nautaka tena
Senior Member
- Jun 29, 2021
- 182
- 213
Viongozi wa hii nchi hivi hawaoni umuhim au ni ushenzi tuu kula like umemaliza uziNafikiri akili sasa zitatukaa vizuri. Tunaposema Katiba Mpya ni muhimu tunamaanisha.
Nchi ni lazima iwe na dira ya maendeleo na si kama hivi sasa inavyoongozwa Kwa kufuata mawazo ya mtu mmoja. Yawe mazuri au ya hovyo. Anaweza kuamua lolote bila kushauriana na yeyote yule. Mbaya zaidi hakuna chombo Chenye Mamlaka ya kuhoji.
Nije kwenye mada. Rais aliamua Bandari ijengwe. Kwa mawazo yake aliona/aliamini ina faida kubwa kwa Taifa na hata kwa mataifa jirani zetu kusini mwa nchi. Makofi alipigiwa na kupongezwa kwa moyo wake wa kizalendo.
Rais aliyefuata akaja na mawazo yake binafsi. Akasema Bandari ile ni wizi na unyonyaji mkubwa kwa Taifa. Mikataba ya hovyo kabisa ni wapumbavu pekee ndio wanaweza kukubaliana na mikataba hii. Nae kapigiwa makofi na kupongezwa kwa moyo wake wa kizalendo ktk kuwatetea raia wa nchi yake.
Kaja mwingine Kwa mbinu mpya eti ile mikataba haikuwa kweli kama tulivyoaminishwa. Hivyo ni muhimu sana kuwa na Bandari ile kwani ina manufaa makubwa Kwa nchi yetu.
Bwawa la Mwl Nyerere tuliambiwa ndiyo mwarobaini wa tatizo la umeme nchini. Kulingana na hali ilivyo kwa sasa wakati wowote tutaambiwa, kulingana na mabadiliko ya tabia ya nchi umeme wa kutegemea maji siyo ishu. Nalo likapigwa pending.
Ni Nani mkweli kati ya hawa wote?? Mimi sina jibu kwani wenye uwezo na mamlaka ya kupitia mikataba yote ni Wabunge.
Bunge lenyewe ndiyo hilo. Limegeuzwa kuwa kichaka cha kupitishia mawazo ya mtu mmoja kwa mgongo wa Serikali.
Bila kuwa na Katiba Mpya itakayompunguzia Rais Mamlaka/Madaraka basi hatutaweza kuwa na Mihimili mitatu itakayoweza kujisimamia yenyewe bila kuingiliana ktk kutekeleza majukumu yao.