Zanzibar kufuta mitihani ya Taifa na kuwa na Mfumo Mpya wa Elimu

Na sisi Tanzania tufute tunasubiria nini?

---
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Mussa leo October 18,2023 ametangaza baadhi ya mabadiliko na mageuzi ya elimu ikiwemo sera na sheria mpya ambazo zitatarajiwa kuendana na mabadiliko hayo kwa Zanzibar yanayotarajiwa kuanza kwa Wanafunzi waliopo madarasa ya chini kuanzia darasa la kwanza, mabadiliko hayo ni pamoja na kufuta mitihani ya darasa la nne na kidato cha pili.

"Serikali itaondoa mitihani ya Taifa ya darasa la nne na mitihani ya kidato cha pili, Serikali imeamua kufuta hii mitihani, kwanza sio kwamba inamfanya Mwanafunzi ahitimu au inamfanya Mwanafunzi asiendelee kusoma lengo la mitihani ni kumpima kafaulu au hakufaulu, tutaandaa utaratibu mwingine mzuri”
Kwetu ndo ilikuwa Ya kwanza kupitishwa hii sheria
 
Hakuna sehemu nilipozungumiza Swala la Muungano!
Nilichosema ni kwamba Swala hilo lilikwisha Tangazwa na Wizara Ya elimu ya JMT (Jamhuri ya Muungano Tangu mwezi may 2023)

Ok hata hivyo bado unaonekana hata katiba hauijui vizuri Elimu ya Msingi na secondary zinaendeshwa chini ya baraza la Mitihani NECTA...

NA BARAZA LA.MITIHANI LIPO CHINI YA ISHU ZA MUUNGANO

Chukua katiba yako Taratibu nenda kwenye Misc. 1 Au Nyongeza ya 1 Mambo yanayohusu Muungano Soma jambo la 16
View attachment 2785427
Mwenzio kaleta mambo ya Zanzibar wewe unasema lilishatangazwa na waziri wa JMT huoni unajichanganya?
 
Mwenzio kaleta mambo ya Zanzibar wewe unasema lilishatangazwa na waziri wa JMT huoni unajichanganya?
Sasa nimejichanganya wapi hapo Mleta mada baada ya kusema hivyo na yeye akasema kuwa alikuw hafahamu kama wametangaza!
Kwahyo pengine nimemfumbua macho maana Lengo lake alitamani Iwe ni jambo la pamoja kati ya Tz bara na Zanzibar...
Hata hivyi zanzibar ni sehemu ya Muungano kwahyo sioni kama kuna shida!
 
Ukweli kwa hili lakumfanyia assessment mwanafunzi badala ya kumpima kwa siku moja naunga mkono 100% baada ya miaka 10 Zanzibar itakuwa mbali sn kwenye ujuzi badala ya kukaririshana, kwenye mazuri tupongeze hata sisi Tanganyika tuige hiki kitu.
Hakuja ujuzi hambao hauna foundation nzuri, na foundation modules ndo ngumu maana ndo zina mjemga mtu kuisuka idea yake
 
Shule za Zanzibar kwa miaka nenda rudi zimekuwa za mwisho kwenye mitihani ya taifa, suluhisho si kukimbia na kutafuta namna ya kuwalegezea watoto wao bali wazazi waweke mkazo kwenye elimu dunia pia wajifunze kuumia pindi watoto wao wanapofeli.
Hili limekuwa likifanywa makusudi na NECTA ili ionekane hivyo.
 
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inafanya mageuzi makubwa ya mfumo wa elimu kuanzia sasa hivi. Watakuwa na mpango wa muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Katika mipango hiyo kuna mitihani ya Taifa ambayo itafutwa kabisa. Hawaoni sababu ya kuwepo kwa mfumo wao mpya wa elimu.

Jinsi nilivyolisikiliza tamko hili (video chini) la awali, inaonesha kama ni mipango mizuri. Watakuwa na mafunzo ya amali kuanzia mapema, yaani wanafunzi watafundishwa fani mbali mbali za kazi wakati wanaendelea na masomo yao mengine, na si kama ilivyo sasa kwa Zanzibar, kuwa mwanafunzi mpaka amalize kwanza form four ndiyo aweze kwenda vyuo vya kazi. Jisikilizie ufafanuzi zaidi:

Asante kwa taarifa.
 
Hii mbona ilishatangazwa na waziri wa Elimu Wa JMT alisema pia Kwa sasa Shule za Msingi watasoma mpaka Darasa la sita na Kuingia moja kwa moja Form one.

Pia alisema kuwa kutakuwa na mafunzo ya amali kama muziki na elimu ya kazi secondary na hakuna haja ya mtu kusma ma Physics wala ma Chemistry wala ma history.

Kama huu mtaala utafanikiwa nitakuwa wa kwanza kuipongeza Serikali ya CCM rasmi
Bila physics, chemistry, biology, mathematics tutapigaje hatua.
 
Hii nchi mi maishangaa sana badala ya kujenga vyuo vya ufundi na kutoa elimu mbadala ya ufundi tangu msingi wao wanaangaika na kujenga mashule na madarasa.. tukubaliane sio kila kichwa cha kufundishwa physics, chemistry,math, bookkeeping n.k
 
Ukweli kwa hili lakumfanyia assessment mwanafunzi badala ya kumpima kwa siku moja naunga mkono 100% baada ya miaka 10 Zanzibar itakuwa mbali sn kwenye ujuzi badala ya kukaririshana, kwenye mazuri tupongeze hata sisi Tanganyika tuige hiki kitu.
Na kwenye utalaamu je? Maana baadhi ya mifumo inafanya vizuri kwenye nchi ambazo tayari zina wataalamu wao - mfano wanasayansi, watafiti katika masuala mbalimbali, nk. Tunaweza kuiga mfumo fulani wa elimu kumbe tukasahau mambo muhimu yanayofanyika kutoka huko tulikoiga. Pia kama mfumo wetu wa elimu utazaa matabaka ya watu - mfano: wabobezi na wengine wa 'rasharasha' tutatengeneza tatizo lingine.

Kuna articles nyingi nimekuwa nikizisoma kuhusu the 21st century skills (soft skills). Watunzi wanasema kama kuna watu wanatafuta ajira - kwa mfno - employers wanachokitafuta, pamoja na technical (hard) skills ambazo tunazipata darasani ni soft skills ambazo tunajifunza nje ya darasa. Sasa uelewa wa watu wengine ni kwamba technical (hard) skills hazitakiwi, isipokuwa soft skills. Unaona hiyo tofauti?
 
Zanzibar imeathiriwa sana na mafunzo ya kidini/madrasa kiasi kwamba wanafunzi wao hawawezi kuwa na matokeo mazuri sambamba na wenzao wa bara kwenye mitihani ya NECTA/NECTVET. Shule zao haziwezi kushindana kwa matokeo mazuri na shule za bara. Zinafanya vibaya mpaka aibu, kuzipata shule zao kwenye top ten ni shughuli pevu.

Bora wakimbie aibu waanzishe mifumo yao ya mitihani wajipongeze wenyewe huko. Ila kwa upande mwingine wanajitoa taratibu kwenye muungano, hiyo ni hatua mojawapo ya kujitoa kwenye muungano
 
Back
Top Bottom