Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,148
Nimejaribu kuwaza kwa kina haya yanayoendelea hapa Tanzania kuhusiana na sekta ya bandari.
Sote tunajua tayari Serikali na bunge wamepitisha na kusaini mkataba wa uendelezaji na uendeshaji shughuli za bandari zote za Tanganyika kuwa chini ya umiliki na usimamizi wa milele wa muarabu wa Dubai (DP world). Kupitia mkataba huo, automatically bandari ya Bagamoyo nayo itakuwa mikononi mwa muarabu wa Dubai!
Kabla ya hayo kutokea, tayari serikali ilishapitisha mpango wa mkataba wa ujenzi na upanuzi wa Bandari ya Bagamoyo baina ya Tanzania na China, mkataba ambao ulikuwa unaelezwa (Rais Magufuli alilithibitisha hili) kuwa unazuia pia uendelezaji na upanuzi wa bandari zingine zote katika mwambao wa bahari ya Hindi ikiwemo bandari ya Dar na Mtwara. Mkataba huo ulipitishwa mwishoni mwa utawala wa Kikwete, ukazimwa kipindi cha utawala wa Magufuli na baadaye ukafufuliwa na utawala wa Mama Samia.
Nini hatma ya mpango wa ujenzi na upanuzi wa bandari ya Bagamoyo chini ya mchina katikati ya mazingira ya mkataba mpya wa bandari zote za Tanganyika kuwa chini umiliki na usimamizi wa muarabu wa Dubai?
Sote tunajua tayari Serikali na bunge wamepitisha na kusaini mkataba wa uendelezaji na uendeshaji shughuli za bandari zote za Tanganyika kuwa chini ya umiliki na usimamizi wa milele wa muarabu wa Dubai (DP world). Kupitia mkataba huo, automatically bandari ya Bagamoyo nayo itakuwa mikononi mwa muarabu wa Dubai!
Kabla ya hayo kutokea, tayari serikali ilishapitisha mpango wa mkataba wa ujenzi na upanuzi wa Bandari ya Bagamoyo baina ya Tanzania na China, mkataba ambao ulikuwa unaelezwa (Rais Magufuli alilithibitisha hili) kuwa unazuia pia uendelezaji na upanuzi wa bandari zingine zote katika mwambao wa bahari ya Hindi ikiwemo bandari ya Dar na Mtwara. Mkataba huo ulipitishwa mwishoni mwa utawala wa Kikwete, ukazimwa kipindi cha utawala wa Magufuli na baadaye ukafufuliwa na utawala wa Mama Samia.
Nini hatma ya mpango wa ujenzi na upanuzi wa bandari ya Bagamoyo chini ya mchina katikati ya mazingira ya mkataba mpya wa bandari zote za Tanganyika kuwa chini umiliki na usimamizi wa muarabu wa Dubai?