Kwanini familia masikini zinaamini kujua Kiingereza tu ndiyo kuelimika wakati zinazojiweza zinaamini kwenye maarifa makubwa kitaaluma?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,516
108,791
Kuna Mzazi (Masikini au Mnyonge) Mwenzangu Chumba cha Pili tu nimetoka kumuamlia asimchape mwanae kwakuwa hajui Kiingereza huku akimwambia kuwa ni bora Afeli masomo yote ila siyo Kiingereza ambacho kwake ndiyo Ishara Kuu ya Mtu Msomi.

Cha kushangaza sasa huyu huyu Mwanae asiyejua vyema Kiingereza na kinampiga Chenga ni Bingwa wa Masomo ya Hesabu, Kemia, Fizikia na Jiografia kiasi kwamba hata Wanafunzi wengine huja Kufundishwa nae hapa Kwao na wanamkubali ile mbaya.

Hata Wanawake (Mademu) zetu wa 'Kiswahili' hasa wa huku Kwetu kwa Wanyonge (Masikini) ukithubutu tu Kuwatongoza kwa Kiswahili na siyo kwa Kiingereza si tu kuwa Wanakucheka bali wanasema Wewe si Msomi.

Ni kwanini Masikini tuna Ushamba mno?
 
Matajiri kwenye kiingereza walishatoka, unapoongelea tajiri unaongelea mtu anayefanyiwa kazi na hela ili kupata hela na si yule anayefanya kazi ili kupata hela.

Kwa maskini kutaka mtoto wake afahamu kiingereza yuko sahihi kwa sababu ndiyo lugha kuu ya mawasiliano.

Wakati wa kutafuta kazi hatoanzia kwenye kazi bali ataanza na kujieleza. Hata wale waliotanagaza nafasi zile za form point 32, written interview ni kiingerez. Japo lazima pembeni uwe na kimemo cha nani kakupeleka pale.

Hitimisho maskini anakihitaji kiingereza kuliko mtoto wa tajiri kwa sababu yeye anafikiria kuakiriwa, wakati mtoto wa tajiri anafikiria kuwa mkurugenzi kwenye moja ya co za mshua.
 
Kwa dunia ya leo hayo hayo maarifa unayapayaje bila Kiingereza?

Kingereza ni lugha ya to drill maarifa ya ziada.

Mfano fundi simu, umeme magari au electronics, kupitia video za you tube anaweza kujiongezea maarifa sana.

Chukulia accounting, engineering software hizi nyingi zina demo huko mitandaoni ila kwa kingereza

Ukweli ni kwamba kingereza kitabaki kiwa lugha ya katikati ya maarifa hasa kwetu tisiojua kichina , kijapani na lugha zingine adimu
 
Genta, Kiingereza ni muhimu sana aisee kwa maisha haya, ndio Lugha kubwa ya kibiashara na ndio lugha inayotumika pia kutafutia hayo maarifa popote pale.
 
Nafikiri sio familia maskini ni kwa zote (masikini na tajiri) na ndio sababu wanao jiweza wote huona deal ni kukimbizia watoto kwa shule za kiingereza.

Ukienda kwenye soko la ajira (hata nafasi ya engineering) unaweza kusikia baada ya interview, 90% ya interviewer wanajadili kuwa hata hajui kiingereza vizuri badala ya kujadili Content/ujuzi wake; Utafikiri Kiingereza kinajenga daraja

Kama mtu anasoma course za Art zinazohitaji mtu ajue lugha nyingi kwa ufasaha ni sawa ajue Kiingereza structure ila hizi Couse nyingine; kiingereza ni lugha ya mawasiliano akishaweza kuwasiliana inatosha;
Tuna mawazo ya kikoloni; Tunahitaji mabadiliko!
 
Mtu anayesoma fizikia yupo sekondari, bado anapigwa na mzazi kuhusu masomo.!!
 
Jamaa amerudi kutoka Ujerumani, amempata Mwajuma Ndalandefu wakale bata. Wamefika viwanja swagager za Mwajuma anataka kula pizza wakati jamaa anamiss soup ya kongoro.

You know na actual nyingi karibu kila sentence. Jamaa aliona Mwajuma ana mzengua alitafuta kuku wa kienyeji original kutoka mkoani.
 
Kiingereza ndicho nguzo ya maarifa yote na rejea ya kimataifa kama Kirumi na Kigiriki kwa mambo ya Kisayansi. Kukipuuza Kiingereza ni sawa na kuvaa shati juu ya koti, ukalifunga vifungo na tai kabisa, katika dunia ya watu waliostaarabika.
 
Utajiri sio kuwa na Mali nyingi utajiri ni kuridhika na ulicho nacho.
Hiyo ni tafsiri yako na huwezi kuipata mahali popote. Na kwa kuwa uko duniani lazima uishi na theory ya tafsiri ya utajiri na tajiri kwa mtizamo wa dunia.

Kama utajiri kuridhika neno maskini lingeshafutika.
 
Bila kujua kiingereza fasaha hata uhandisi wako utakupa tabu sana katika kutafuta ajira. Labda uende kwa Wachina. But internationaly you can't complete! Otherwise Serikalini, maana huko wanachanganyaga kiswahili na kiingereza!
 
Bila kujua kiingereza fasaha hata uhandisi wako utakupa tabu sana katika kutafuta ajira. Labda uende kwa Wachina. But internationaly you can't complete! Otherwise Serikalini, maana huko wanachanganyaga kiswahili na kiingereza!
Compete!
 
Kuna Mzazi (Masikini au Mnyonge) Mwenzangu Chumba cha Pili tu nimetoka kumuamlia asimchape mwanae kwakuwa hajui Kiingereza huku akimwambia kuwa ni bora Afeli masomo yote ila siyo Kiingereza ambacho kwake ndiyo Ishara Kuu ya Mtu Msomi.

Kwa nini familia masikini zinaamini kujua Kiingereza tu ndiyo kuelimika wakati zinazojiweza zinaamini kwenye maarifa makubwa kitaaluma?

Katika research, sampuli moja haitoshi kutolea conclusion. Huyo maskini na mnyonge mmoja hawezi kuwakilisha kundi kubwa bila kupata matokeo ya utafiti
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom