Diehard
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 467
- 347
Mzee naona unafuatilia kwa umakini sana, hapa mtu unapata picha Kibatala alikuwa anataka nini kutoka kwa shahidi
Mzee naona unafuatilia kwa umakini sana, hapa mtu unapata picha Kibatala alikuwa anataka nini kutoka kwa shahidi
Bora angetafsiri maana yake nimechumbiwaMallya: I have been Engaged Maana yake nini
Shahidi: Maana yake "Nimefanya Uchunguzi
Sasa hapo huelewi nn, kwani kozi na kazi inaanza niniHivi jamani mbona kama mimi sijaelewa au nyie mmelewa vipi shahidi namba 3 anasema kaanza kazi 2013 na uko elfu 2004,2006 sijui kasoma kozi za mambo ya bunduki zanzibar na mambo mengine mara sijui 2010 kasomaje hayo mambo wakati kazi kaanza 2013?
IGP alisema kuna ushahidi wa kutisha katika kesi hii. Nadhani tunaanza kuamini sasa.Barua iliyoambatanishwa na vithibitisho hailandani na report ya afande....
Barua inasema ufanyie uchunguzi hivyo vitu, yeye report yake inasema conspiracy to commit terrorism.
Kutokujua kiingereza haikufanyi ukawa mjinga mkuu. Mbona Wachina, Warusi, Wakorea n.k. hawajui kiingereza lakini ni wagunduzi wa mambo mengi tu hapa duniani.Tatizo katumia muda mwingi kusema kasoma mpaka Botswana kwenye mambo ya vilipuzi ni mtaalamu mbobezi ina maana huko Gaborone alikua anaongea kizigua chetu asijue hata maana ya utalii kwa kimalkia..
Kama hujui kitu kwanini ukitumie, angeandika tu kwa kiswahili, lakini kuandika kitu ambacho hujui maanake huo ni uzuzu.Kutokujua kiingereza haikufanyi ukawa mjinga mkuu. Mbona Wachina, Warusi, Wakorea n.k. hawajui kiingereza lakini ni wagunduzi wa mambo mengi tu hapa duniani.
Mawakili wa utetezi mbona maswali yenu butuKesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine.
Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 29/10/2021
UPDATES
Mpaka sasa mawakili upande wa utetezi tayari wamewasili mahakamani.
Mpaka sasa ni saa nne kasoro, kesi bado haijaanza.
Jaji anaingia 3:50
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe dhidi ya Jamhuri inatajwa.
Wakili wa Serikali Robert Kidando anasimama kutambulisha
1. Robert Kidando
2. Nassoro Katuga
3. Ignas Mwanuka
4. Esther Martin
5. Tulumanywa Majige
6. Jenitreza Kitali
7. Abdallah Chavula
Wote ni Mawakili wa Serikali Waandamizi isipokuwa Jenitreza Kitali ni Wakili wa Serikali.
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shauri limekuja kwa ajili ya kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja, tupo tayari Kuendelea
Jaji: Utetezi
Wakili Peter Kibatala: na sisi tupo tayari Kuendelea
Jaji anaandika
JAJI: Anakuwa Shahidi namba ngapi?
Wakili wa Serikali: Namba 03
Jaji: Majina
Shahidi: namba F 5914 D Coplo Hafidh Abdallah Mohamed
JAJI: umri
Shahidi: 38yrs
Jaji: Kazi S
hahidi: Askari Polisi
Jaji: Dini
Shahidi: Muislam
Shahidi: Mimi namba F5914 Coplo Hafidh naapa kuwa kwa ushahidi huu nitakaotoa utakuwa wa kweli, Eeeh Mwezi Mungu nisaidie
JAJI: KIAPO KIPO SAWA?
Jaji: asaidiwe
Shahidi: Mimi Coplo Hafidh nathibitisha kuwa Ushahidi nitaka toa utakuwa wa kweli, kweli mtupu, Eeh Mwenye Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali: nitakuuliza Maswali utajibu kwa Sauti
Wakili wa Serikali: Kazi yako
Shahidi: Askari Polisi, nafanya Makao Makuu DSM
Wakili wa Serikali: Askari polisi tangu lini
Shahidi: 2013
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama tukufu Kituo chako cha kazi ni wapi
Shahidi: Forensic Beaural Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Forensic Beaureau ni kitu gani
Shahidi: ni Maabara ya Uchunguzi wa Kisayansi
Wakili wa Serikali: Upo Kitengo gani
Shahidi: Silaha na Milipuko
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Kitengo chako kinahusika na Nini (Ballistic and Explosions)
Shahidi: Uchunguzi wa silaha na Milipuko
Wakili wa Serikali: Upo tangu lini?
Shahidi: Tangu 2014
Wakili wa Serikali: umesema Kitengo Chako Kinahusika Kuchunguza silaha, eleza Majukumu yako ya Msingi ni yapi
Shahidi: Kuchunguza Kitako cha Risasi(cartridges)
Wakili wa Serikali: Jingine
Shahidi: Kwenda Eneo la tukio kwa Uchunguzi
Wakili wa Serikali: Jingine
Shahidi: Kuandaa Riport baada ya Kuchunguza Ballistic and Explosion Report
Wakili wa Serikali: Jingine
Shahidi: Kutoa Ushahidi Mahakamani
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama kama unajukumu lingine
Shahidi: Hakuna
Wakili wa Serikali: Mnafanya Mambo yapi
Shahidi: Kupokea Silaha mbalimbali zinazofanya Uhalifu, Je hii silaha Inafanya kazi..? Hii silaha ni Mzima..? Hii sasa ni Physical Examination.
Wakili wa Serikali: sasa Mnafanya nini
Shahidi: Tunafanya Visual Examination
Shahidi: hii Bunduki ni Mzima, Ina Koki,.? Ina Magazini.? Je Magazini ni Nzima..? Kama inagonga Vizuri kama Nyundo inanguvu..? NitaIkoki katika Upande wa Mitambo Inafanya Vizuri Je Fine pin Inafanya Kazi?
JAJI: fine pin ni nini?
Shahidi: Kiwashio cha Risasi
Shahidi: Nitaangalia Ndani ya Bao (Mtutu) internal Ballistic Ni Safi..? Nitaikoki kama Inafanya Vizuri, Ni hayo tu
Wakili wa Serikali: sasa Uchunguzi wa aina ya pili ni upi
Shahidi: Nimepokea Pistol au SMG
Wakili wa Serikali: Unaitwaje huu Uchunguzi wa Pili
Shahidi: Comparison Examination
Wakili wa Serikali: Kitu gani kinafanyika
Shahidi: Nachukua Ganda nililoletwa na Mteja Kisha napeka kwenye Mitambo Maalum
Wakili wa Serikali: Unafanya hii Comparison Kubaini nini
Shahidi: Je hii Risasi inasifa hii
Wakili wa Serikali: Mnatumia Mitambo Maalum
Shahidi: Unaitwa Computer Microscope and digital Camera Forensic Machine LAECA 2004
Wakili wa Serikali: Umeeleza Vyema, Kuhusu Uchunguzi wa Silaha Kwenye Risasi unafanya kitu gani
Shahidi: Kitaalamu inaitwa Life ammunition...Risasi itaangalia Kiwashio, Je imegongwa..!
