FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,890
- 109,227
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inafanya mageuzi makubwa ya mfumo wa elimu kuanzia sasa hivi. Watakuwa na mpango wa muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Katika mipango hiyo kuna mitihani ya Taifa ambayo itafutwa kabisa. Hawaoni sababu ya kuwepo kwa mfumo wao mpya wa elimu.
Jinsi nilivyolisikiliza tamko hili (video chini) la awali, inaonesha kama ni mipango mizuri. Watakuwa na mafunzo ya amali kuanzia mapema, yaani wanafunzi watafundishwa fani mbali mbali za kazi wakati wanaendelea na masomo yao mengine, na si kama ilivyo sasa kwa Zanzibar, kuwa mwanafunzi mpaka amalize kwanza form four ndiyo aweze kwenda vyuo vya kazi. Jisikilizie ufafanuzi zaidi:
Jinsi nilivyolisikiliza tamko hili (video chini) la awali, inaonesha kama ni mipango mizuri. Watakuwa na mafunzo ya amali kuanzia mapema, yaani wanafunzi watafundishwa fani mbali mbali za kazi wakati wanaendelea na masomo yao mengine, na si kama ilivyo sasa kwa Zanzibar, kuwa mwanafunzi mpaka amalize kwanza form four ndiyo aweze kwenda vyuo vya kazi. Jisikilizie ufafanuzi zaidi: