Watu wanaoendelea kusema kuwa CCTV Camera haiwezi kuchukua pia za ubora huo sijui kama walimsikiliza IGP, na kama walimsikiliza hawakumuelewa.cctv camera za tz ni kwere zinaifata gari hadi makutano ya barabara.
alafu zinatoa picha tofauti na cctv zingine.
Maelezo ya ajabu ajabu ya igp yaanacha maswali mengi sana kwamba kuna kitu anafahamu na anaficha
Hajasema kuwa picha za gari alizoonyeshwa ZILIPIGWA NA CCTV ZA HOTEL ALIPOTEKEWA MO, alisema kuwa PICHA ZA CCTV ZA HOTEL ZIMEWASAIDIA KUITAMBUA GARI inayoaminika kumteka.
Na kwa maana hiyo, pengine picha hizo za gari alizozionyesha ni za gari husika sehemu tofauti - na hii inatoa picha kuwa walifanya uchunguzi hata kubaini picha halisi za gari hilo.
Ugumu uko wapi kuelewa hapo?
Ni sawa umuone mharifu kwenye picha ya CCTV halafu ukamtambua, ukipata picha zake zinazomuonyesha CLEAR zaidi si utazitumia hizo kwa upelelezi?
Tujifunze kutumia vichwa kufikiri!