Wakili wa Serikali: na hiyo Miss fired ieleze Mahakama, Je live ammunition ikiwa Miss fired Maana yake ni nini
Shahidi: Ni mbovu sababu ulipiga haikulipuka
Wakili wa Serikali: fafanua sasa Mahakamani endapo haijagongwa ni vipi
Shahidi: kama haijagongwa ni Nzima
Wakili wa Serikali: Tofauti na Kugomgwa na kutokugongwa Mnafanya kitu gani
Shahidi: tunaangalia Gun Powder Resolutions
Shahidi: kwemye Risasi Kuna Powder tunaangalia Je powder yako imeganda au Nzima
Yani Bullets Catridge tuna angalia Michuruzi yani Internal Ballistic
Hizo alama za Kipekee tunasema Proved, Shahidi Tuna angalia kitu kinaitwa Twist, Twist silaha/Risasi Kuna Twist Right na Twist Left, Na angalia Counts inasema Twist Right na Left Nyingine unapopiga Kuna Counts Mbili unapopiga Mpaka Kumdhuru Mtu. Inatusaidie Silaha mbalimbali zinazoweza Kufanya uhalifu
Wakili wa Serikali: Tumalizie kwenye Mlipuko, unachunguza nini
Shahidi: Inapotokea Mlipuko wowote sisi tunakwenda Kwenye Eneo la Tukio (SCENE), Wanaenda Askari wa awali. Alafu tunaenda sisi wataalamu Kuangalia kama Kilichotokea ni Local Explosive au Industrial Explosive
Wakili wa Serikali: Wewe unautalamu gani sasa,
Shahidi: Kuchunguza Silaha Mbalimbali ambazo zinatumika kwenye Uhalifu
Wakili wa Serikali: Kozi ya kwanza
Shahidi: Kuchunguza Maganda ya Risasi Mbalimbali
Wakili wa Serikali: Ulifanya kwa Muda gani
Shahidi: kwa Miaka 2
Wakili wa Serikali: kingine tofauti ya kuchunguza
Shahidi: Kuandaa Riport za Kitaalamu
Wakili wa Serikali: Kozi gani Nyingine umefanya
Shahidi: Kozi ya Uchunguzi wa awali ya Upelelezi, Basic CID course
Wakili wa Serikali: Ulifanya Mwaka gani na wapi
Shahidi: Mwaka 2004 kwenye Polisi College Zanzibar
Wakili wa Serikali: Ulijifunza nini huko Zanzibar
Shahidi: Nilijifunza Mambo mbalimbali ya Kiupelelezi, Nilijfunza Bunduki Kupiga, Kuchukua alama za Vidole, kutafuta Finger Prints. Kulift Finger Prints, baada ya Kuchunguza Finger prints na Kuhamisha
Wakili wa Serikali: Kingine
Shahidi: Kufungua na Kuirudishia Bunduki
Wakili wa Serikali: Kingine
SHAHIDI: Nilipata Elimu ya awali Juu ya ku Collect Ushahidi Katika Crime scenes
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama kama ulioata Kozi Nyingine
Shahidi: Baada ya Kurudi Ofisni nilihitajika kwenda Kozi Nyingine Moshi Mwaka 2006
Wakili wa Serikali: Ulijifunza kitu gani
Shahidi: Techniques, protocol in Fire arms Evidence
Wakili wa Serikali: fafanua
Shahidi: Kufungua silaha, Vifaa vyake Kuirudishia, na Kutengeneza kama inawezekana NikAfanya Polisi College Dar es Salaam ambayo inaitwa Ballist tools, fire arms, tools and Ballistic Materials testing Mwaka 2007.
Wakili wa Serikali: Kozi Nyingine
Jaji: Jina Kozi rudia
Shahidi: To determine and Examination of fire arms
Wakili wa Serikali: Wapi
Sahidi: Botswana police College Mwaka 2010
Wakili wa Serikali: NYINGINE
Shahidi: 2015 inaitwa Forensic in General
Ballistic Woundage, Vidonda, Mtu amepigwa Bastola amekufa naangalia Shooter alikuwa Upande gani
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Utaratibu wa Kupokelewa Vitu Vya kufanyia kazi ukoje
Shahidi: Kwanza Mteja awe na Barua
Wakili wa Serikali: kwenye Barua kuna kuwa na nini
Shahidi: Barua ionyeshe kosa
Wakili wa Serikali: Kingine
Shahidi: aeleze nini anaomba tumfanyie
Wakili wa Serikali: Tofauti na Barua anakuwa na Nini
Shahidi: aje na hivyo Vielelezo husika sasa
Wakili wa Serikali: Barua pamoja na Vielelezo hupokelewa eneo gani na nani anapokea
Shahidi: anakuwa Afisa wa zamu anayetupangia Leo utakuwa zamu na Kupokea Vielelezo Tunakuwa wawili
Wakili wa Serikali: Makishapokea kama Afisa wa zamu anafanya nini
Shahidi: Tunapokea Barua na Kielelezo nafungua Kujiridhisha Alivyovileta yupo sahihi
Wakili wa Serikali: Ofisini Kwako Unapofanyia kazi, ifahamishe Mahakama Silaha au Mlipuko I natokea wapi
Shahidi: Vituo Vya Polisi na hata TANAPA kuja Kufanya Uchunguzi
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Utaratibu wa Kupokelewa Vitu Vya kufanyia kazi ukoje
Shahidi: Kwanza Mteja awe na Barua
Alivyovileta yupo sahihi
Wakili wa Serikali: Ukishajiridhisha
Shahidi: Lazima niangalie Safety kabla haijaingia Laboratory
Wakili wa Serikali: Umeshajikizisha Vielelezo na Usalama sasa, Unatakiwa Ufanye kitu gani
Shahidi: Natakiwa Kuingia Laboratory nitai Register
Wakili wa Serikali: Barua pamoja na Vielelezo hupokelewa eneo gani na nani a napokea
Shahidi: anakuwa Afisa wa zamu anayetupangia Leo utakuwa zamu na Kupokea Vielelezo, Tunakuwa 2
Wakili wa Serikali: Mkipokea kama Afisa wa zamu anafanya nini
Shahidi: Tunapokea Barua na Kielelezo nafungua Kujiridhisha
Wakili wa Serikali: inapelekwa kwa Afisa incharge kwa Madhumuni gani
Shahidi: Lazima atambue ni silaha gani, Na nitampa Mtu Kuchunguza hii Kesi
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Mnamo tarehe 25 November Unakumbuka ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Ofisini Kwangu Makao Makuu madogo Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Kwa Kufanya nini
Shahidi: Nita andika Exibit K1 nitaweka FStroke ya Mwaka gani
Wakili wa Serikali: inapelekwa kwa Afisa incharge kwa Madhumuni gani
Shahidi: Lazima atambue ni silaha gani Na atampa Mtu Kuchunguza hii Kesi
WS: baada ya Kusajili Vielelezo Upelekwa wapi
Shahidi: Nitapeleka Sehemu ya Kuhifadhi silaha WS Barua utaipekeleka wapi
Shahidi: Kwa Afisa Incharge
Wakili wa Serikali: inapelekwa kwa Afisa incharge kwa Madhumuni gani
Shahidi: Lazima atambue ni silaha gani Na atampa Mtu Kuchunguza hii Kesi
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Mnamo tarehe 25 November Unakumbuka ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa Ofisini Kwangu Makao Makuu madogo Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Ulikuwa wapi
Shahidi: Kwenye Dawati la Kupokea Vielelezo Mbalimbali
Wakili wa Serikalil Ulipokea Vielelezo Vipi Siku hiyo
Shahidi: nikipokea Vielelezo Kutoka Ofisi ya DCI, Ambavyo ni Pistol yenye namba A5340 callibre 9mm, Ikiwa na Magazine Yenye Rangi Nyeusi Na Nikapokea Risasi 03 WS: za Silaha gani
