esther mashiker
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 616
- 552
RAIS John Magufuli amesema sababu kubwa ya kusitishwa kwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ni masharti magumu yaliyomo katika mkataba wa utekelezaji wa kazi hiyo.
Jiwe la msingi la ujenzi wa bandari hiyo liliwekwa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete mwaka 2015 na ulitarajiwa kugharimu dola za Marekani bilioni 10. Bandari hiyo endapo ingejengwa ingekuwa kubwa zaidi Afrika Mashariki ikiwa na ukubwa wa ekari 3,000 na viwanda 190 vingejengwa.
Akizungumza jana kwenye mkutano wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliowashirikisha wafanyabishara kutoka wilaya 139 nchini, Rais Magufuli aliweka wazi sababu za kusitishwa kwa ujenzi wa bandari hiyo. Rais Magufuli alisema “kwenye mkataba wa ujenzi wa bandari hiyo kulikuwa na vipengele vya ovyo”. Rais Magufuli alisema mojawapo ya masharti ni kutojengwa wala kuendelezwa kwa bandari yoyote kuanzia eneo la Tanga hadi Mtwara.
"Yaani kwenye eneo lote kuanzia Tanga hadi Mtwara kusijengwe bandari yoyote. Bandari ya Kilwa tusiiendeleze, Bandari ya Mtwara ambayo itawezesha mikoa ya kusini kupokea mafuta badala yake Dar es Salaam kisha yarudi huko, hatutakiwi kuiendeleza, Barabara kutoka Mtwara hadi Bamba Bay ambayo itatuwezesha kusafirisha mizigo hadi Msumbiji tusiijenge," alisema Rais Magufuli
Pia alisema wawekezaji hao wangeweza kumiliki ardhi kwa hati ya miaka 99 pamoja na kutoruhusiwa kuuliza nani anamiliki eneo hilo. Rais Magufuli alisema sharti lingine ni gharama zitakazotumiwa na mwekezaji huyo katika ujenzi wa bandari hiyo kutakiwa kurejeshwa.
Bandari ya Bagamoyo: Je, sababu alizotoa Rais Magufuli ni za kweli?. Je, haya mazungumzo ni ya nini tena kama wameachana na mradi huo? - JamiiForums