Hali hii ya mgandamizo, yaani unakuwa mzito, wasiwasi mwingi, maswali mengi, unajiuliza hivi nikiondolewa hapa nitaenda wapi?
Mtu anafanya kazi mahali fulani ila haoni kabisa kitu kingine cha kufanya kwenye maisha yake isipokuwa hiyo kazi anayoifanya.
Nikiwa na maana ofisi aliopo, haoni kitu...
Moja ya kitu ambacho hupaswi kukiruhusu ni siku yako kupita bila kusoma biblia yako na kutafakari.
Tumekuandalia kundi zuri la wasap la kusoma biblia kila siku na kutafakari, sio hivyo tu, unapata ufafanuzi au uchambuzi wa sura moja ya biblia kila siku.
Hii inakusaidia kuelewa kwa usahihi kile...
Kum 24:14-15 SUV
[14] Usimwonee mtumishi mwenye ujira aliye maskini na uhitaji, kama ni wa nduguzo, au kama ni wageni wako mmojawapo walio katika nchi yako, ndani ya malango yako; [15] mpe ujira wake kwa siku yake, wala jua lisichwe juu yake; kwa maana ni maskini, moyo wake umeutumainia...
Kum 16:19 SUV
[19] Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki.
Agizo hili la kukatazwa kupokea rushwa walipewa maakida na waamuzi wa Israeli, waliagizwa wasipokee rushwa, maana rushwa...
Hes 30:2 SUV
[2] Mtu atakapomwekea BWANA nadhiri, au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake; atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake.
Ukisoma sura hii yote ya Hesabu 30 utaona kuwa Mungu aliwataka watu wake kutunza ahadi zao kwake na...
Shelfu imejaa vitabu vizuri ikiwemo na biblia, vimepangwa katika utaratibu mzuri.
Meza ya ofisi imejaa vitabu vikubwa vikubwa, vimepangwa vizuri na vinapendeza.
Hatua kubwa sana kwako, mtu kukumbuka kuwa na kabati/shelfu zuri la vitabu na kuvijaza ni hatua kubwa sana.
Mtu kununua vitabu...
"Watu wakawa na kiu huko; nao wakamnung’unikia Musa, wakasema, Mbona umetupandisha kutoka Misri, kutuua sisi na watoto wetu na wanyama wetu kwa kiu?" Kut 17:3 SUV.
Musa alikutana na mengi katika uongozi wake wa kuwatoa Waisraeli Misri, tunaona hata walivyofika bahari ya Shamu na wakaona jeshi...
"Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe", 1 Kor 6:18 SUV.
Zipo dhambi nyingi zilizo chukizo mbele za Mungu, lakini hizi dhambi zinatofautiana katika utendaji wake na viwango vyake.
Zinaa ina...
"Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu", Rum 13:1-2 SUV.
Mungu ameweka bayana kuhusu kutii mamlaka ya serikali...
"Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?" Warumi 2:3 NEN.
Wapo watu hupenda kusema usiangalie tabia yangu bali zingatia ninachokuambia au ninachokuhubiri au ninachokufundisha.
Hatujui kuwa watu hujifunza zaidi kwa matendo...
"Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. Watu wakapiga kelele, wakisema, ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara Malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na...
"Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya mitume, akataka kuwapa fedha akisema, Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu. Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za...
"Yesu alipomwona mama yake mahali pale pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wamesimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, huyo hapo ndiye mwanao,” Kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Nawe huyo hapo ndiye mama yako.” Tangu wakati huo yule mwanafunzi akamchukua mama yake Yesu nyumbani...
Tunajenga nyumba nzuri na za viwango vya juu lakini zinaungua moto, zinabomolewa na kuharibiwa vibaya sana ila hatuachi kujenga.
Magari yanapata ajali na kuteketea kwa moto ila hatuachi kununua, kuyapanda na kusafiri nayo.
Watu wanafiwa na watoto wao, wanazaa wengine wanakuwa walevi...
Sio ajabu kuliona hili hasa kwenye jamii zetu za Kitanzania, mwanaume kulia machozi anaonekana kwenye jamii kama mtu wa kulialia hovyo na asiye na ukomavu wa mambo.
Kasumba hii imesababisha wanaume wengi kukaa na uchungu mwingi vifuani mwao huku wakijizuia kulia juu ya mambo yanayowasibu katika...
“Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani au hata kifoni”, Lk 22:33 SUV.
Petro alikuwa ni mmoja wa wanafunzi wa Yesu mahiri na waliokuwa karibu sana na yeye, ukimfuatilia Petro utaona matukio kadhaa aliyoyafanya akiwa na Yesu, huyu huyu Petro ndiye aliyeahidiwa...
"Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi", Lk 19:17 SUV.
Mtu yeyote ambaye amekuwa mwaminifu katika kumtumikia Mungu na kulitumikia lile kusudi lake kwa uaminifu, mtu huyo atapata thawabu kubwa katika dunia ya sasa...
"Na watu wote walikuwa wakilia na kumwombolezea; akasema, Msilie, hakufa huyu, bali amelala usingizi tu. Wakamcheka sana, maana walijua ya kuwa amekwisha kufa", Lk 8:52-53 SUV.
Wakati mwingine huwa tunaonekana kama tumechanganyikiwa au hatuna akili sawa sawa, hasa tulioamini.
Kuna mambo...
Tuingie moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu, watu baadhi wameingia kwenye ndoa na watu sahihi ila mitazamo yao juu yao sio sahihi, wapo wameingia kwenye ndoa sio sahihi kwa sababu ya mitazamo yao isiyo sahihi, na wapo hawataki kuingia kwenye ndoa wamebaki kutangatanga na kila...
Kesho 23.8.2022 ni siku ya kuhesabiwa(sensa) kwa nchi yetu Tanzania, hili ni suala la kibiblia kabisa watu kuhesabiwa wala sio suala la kisiasa.
Namaanisha usichanganye siasa na Sensa, utaratibu wa kuhesabiwa umetajwa kwenye biblia (LK 2:1-5). Wala hujapingwa au kukatazwa.
Nakusihi uonyeshe...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.