Shahidi: za Pistol Caliber 9mm
Wakili wa Serikali: Vielelezo hivyo viliambatana na nini
Shahidi: kwanza alivileta PC Goodluck kutoka Ofisi ya DCI
Wakili wa Serikali: Goodluck aliwasilisha nini
Shahidi: Barua
Wakili wa Serikali: baada ya Kupokea Vielelezo hivi na Barua ieleze Mahakama Ulifanya nini
Shahidi: Nilivi-Lebel kama nilivyosema awalI Pistol niliioa alama Exhibit K1, Nikosa ili kwa FB /BALL/LAB 158/2020
Wakili wa Serikali: na hizi Risasi 03
Shahidi: nilizipa alama ya K2 K3 na K4 Wakili wa Serikali: Risasi hizi ulizipa Usajili upi
Shahidi: 158 Kama Pistol
Wakili wa Serikali: Baada ya Kukamilisha Usajili wa Vielelezo Ulichukua hatua gani
Shahidi: Kufanya Uchunguzi wa Kuutambua Hiyo Bunduki na Risasi ni Nzima K2, K3 na K4
Wakili wa Serikali: na Kuhusu Vielelezo Pistol na Risasi ukafanya nini
Shahidi: Kwanza ile Pistol niliipima
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kupima, Tupo kwenye hatua ya Upokeaji
Shahidi: Nika-Minutes Kumpelekea Boss
Wakili wa Serikali: Vielelezo Ukapeleka wapi
Shahidi: Nilipeleka Chumba cha Kuhifadhia Silaha
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Nani aliteuliwa kufanya Uchunguzi
Shahidi: Mimi Mmoja wapo
Wakili wa Serikali: Uchunguzi huo ulifanya lini
Shahidi: nilianza Kufanya Tarehe 25 Uchunguzi wa Awali
Wakili wa Serikali: Katika Uchunguzi wako Ulifanya nini Kulingana na Mahitaji
Shahidi: Hatua ya kwanza
Wakili wa Serikali: Mteja alikuwa anataka nini
Shahidi: Mteja alikuwa anataka Kujua ile Pistol na Risasi zilifanya kazi
Wakili wa Serikali: sasa wewe Ulifanya nini
Shahidi: Kwanza Ile Bastola nilipima na Kifaa kinaitwa GUN BARROW GAUGE
Hapo nilikuwa napima Kwenye Barrow yani Mtutu kwamba ile Callibre ni kweli 9mm
Nikaona ni kweli ipo sahihi ni 9mm
Wakili wa Serikali: KingiNe
Shahidi: nikatoa Magazine kumbuka ilikuwa na Magazine inaitwa MAGAZINE RELEASE, Naangalia Magazine yake ile Bastola ni ya kwake, Nikaona Okey Magazine ni ya Kwake
Wakili wa Serikali: Jingine
Shahidi: Ndani ya Magazine Kuna Spring ambayo Ukiweka Risasi inashuka Chini, yenyewe inapandisha Risasi juu, Nikaona Nzima Nikaangalia Nyundo Hummer Kama Nzima sometime inakuwa loose nimabaini, Nzima Nikaangalia Triger kwa kutumia Triger Pull ....kama inafika kwenye 100 nimEbaini ni Nzima
Shahidi: Nikaenda ndani ya Barrow nikatumia Mdeki Kuangalia kama Ilikuwa Safi au Chafu Kupoteza Ubora wake, Nimabaini Barrow lipo Vizuri halina Vumbi hakuna Mchanga Maana yake Barrow lipo safi, Lolote linaweza Kufanya Baada ya hapo nikaikoki kungalia Firing Pin Mechanism kama ..Nilibaini Ipo
Kwa hatua hiyo niliishia hapo
Wakili wa Serikali: Kwa Aina za Uchunguzi ulizotutajia huu ni Uchunguzi wa aina gani
Shahidi: ni Visual Examination
Wakili wa Serikali: kwenye zile Risasi 3 ulichunguza nini
Shahidi: pale niliingia Sana kwenye Pin Impresion kwa Maana Primer au Kiswahili Chake ni Kiwashio au Kitako cha Risasi
Wakili wa Serikali: Hatu gani ikafuata Shahidi: Hatua ya Pili ya Uchunguzi wa Pili
Shahidi: Nilichukua Risasi Mbili ya zile nilizoletewa callibre yake 9mm, Nikaenda kwenye Chumba Maalum Kwenye Chumba Kuna sehemu ya kupigia Silaha Mbalimbali.
Wakili wa Serikali: Ulienda na Kitu gani
Shahidi: Nilikuwa na Pistol na Risasi 03
Wakili wa Serikali: Ulienda Kufanya akitu gani hasa
Shahidi: Kuna Kifaa kinaitwa Tank Water Recovered Bullets
Wakili wa Serikali: Kiswahili ni nini
Shahidi: Ni tanki la Maji tunalotumia kupata risasi
Wakili wa Serikali: Kwanini sasa Mnapiga Risasi Kwenye Tanki la Maji
Shahidi: ili Kupata Maganda ya Risasi na Vichwa vyake
Wakili wa Serikali: Kwanini sasa Mnapiga Vile Vielelezo
Shahidi: Najiridhisha sasa, Je Ni kweli zile Risasi ni Nzima.? Na kwenda Kupiga sasa
Wakili wa Serikali: Nini Matokea ya Uchunguzi wa Kina
Shahidi: Nikichukua Risasi Mbili nikaweka Kwenye Magazine Nikaweka kwenye ile Bastola nikapiga sasa, nikapata Maganda na Vichwa Vya risasi. Nikafanya hivyo tena kwa Risasi ya pili, nikapiga
Wakili wa Serikali: Risasi zako zilikuwa na alama, Je Risasi zina alama zipi ambazo ulipiga
Shahidi: K2 na K4
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini sasa kuhusiana na Yake maganda
Shahidi: Nilienda kuyalebo yale Maganda yangu mawili
Wakili wa Serikali: Kwa kuyapa alama gani
Shahidi: T1 na T2, T1 ilikuwa K2 na T2 iliyokuwa K4
Wakili wa Serikali: baada ya Labeling Kitu gani sasa Kingine kilifuata
Shahidi: Nikaenda Kuandaa Report yangu (Ballistic Examination Report)
Wakili wa Serikali: baada ya Kuandaa Ulifanya nini
Shahidi: Nilisaini
Wakili wa Serikali: Kingine
Shahidi: Nilipiga Muhuri
Wakili wa Serikali: Muhuri gani
Shahidi: Forensic Beaural Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Kuhusiana sasa na Silaha Yenyewe
Shahidi: Baada ya hatua zote zote hizo nikafunga kwenye Mfuko na Nikafunga seal, nikasaini na Kuandika Tarehe
Wakili wa Serikali: Baada ya Kusaini Ukapeleka wapi
Shahidi: Chumba cha Kutunzia Silaha Wakili wa Serikali: Na Report yako sasa
Shahidi: Niliweka kwenye Bahasha na Nikairudisha kwenye File Book. Baada ya hapo nikiwa nasubiri wenyewe Waje Kuchukua Vielelezo vyao
Wakili wa Serikali: Vielelezo Vyao Vilikuwa Kuchuliwa Siku gani
Shahidi: Tarehe 27 November 2020
Wakili wa Serikali: Nani alikuja Kuchukua Vielelezo hivyo
Shahidi: Afande Swila Kutoka Ofisi ya DCI
Wakili wa Serikali: Nani aliyemkabidhi afande Swila hivyo Vielelezo
Shahidi: Mimi Mwenyewe
Wakili wa Serikali: Ulimkabidhi Swila Vitu gani
Shahidi: Riport yangu ya Kiuchunguzi Ballistic Examination Report, nikamkabidhi Pistol Moja ambayo ni Exibit K1 Callibre A5340 9mm Model yake CZ 41 Rangi Nyeusi Ikiwa na magazine yake. Pia nikamkabidhi Risasi Moja Nzima iliyobaki Ambayo nili nililebel K3. Nikamkabidhi Maganda Mawili na Bullets zake Yale Maganda niliyalebel kama T1 na T2
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Kwamba tangu ulivyomkabidhi Swila ni Lini tena ulipata Kuviona tena Vielelezo
Shahidi: Jana
Wakili wa Serikali: Kwa Jambo lipi
Shahidi: ili aniletee Vielelezo Kwa ajili ya Ushaidi Mahakamani hii Leo.
Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama hii Report yako ya Kiuchunguzi uliyoiandaa ni kitu gani kitakutambulisha
Shahidi: Kwanza Kwa Nembo ya Ofisi, Nembo ya Polisi Force a namba zangu F5914 Majina yangu ya Copo Hafidh Abdallah
Wakili wa Serikali: Kingine
Shahidi: Na Signature Na Muhuri wa Ofisi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaonyesha anaweza akatambua Nyaraka aliyofanyia Kazi kwa Ruhusa ya Mahakama Tunaomba Kumuonyesha Shahidi anakabidhiwa
Wakili wa Serikali: Shahidi itizame hiyo Kabrasha Ndogo sasa Uimbie Mahakama nilichokupatia ni Kitu gani
Shahidi: Ni report Yangu niliyoindaa kuhusiana na Uchunguzi wa Silaha na Risasi
Wakili wa Serikali: Ifahamishe Mahakama Vitu gani vinaonyesha wewe Ndiyo uliandaa
Shahidi: Kuna Nembo ya polisi, Force Namba, Signature yangu, Kuna Muhuri wa Ofisi kwa hiyo Riport hii ni ya kwangu
Wakili wa Serikali: Unaiomba nini Mahakama hii
Shahidi: Naomba Mahakama hii Ipokee Riport yangu kama Sehemu ya Ushahidi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Ipokelewa Ballistic Examination Report Wakili wa Serikali Wanaipeleka Upande wa Mawakili wa Utetezi
Nashon Nkungu: kwa niaba ya Mshitakiwa wa kwanza sina Pingamizi
John Mallya: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili Pia sina Pingamizi
Dickson Matata: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa tatu pia hatuna Pingamizi
Peter Kibatala: Kwa niaba Ya Mashitakiwa wa Nne pia hatuna Pingamizi
Jaji anapelekewa Nyaraka Mahakama bado Ipo Kimya Kidogo, Jaji anaendelea kuandika
JAJI: Mahakama Imepokea Nyaraka Hii yenye Kichwa cha Habari Ballistic Report Ambayo iliandaliwa tarehe 26 November 2020, Napokea na Kama Kielelezo namba 02
Jaji: Nakuomba Shahidi usaidie Kuisoma
Shahidi anapewa
Shahidi: Forensic Beaural Ballistic Laboratory DSM/F Ya Tarehe 26, Nov 2020 Shahidi anaisoma upya yote
Shahidi amemaliza Kusoma Riport yote ambayo Ndiyo yale aliyokuwa anayaeleza, lakini Sheria inataka asome Upya Mahakamani.
Wakili wa Serikali: Kwa mujibu wa a Taarifa hiyo ulikuwa unachunguza silaha ya aina gani
Shahidi: Pistol A5340 ya Callibre 9mm
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Uchunguzi wako Ulibaini nini Kuhusu Bastola
Shahidi: Ni Nzima
Wakili wa Serikali: Unamaanisha Nini Nzima
Shahidi: Ukiweka Risasi inalipua
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Taarifa yako uliyofanyia Uchunguzi Risasi tatu, Je za Silaha gani
Shahidi: za Pistol caliber 9mm
Wakili wa Serikali: Uhusiano wake Risasi na Bunduki ukoje
Shahidi: Ni za Kwake, kwa Maana zimeingia na Ikapiga (Fire)
Wakili wa Serikali: Kwa Mujibu wa Taarifa yako umesema Unaambatanisha K1, K2, K3 na K4, was attached, sasa Elezea kwanini Kwenye Taarifa Yako Umeandika tena K4 Wakati unasema Ulishailipua
Shahidi: Nimekosea Mheshimiwa Jaji, Ni Typing Error Kwa sababu Nilishailipua.
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo attachments zitakuwa ni nini
Shahidi: K1 ambayo ni Bastola na K3 Wakili wa Serikali: Ukionyeshwa utavitambuaje
Shahidi: Nimeweka Kwenye bahasha, nimesaini nikaandika na tarehe
Wakili wa Serikali: Mbali na hivyo, silaha ina vitu gani Vingine vitakavyokufanya uitambue
Shahidi: kwanza ni serial Namba, Lebbeling ya Forensic ambayo ni K1 FB /BALL /LAB 158 of 2020 Maganda niliya-Lebel kwa T1 na T2 Na vile vile Nika-Lebel FB /BALL /LAB 158 of 2020
Na Bullets nili-Lebel kwa Maganda yake
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi ameonyesha Uwezo wa Kuvitambua, Kwa Ruhusa ya Mahakama naomba Kumuonyesha anaruhusiwa na mahakama Shahidi Tizama Mfuko Mmoja baada ya Mwingime Shahidi anatizama Mifuko ya Nailon ambayo ni Transparent
Wakili wa Serikali: Huo Mfuko ni nini
Shahidi: Mfuko wa Kuwekea Vielelezo Mbalimbali
Wakili wa Serikali: Una uhusiano gani na wewe Shahidi
Shahidi: Ndiyo nilitumia kuweka Bastola
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kinachotambulisha kuwa wewe ndiye Ukiweka silaha
Shahidi: Nilisaini nikaweka na Tarehe 26 November 2020
Wakili wa Serikali: Unasema Kwenye Mfuko huo kuna Kitu gani
Shahidi: Bastola yenye serial Namba A5340 Callibre 9mm CZ 100 nyeusi
Wakili wa Serikali: Mfuko wa Kwanza
Shahidi: Una Risasi, na Nika Lebel na Nikafunga Kwa Seal
Wakili wa Serikali: Kinachokutambulisha kuwa wewe Ndiye Uliweka
Shahidi: Nilisaini na Nikaweka Tarehe, ina alama Exibit K3
Wakili wa Serikali: Tumalizie Mfuko wa Mwisho
Shahidi: Niliweka Maganda T1 na T3 na Bullets zake
Wakili wa Serikali: Unaiomba nini Mahakama
Shahidi: Naomba Mahakama hii Ipokee Vielelezo hivi kwenye kesi husika Wakili wa Serikali: Ipokee nini
Shahidi: Bastola yenye serial Namba A5340 Callibre 9mm ikiwa na Magazine Nyeusi kwa Rangi yake, Model ni CZ 100.
Wakili wa Serikali: Kwenye hiyo Mifuko Mingine
Shahidi: Naomba Mahakama Ipokee Risasi ya Pistol ya Callibre 9mm
Wakili wa Serikali: Uliipa alama gani
Shahidi: K3
Wakili wa Serikali: Mfuko wa Mwisho Mahakama Ipokee
Shahidi: Maganda Mawili ya risasi na Bullets Mbili (Vichwa Vya Risasi)
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi ameomba Vielelezo ambavyo amevitaja Vipokelewe na Mahakama
Wakili wa Serikali Wanaipeleka Mifuko 3 kwa Mawakili Wa Utetezi Mawakili Wa Utetezi Wamezingira Vielelezo wanavikagua Kimoja baada ya Kingine vikiwa bado ndani ya Mifuko.
