vya kisasa nje ya nchi.
Fuatilieni scholarship vizuri muone watoto wa viongozi wanavyohangaika kuwaombea watoto wao.
Fuatilieni mashirika makubwa ya kimataifa mtawakuta watoto wa viongozi wa kisiasa huko WHO, UNICEF, WORLD BANK, UNESCO, UNHCR, CITI BANK na Bank zote za Kimataifa wapo watoto wao wanaoongea Kiingereza kwa ufasaha.
Ofisi nyingi na Bank kubwa kubwa Dar Salaam hakuna mfanyakazi wa kitanzania anaongea kiswahili ni Kiingereza tu kilichonyooka labda waamue kukuongelesha kwa Kiswahili.
Lini ulisikia watu wenye account Citi Bank, Standard chartered Bank hawajui Kiingereza, kuanzia wateja wa Bank hizo mpaka waajiriwa wanaongea wengi lugha vizuri ya Kiingereza. Hizo Bank ndani watanzania walioajiriwa wanaongea Kiingereza kwa ufasaha kama wazungu, usiyejua Kiingereza hupati kazi sehemu hizo.
Endeleeni kusema elimu ni uelewa wakati ulichokielewa huwezi kukielezea kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.
Hakuna mwana siasa wa zama hizi ambaye mtoto wake anasoma shule ya kata au anasoma masomo ya msingi kwa lugha ya Kiswahili.
Usahili au Interview za sasa anayejua kujieleza kwa Kiingereza kwa ufasaha zaidi ndiye anayepata ajira kwenye Makampuni na mashirika binafsi.
Sekta binafsi zinahitaji watu wanaojua lugha kwa ufasaha ya Kiingereza.
Nilifika ofisi moja hapa Tanzania, hakuna mfanyakazi wa kitanzania anayoongea kiswahili, Wote wanatumia kiingereza fasaha kuanzia mlinzi nje mpaka wahudumu ndani.
Watoto wa watu wenye uwezo na waliosoma shule za kimataifa za kiingereza ndio Wanao kwenda kuongoza sekta zote nchi hii, Na hao watoto wengi ni wabunge, Mawaziri, Wafanyabiashara wakubwa, Wakurugenzi wa taasisi na Mashirika au wale wafanyakazi wa serikali wenye mishahara mikubwa.
Vijana wa sasa wanakosa ajira kwa kushindwa kujieleza kwa Kiingereza fasaha kwenye Usahili wa mahojiano au Oral interview.
Vijana tumieni simu zenu kujiimarisha uwezo wa kuongea Kiingereza Fasaha, Degree bila kuongea Kiingereza kwa ufasaha ajira ni ngumu kupata sekta binafsi na hata taasisi baadhi za Serikali.
Kiingereza cha kufikiria maneno kama oooh, you know sir, Infact Sir. OK no problem..... The... The.... and.... OK you know... know huwezi kupata ajira kwa sasa.
Mtoto wa kihindi Tanzania wa darasa la tano anajieleza vizuri kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.
Mtoto wa chekechea Feza na Class three IST anajieleza kwa ufasaha kuliko mwanafunzi wa chuo kikuu.
Zamani watu walisoma shule za Serikali na waliongea Kiingereza kwa ufasaha lakini sio kwa walimu wa sasa na shule zilizopo sasa.
Shule za Tanzania hasa za serikali na baadhi sekta binafsi walimu wenyewe tu hawajui kiingereza, Je hao wanafunzi watajua Kiingereza?
Jitihada binafsi zinahitajika kwa wahitimu wa sasa kujifunza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha.
Kila siku ajira zinatangazwa za Kitaifa na kimataifa, Lakini vijana wetu wanaogopa na hata wakiomba hawawezi kufurukuta na watoto wa nchi jirani za Kenya na Uganda.
Hata sisi wakinga siku hizi familia zetu zinasoma shule za kisasa na vyuo vya kisasa nje ya nchi.
Fuatilieni scholarship vizuri muone watoto wa viongozi wanavyohangaika kuwaombea watoto wao.
Fuatilieni mashirika makubwa ya kimataifa mtawakuta watoto wa viongozi wa kisiasa huko WHO, UNICEF, WORLD BANK, UNESCO, UNHCR, CITI BANK na Bank zote za Kimataifa wapo watoto wao wanaoongea Kiingereza kwa ufasaha.
Ofisi nyingi na Bank kubwa kubwa Dar Salaam hakuna mfanyakazi wa kitanzania anaongea kiswahili ni Kiingereza tu kilichonyooka labda waamue kukuongelesha kwa Kiswahili.
Lini ulisikia watu wenye account Citi Bank, Standard chartered Bank hawajui Kiingereza, kuanzia wateja wa Bank hizo mpaka waajiriwa wanaongea wengi lugha vizuri ya Kiingereza. Hizo Bank ndani watanzania walioajiriwa wanaongea Kiingereza kwa ufasaha kama wazungu, usiyejua Kiingereza hupati kazi sehemu hizo.
Endeleeni kusema elimu ni uelewa wakati ulichokielewa huwezi kukielezea kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.