Nashon Nkungu: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa kwanza hatuna Pingamizi dhidi ya Vielelezo hivi vyote kwa Pomoja
John Malya: hatuna Pingamizi kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili
Dickson Matata: Hatuna Pingamizi kwa Vielelezo Vyote
Peter Kibatala: Mhe. Jaji nasi pia hatuna Pingamizi
Jaji anainama anaandika Kidogo Jaji anawakumbusha kuwa Mahakama Ya Rufani imesema Kuwa Vielelezo havipaswi kupokelewa kwa pamoja Kwa hiyo kwa namba nitavipokea Kwa tofauti tofauti.
Jaji: Basi Mahakama Inapokea Silaha Moja ya Moto aina ya Pistol aina ya A5340 kama Kielelezo Mahakama Inapokea Maganda Mawili ya Risasi ambayo yametumika kama T1 na T3
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Sasa Shahidi akate Mifuko ili aweze Kutuelezea anaruhusiwa Shahidi anachana Mifuko MAHAKAMA ipo Kimyaaaaa
Wakili wa Serikali: Shahidi hiyo unasema ni silaha ya aina gani
Shahidi: Ya Pistol
Wakili wa Serikali: anaishika na yeye
JAJI: Wakili wa Serikali nakutaadharisha ulivyoibeba naona Unamuelekezea Jaji MAHAKAMA KICHEKO Kidogo
Wakili wa Serikali: hii ni Pistol ya aina gani
Shahidi: Luger ya 2005
Wakili wa Serikali: elezea mahakama ulivyokuwa unaelezea hii Pistol
Shahidi: Hiki ni Kifunguo cha Magazine Ukiminya Unaruhusu Magazine Itoke Magazine hii inauwezo wa Kuchukua Risasi nane
Wakili wa Serikali: Unasema Ulitest Magazine
Shahidi: Ukibonyeza hii spiring, nilipima Kama Inanguvu ya kusukuma Risasi Na hiii ni Box Magazine, Na Magazine hii ni Nzima
Wakili wa Serikali: na Ulisema Barrow ndiyo ipi
Shahidi: Ndiyo hii kwa Kiswahili ni Mtutu. Nilipima kwa Kuchukua Barrow Gauge nikatoa kwenye Barrow, Je hii ni 9mm, Ikaniambia ni Yenyewe
Wakili wa Serikali: Ulisema Triger, Triger eleze Triger ipo wapi
Shahidi: nilipima Triger kwa Kuminya hivi, Nikaona Ikafika kwenye 100
Wakili wa Serikali: Kwenye 100 Ikafika hapa
Wakili wa Serikali: Hebu onyesha Mahakamani Firing yake na Uwezo wake
Shahidi: Hapa naikoki, hii ni Pini na hapa Nikikoki pana kuwa na Risasi inaenda Chemba nikaikoki nika-fire nikaona Nyundo Inagonga Vizuri.
Wakili wa Serikali: Kitu gani Nyingine Ulifanya
Shahidi: Nilipima Barrow Kupima Kama ni safi, Nikaona Barrow ipo Safi hii ina serial Namba hawa Luger wanaweka Serial Namba hapa na hapa
Wakili wa Serikali: Ni ipi
Shahidi: Imesajiliwa A5340 Kama haijagongwa serial Namba sijajua imeingia Vipi Nchini hii pia ni Risasi niliipa K3
Wakili wa Serikali: Ulichunguza nini kwenye hii Risasi
Shahidi: Nilichunguza Kiwashio, hapa ikiwa na Chuma Ukigonga inalipuka
Wakili wa Serikali: Kiwashio cha hiyo Risasi kikoje
Shahidi: Kizima
Wakili wa Serikali: Twende Kielelezo Cha Mwisho
Shahidi: Haya ni Maganda Kama Ulienda Marekani wanakuandika 9mm Pass 50 Kwamba Kutoka kwenye Base hadi kwenye Kichwa ni Pass 50 Hizi mbili ni Bullets nimezipata baada ya Kupiga kwenye tenki la Maji Kwa Maana hazikudhuru Mtu. Wanaita Terminal Firing Shahidi anarudishia Vielelezo kwenye mifuko yake
Wakili wa Serikali: Mwisho, kwa ufupi nini Ugunduzi wako
Shahidi: Kwamba Vyote Kuanzia Bastola na Hizo Risasi 3 ni Vizima na Vinafanya kazi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu
Jaji: upande wa Utetezi
Wakili Peter Kibatala: Naomba kwa Ruhusa yako nimtambulishe Jeremiah Mtobesya ambaye alichelewa kwa sababu alikuwa Mahakama ya Rufaa Na ninamatambulisha kwa sababu Yeye Ndiye ataanza Maswali Kwa niaba ya Mshitakiwa wa kwanza
Jaji anaandika Kidogo
Jaji: naliingiza Jina lako kwenye Orodha ya Mawakili
Jaji: Nitaruhusu watu wapumzike Kidogo kunyoosha Miguu na Kupata maji Mpaka Saa saba Na nusu
Naomba tujitahidi Kutunza Muda
Jaji anatoka
Mpaka sasa mahakama haijarejea
Jaji anaingia
Wakili Jeremiah Mtobesya anauliza maswali Kwa niaba ya Mshitakiwa wa kwanza
Mtobesya: Mueleze Mheshimiwa Jaji Kama Unajua Fomu Polisi Fomu Namba 145
Shahidi: Siijui
Mtobesya: shahidi Unafahamu kitu kinaitwa Exibit Lebel
Shahidi: sifahamu
MTOBESYA: wewe Kama Polisi nitakuwa sahihi Nikisema Exibit Lebel ni fomu namba Ngapi
Shahidi: siyo fomu ni Lebel, Siyo Fomu, sisi Ballistic Tunayakwetu, siyo fomu
Mtobesya: unaelewa Kwamba ni Matakwa ya Kisheria Kuhusu Movements za Exibit Kwamba Polisi yoyote anaye Hamisha Kielelezo, hasa Polisi Kuweka Kumbukumbu ya Jina lake na Cheo Chake anatakiwa Kufanyia nini.
Shahidi: Hakuna kitu kama Hicho, Sisi tunasaini uweji Jina wala Cheo
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi nikisema Kwenye Mdomo wa Silaha huwa Kuna Vitu ambavyo Risasi ikitoka inaacha, inaacha Groove ambayo ni Unique kwa Kila silaha
Shahidi: Hapana wewe Unazungumzia Gun powder
MTOBESYA: sasa ndiyo nasema Bullets Ikitoka inaacha Groove?
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Hizo impression za Grooves zinatoka wapi
Shahidi: Hapana, wewe Unasema Gun Powder
MTOBESYA: sasa tuokea Muda wa Mahakama, wewe Unajua Grooves ni nini
Shahidi: Ni Michirizi baada ya Kutoka Risasi
Mtobesya: Kwa hiyo Grooves inapatikana kwenye nini
Shahidi: Baada ya Risasi Kutoka Kwenye Silaha
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi sasa Nikisema kila Bullets inapotoka inaacha Grooves ambayo ni Unique kwa Kila silaha
Shahidi: Sahihi
MTOBESYA: Nitakuwa sahihi, ili utambue Kuwa Risasi hii imetoka kwenye Silaha gani ni lazima nifafanishe Barrow na Grooves Kujua imetoka kwenye silaha gani
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Ni kwanini nikitaka Kujua Kuwa Risasi Imetoka kwenye silaha hii, Imetoka kwenye silaha fulani ni lazima nipigie (Fire) na Kwenda Kulazimisha
Shahidi: Lazima uwe na Specimen ambayo ina Standard fulani ili kuweza Ku-Compare Kwahiyo mimi ni lazima nitapiga Kwenye Bullets water Tank kufanya Mlinganisho
Mtobesya: Kwa hiyo ili Ujue ni lazima Kulinganisha grooves?
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwa hiyo Wakati Unaonyesha Vielelezo ulituonyesha hizi Grooves ndiyo zilizofanana?
Shahidi: Nilionyesha Bullets
Mtobesya: Ulionyesha Grooves
Shahidi: Nilionyesha Pin Impresion
MTOBESYA: Ulionyesha Grooves hukuonyesha shahidi: nilionyesha Pin Impresion
Mtobesya: Kuna tofauti gani kati ya 9mm na 9mm Luger
Shahidi: 9mm ni aina ya Risasi na Luger ni aina ya Bunduki
Mtobesya: Ni Ushahidi wako kwamba Luger siyo aina fulani ya Bastola
Shahidi: Luger ni aina ya Bastola
Mtobesya: Mwambie Mheshimiwa Maana ya CZ 100
Shahidi: Maana yake ni ZCheck republic ni Majina yake
Mtobesya: Kwa hiyo Unakumbuka wakati Goodluck anakupatia Silaha alikwambia ni silaha ya aina gani
Shahidi; Ile ni Ofisi tunaenda kwa Documents Siyo Lala lalala lala tunaenda Kwa Documents Bwanaaaaa
Mtobesya: Wakati anakukabidhi alikukabidhi nini
Shahidi: Pistol yenye Serial Namba A 5340 Callibre 9mm black in Colour
Mtobesya: Unaweza Kuiambia Mahakama Kama kuna sehemu Yoyote Mliandikishana wakati mnakabidhishana
Shahidi: Niliandika Kwenye PF113 Mtobesya aliweka Model Namba
Shahidi: Ndiyo aliweka CZ 100
Mtobesya: Baada ya wewe Kumalizia ulimrudishia nani
Shahidi: Afande Swila
Mtobesya: Mliandikishana pia
Shahidi: Ndiyo nilimkabidhi kwa Documents
Mtobesya: Na Kwenye Makabidhiano uliandika Model Namba
Shahidi: Ndiyo Niliandika Model namba, aina ya silaha, Callibre yake na namba za Risasi
Mtobesya: Wakati wewe umeletewa Silaha Kwa ajili ya kungalia kama ni Nzima Je Mlifanya Finger Prints Kuangalia hiyo silaha
Shahidi: Sikufanya
Mtobesya: Kwa Upande wa Shitakiwa namba 1 naomba Kuishia hapo
Wakili Mallya anauliza maswali
Mallya: shahidi nitakuuliza mambo machache Malya: ni sahihi nikisema ni Maabara iliyosheeni Vifaa Vya Kisasa
Shahidi: Of course
Mallya: Ni sahihi inauwezo wa Kufanya Uchunguzi wa maswala yote unayoyafanya
Shahidi: Inafanya Yote
Mallya: Ni sahihi Kwamba Mnafanya Uchunguzi Kwa Mujibu wa Barua
Shahidi: Ni sahihi kwamba nafuata Maelekezo ya Barua
Mallya: Naomba Kielelezo Mheshimiwa Jaji
Mallya: Soma Paragraph ya Kwanza hapa
Shahidi: I F5914 Hafidh Abdallah Mohamed Coplo wa Police Force States Thats have been engaged in Examination of Fire Arms, Catridge, suspected.... "
Mallya: Kwa Maelezo Yako Ulitumwa na Barua kufanya Nini
Shahidi: nilitumia Kuchunguza Bunduki, Risasi na Maganda ya Risasi
Mallya: We uliletewa Vitu gani Uchunguze
Shahidi: Risasi 03 na Bunduki
Mallya: Maganda yalikwepo
Shahidi: Sikuletewe
Mallya: Vichwa Vya Risasi Uliletewa
Shahidi: Sikuletewa
Mallya: I have been Engaged Maana yake nini
Shahidi: Maana yake "Nimefanya Uchunguzi
MAHAKAMA kicheko
MALYA: uliletewa Maganda ya Risasi?
Shahidi: Nililetewa Risasi
Mallya: uliletewa
Shahidi: Sikuletewa
Mallya: Kwenye Maandishi yako Umeandika "and tools" Vifaa ambavyo hapa hujatuletea
Shahidi: Sikuletewa Vifaaa
Mallya: Soma hapa
Shahidi: And tools, Vifaa Mbalimbali
Malya: eenheee alafu wewe hujatuletea hivyo Vifaa
Jaji: asome sentence Yote tuelewe
Malya: Kwa hiyo Mwambie Jaji Riport yako siyo ya Kesi hii tu
Shahidi: Mimi Sikuletewa Vifaa kwa kesi hii
Malya: Riport hiyo kwa Ushahidi wako inahusiana na Kesi hii na Inazungumzia Uzoefu wako wa kazi
Shahidi: Ndiyo, ndiyo Maana Nimeweka hapa
Shahidi: anasoma... Mwisho and tools Malya Kwa hiyo hizo tools ziko wapi
Shahidi: tools siyo kwa kesi hii tu
Malya: Mwambie Mheshimiwa Jaji
Mallya: Ulisema Umeanza Kazi Mwaka 2013 ni sahihi
Shahidi: Sahihi, Kutoka Mwaka 2013 Mpaka sasa Ni Miaka Mingapi
Shahidi Miaka 18
Malya: haya Katika Riport Yako unasema Unauzoefu wa Miaka 18 Je Umetoa wapi Miaka 18
Shahidi: Siyo kwamba tangu nianze kazi yangu, nikiwa nasoma.
MALYA: Kwenye Riport yako umesema hapa Kuna Errors, Je kuna Erros Ngapi
Shahidi: Hiyo hiyo moja.
Mallya: Shahidi Maana ya Terrorist Maana yake nini?
SHAHIDI: ni ugaidi
Mallya: Terrorism Maana yake nini
Shahidi: Ni Maswala ya Utalii
MAHAKAMA KICHEKO
Malya: narudia tena, Terrorist umesema ni Ugaidi na Terrorism Maana yake nini
Shahidi: Ni Maswala ya UTALII
Mallya: Msomee Mheshimiwa Jaji hapo Ulipoandika Kuhusu "Conspiracy" na Terrorist
Shahidi: anasoma Spelling zake C. o. n. s. I. p. a. r. a. n. C. y
Mallya: Ulikuwa unajua Kuwa Unafanyia Uchunguzi Silaha Zimetoka wapi
Shahid:i Ndiyo
Mallya: Kwa hiyo Ulikuja Kujua Muda gani kuwa Silaha zinahusika na Ugaidi
Shahidi: nilijua baada ya Kufungua Barua
Mallya: Je, kati ya Barua na Silaha Ulianza Kupokea nini
Shahidi: Nilipokea Vyote kwa Pamoja
Mallya: Kabla ya Kesi hii Ulishawahi Kufanya Uchunguzi Juu ya mabomu Au Bunduki
Shahidi: Ndiyo, Niliwahi Kufanya
Mallya: Kwa hiyo unafahamu kwamba Makosa ya Ugaidi ni Makosa Serious au Ni Makosa Mepesi
Shahidi: Mimi niulizie kuhusu Bunduki na Risasi tu mambo ya Ugaidi siyajui. Nita eleza facts Kuhusu Risasi na Bunduki
Malya: Mheshimiwa Jaji aambiwe ajibu swali langu
Shahidi: Sijui Kama ni Makosa Serious au Mepesi
Mallya: Wakati unaelezea Ushahidi wako ulitueleza kwamba wakati unapokea, ulivaa Gloves na Vifaa vingine
Shahidi: Hayo ni Mambo ya Kawaida sana siwezi Kueleza Kila Kitu hapa kwamba Nilivaa Miwani, Gloves na Hijab
Malya: Mheshimiwa Jaji naomba ajibu swali langu
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Je Mtu akiwa na Bunduki haijasajiliwa na haimiliki kihalali Je imaanisha amefanyia uhalifu
Shahidi: Jibu linategemea
Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe risasi, MALYA anapewa anamkabidhi Shahidi
Mallya: Je Shahidi Kuna uwezekano hii ambayo hujaipiga, hatujui kama Inafanya kazi
Shahidi: Hii nimeiacha
Mallya: Si Kuna uwezekano wa kapiga Risasi halafu isilipuke
Shahidi: Ndiyo kama Kumefanyika Mishandling.
Mallya: Kwa hiyo hata Hii inawezekana iwe Nzima
Shahidi: Ndiyo lakini Nilipiga Mbili nikabakisha moja
Mallya: Katika Maabara yenu kuna Vifaa Vya Kupima Finger Prints
Shahidi: Kwa Ofisi yetu?
Mallya: Ndiyo
Shahidi: Ipo lakini Ni Upande wa Mtu Mwingine
Malya: na wewe hukujisumbua kutaka Kujua Kama hii Bunduki Imetoka Kwa binadamu au Kwa Ng'ombe hukujisumbua Kufanya hivyo
Shahidi: Miye nacheza na Barua kwa sababu inataka nifanye nini, nafanya hicho tu.
Mallya: Soma tena hapa
Shahidi: I have been engaged in identification Malya: Mnapo Identify Silaha, Mnafanya Nini
Shahidi: Kungalia Serial Namba Kuangalia Magazine, Tuna angalia Silaha Kwa Ujumla, Tuna angalia Fire arms, Firing Pin, pin Impresion, Hammer, Barrow ..aina ya silaha, Serial Namba yake, Model yake.
Mallya: hapo hapo Kuna Mahali umeandika Examination Report Page Number 02 Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Orodha Ya Vitu Vyote kama Umevionyesha ama Ku-Identify Katika hiyo Report Yako
Shahidi: Sikuvionyesha
Malya: Mheshimiwa Jaji ya kwangu ni hayo tu
Dickson Matata: Kwa ajili ya Mashitaka Wa tatu Sitofanya Cross Examination
jaji: Wakili wa Mshitakiwa namba 04
Wakili Kibatala anauliza maswali
Kibatala: Naomba Nipatiwe Kielelezo P3 P4 na P5 halafu nipewe Dakika 01
JAJI: umevaa Gloves MAHAKAMA kichekoooooo
Kibatala: Sijavaa Gloves
Kibatala; nipo tayari Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Nimeomba Kielelezo Namba 04 Live Amution
Kibatala: umesema hizi Risasi Zina Uhusiano na Luger..?
Kibatala: na Kuonyesha Usome kwenye Kitako
Shahidi: 9mm
Kibatala: Kuna Sehemu imeandikwa Luger
Kibatala: Kuna Sehemu yoyote Umefafanua kwa Jaji kwamba Ktk Kielelezo namba 04 utaona 9mm lakini hakuna Maneno Luger
Shahidi: Sikufanya hivyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: nakuonyesha Risasi Nyingine Soma Kwenye Kitako Iwapo Maneno 75 kama Ilivyokuwa kwenye kielelezo namba 04
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Je, ulifafanua kwa Mheshimiwa Jaji kwamba Kuna Utofauti wa namna hiyo
Shahidi: Sikueleza
Kibatala: Ushahidi wako Katika Mahakama Kwamba hakuna Neno Luger kwenye Risasi na Mheshimiwa Jaji atumie Kupima Ukweli na Uongo wako.
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji hii ni Bunduki au Risasi
Shahidi: Risasi, Ganda la Risasi
Kibatala: Hakuna Neno Luger Chini ya Kitako?
Shahidi: Sioni naona tu 9mm
Kibatala: naomba Mheshimiwa Jaji upatiwe uone
Kibatala: Nakuuliza tena Chini ya Kiapo Usichezee Mahakama
Shahidi: Maneno Luger yapo
Kibatala: Bado unataka Mahakama Ukichukulie wewe ni shahidi Serious kabisa na ni Afisa wa Polisi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Kielelezo hicho kina Maneno 75
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: umesema, wewe Moja ya kazi yako ni Kufanya Comparison Analysis
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kuna tofauti au Hakuna
Shahidi: Upo
Kibatala: Kwa hiyo wewe Unasisitiza, wewe ni Shahidi wa Ukweli Kabisa
Shahidi: Ni sahihi pamoja na haya uliyoyasema
Kibatala: Kazi yangu Kuuliza Maswali tu analysis watafanya watu wengine
Kibatala: Uwepo wa Utofauti wa Maneno Luger na hii 75, hukufafanua kwa Jaji
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Na Kwenye report hiyo tofauti haipo
Shahidi: Haipo ndiyo
Kibatala: KWENYE report umesema wewe Ni Mtaalamu wa Miaka Mingapi
Shahidi: 11
Kibatala: umesema Kilichokufanya Ufanye Uchunguzi ilikuwa ni Barua kutoka KWA NANI
Shahidi: DCI
Kibatala: na Barua hii ni Nyenzo Muhimu sana
Shahidi: Ndiyo, sababu inasema Nini nifanye
Kibatala: na Kwamba Riport yako haiwezi kuwepo bila Barua
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Kwamba wewe ndiyo ulipokea Barua kutoka kwa DCI
Shahidi: Ndiyo Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Iwapo hiyo Barua Umetoa kama Kielelezo
Shahidi: sikuitoa
Kibatala: Sema kwa Mheshimiwa Jaji Iwapo Uliitambua kuwa Barua hiyo ni Hii Hapa hata Kama hujatoa kama Kielelezo
Shahidi: Haipo hapa
Kibatala: Kwa hiyo hujaitambua
Shahidi: Niliitambua Ofisni
Kibatala: Kwani hapa ni Ofisini
Shahidi: Hapa Mahakamani
Kibatala: Uliitambua
Shahidi: Hapana
Kibatala: Barua inaonyesha Bunduki na Risasi Zimetoka kwa nani
Shahidi: Haupo sahihi inaonyesha makosa tu
Kibatala: Kwa hiyo wewe yale Makosa Kwenye Riport yako yametoka kwenye ile Barua
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ambapo hiyo Barua hapa Mahakamani Haipo
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Hapana hatuwapi watuletee Ombi Kwa Mujibu wa Sheria.
Jaji: Kwa nini sasa
Wakili wa Serikali: Ndiyo Msimamo wetu
Kibatala: Mheshimiwa Jaji ili Kuokoa Muda Wakili Mtobesya ataendelea Kunitafutia
Kibatala: Naomba Mahakama Inisaidie Kielelezo p2
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Ulisema Uliletewa Vielelezo Vya Bunduki na inatoka Ofisi ya DCI
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Katika Maelezo yako Hukusema D. COPLO Goodluck anatoka Ofisi ya Upelelezi Dar es Salaam
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati Unatoa Ushahidi Ulisema Uliletewa Vielelezo Vya Bunduki na inatoka Ofisi ya DCI
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Katika Maelezo yako Hukusema D. COPLO Goodluck anatoka Ofisi ya Upelelezi Dar es Salaam
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na Hukusema D. COPLO Goodluck anatoka CID Arusha..?
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Barua inasema D. COPLO Goodluck Anatoka wapi
Shahidi: Ofisi ya DCI
Kibatala: Shahidi Una uhakika na hilo nakukumbusha Upo chini ya Kiapo
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Katika Report yako hii hakuna a Mahala popote Hakuna Mahala umezungumzia Bunduki aina ya luger
Shahidi: Sikuweka, Nimeweka Model na Namba
Kibatala: Shahidi CZ100 Ulitoa wapi
Shahidi: Kwenye Bunduki
Kibatala: Hukutoa Katika Nyaraka za Makabidhiano wala Katika Barua iliyotoka kwa DCI
Shahidi: Ilikwepo
Kibatala: Je katika Hati ya Makabidhiano hii MODEL CZ 100 Ilikwepo au haikuwepo
Shahidi: Ilikwepo
Kibatala: Kupitia Kielelezo P2 unasema Ulipokea K2 Mpaka K4 Mwambie Mheshimiwa jaji Kama Maelezo hayo yapo au hayapo
Shahidi: Sikuweka
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji pia Kuwa Maelezo ya ufafanuzi tuliyoyaona katika Live Catridge hapa, hayapo
Shahidi: Sikuweka
Kibatala: Unafahamu Kwamba Riport Kama hii haiongezewi Nyama Kutoka kwenye kizimba inatakiwa ijiongelee Yenyewe, Unafahamu au hfahamu
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Ni sahihi Nikisema wewe Kingereza Unakifahamu Ndiyo Maana Taarifa umeandika kwa Kiingereza
Shahidi: Ndiyo
KIBATALA: Nini Maana ya DCI
Shahidi: Director Criminal of Investigation
Kibatala: na ukasema Goodluck ametokea Ofisi gani DCI
Kibatala: Soma hapa shahidi: D/C Goodluck from Criminal Investigation Office
Kibatala: Nilipokuuliza Ulisema hivyo
Shahidi: Sikusema hivyo
Kibatala: kwa hiyo Kuna Utofauti Ulichoandika na Ulichosema Kwenye kizimba
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Shahidi Kwa Mujibu wa Kielelezo namba P2 ulipewa Risasi 03 ambazo ni Live, ambazo sisi ndiyo Vidhibiti vyetu, Umeviona hapa Mahakamani
Shahidi: Havipo, Nilivipiga
Kibatala: Sijakuuiza Kuhusu Kuvipiga
Kibatala: Ulicholeta Wewe ni Risasi Moja na Maganda Mawili ambayo hata hivyo vinatofautiana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji ilikulazimu Kutimiza Vidhibiti, Kwamba Katika Ofisi ile palikuwa hakuna Risasi Nyingine Mbadala ililazimu Nitumie hivyo
Shahidi: Sikusema hivyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Iwapo Kuna Mahala yoyote ulipata Idhini ya kutumia Vithibiti kutoka kwa incharge wako kwa Kesi ya Ugaidi Kubwa kama hii
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwani Barua upo Mstari unasema Unaweza Kutumia Risasi Kupiga kwenye Water Tanki
Shahidi: Upo Kibatala: ikija tutaona
Kibatala: lakini Mahakamani pia hukusema
Shahidi: Ndiyo sikusema
Kibatala: Rangi ni Kitu ambacho unaweza Kujua Kwa Visual Examination au Ballistic Examination?
Shahidi: Kwa Visual Examination
Kibatala: Na Kuonyesha Kidhibiti kama Uliweka Rangi wakati unapokea
Shahidi: Sikuweka Rangi, Kwenye Visual Niliweka Rangi
Kibatala: Wakati unapokea
Shahidi: Sikuweka Rangi
Kibatala: Pamoja na Rangi unaona kwa Kuangalia tu, ila wewe hukuweka Rangi baada ya Kupokea
Shahidi: Siku weka Rangi
Kibatala: Kwa kuwa hukuweka Rangi huku ukaweka Rangi, Kuna Utofauti au Hakuna Utofauti
Shahidi: Kuna Utofauti
Kibatala: Barua iliyokuja hilo Kosa ambalo limeandikwa huko liliandikwa hivyo Conspiracy to Commit Terrorist
Shahidi: Iliandika kwa Kiswahili Kujihusisha na Ugaidi
Kibatala: Wewe sasa KINGEREZA chake ndiyo Ukatafsiri kuwa "Conspiracy to Commit Terrorist"
Shahidi: Ndiyo Nimetafsiri hivyo
Kibatala: Kuna Mahala Popote Umemwambia Jaji Kuwa wewe ni Gazzeted Officer?
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Umetaja Serial Namba, Je umemwambia jaji Kuwa ile Serial Namba ya Bunduki Kielelezo P3, inapatikana Kwenye Bunduki Moja tu Hapa Duniani, Ulimwambia hivyo
Shahidi: Si kumwambia Hivyo
Kibatala: Wakati wa Ushahidi Wako nilisikia Umesema Mwaka wa Kutengeneza Bunduki ilikuwa Mwaka gani
Shahidi: Mwaka 1995
Kibatala: Ulielezea hivyo
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Nimesikia Ulisema Bunduki hiyo Inauwezo wa Kubeba Risasi 08 ila wewe ulipewa Risasi 03
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mhe. Jaji Iwapo Ulisema Lolote la Kiuchunguzi Iwapo Risasi Nyingine 05 katika Bunduki hiyo Ilipiga Kwa Muda Mfupi uliopita
Shahidi: Sikuzungumzia
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba ni Utaratibu wa Kawaida Kila Bunduki inapokuja Kwenye kwenye Uchunguzi lazima Nitumie Vielelezo Vilevile Kupiga katika water Tank
Shahidi: Nilimwambia
Kibatala: Shahidi Katika Ushahidi wako wote kuna Mahala popote umesema Kuna Nyaraka Ilikuonyesha kwamba Kuna Uhusiano na Mtu anayeitwa Adam Kasekwa
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Katika Barua iliyoletwa Majina hayo yalikwepo au hayakwepo
Shahidi: Hayakwepo
Kibatala: katika Hati ya Makabidhiano Majina hayo yalikwepo au hayakwepo
Shahidi: hayakuwepo
Kibatala: katika Hati ya Makabidhiano Goodluck alikukabidhi wewe Vidhibiti, Je 9mm iliandikwa?
Shahidi: Haikuandikwa
Kibatala: Ulishawahi Kumwambia Mheshimiwa Jaji kwamba Hiyo Calliber 9mm
Shahidi: Sikumwambia
Kibatala: Pamoja na Hati ya Makabidhiano na Barua kutokutaja Callibre 9mm, Katika Kidhibiti K1 Bastola ametaja Callibre 9mm kabla Ya Uchunguzi
Shahidi: Ndiyo Nilijaza Kabla Ya Uchunguzi
Kibatala: Mheshimiwa Jaji kuhusiana Zoezi nililositisha kuhusiana tulichozungumza Asubuhi, Nasubiria sasa
JAJI: nawaomba Mawakili wa Pande zote mbili Ofisini Kwangu
JAJI: nahairisha Kwa Dakika 10
Jaji anatoka
Dakika 10 zimekwisha, bado jaji na mawakili hawajarejea
Jaji amerejea
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire na Wenzie inatajwa
Jaji: Muda uliopita Wakili aliomba Jambo Mahakama, Sasa tunaweza Kuendelea
Kibatala: Unakumbuka Kila kitu D/Coplo Goodluck alikutambulisha anatoka Ofisi ya DCI?
Shahidi: Sikusema anatoka Arusha
Kibatala: Ni Ushahidi Wako Katika Makabidhiano Kwamba D/Coplo Goodluck anatoka KWA DCI au CID Arusha
Shahidi: CID Arusha
Na Nyaraka hii ni Nyaraka ya Kisheria
Kibatala: Unafahamu Madhara ya Utofauti wa Ushahidi Wako na Yaliyopo kwenye Nyaraka?
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ni sahihi Katika Hati hii Ya a Makabidhiano Inasema Vitu Fulani, Kutoka Sehemu fulani na Inasehemu ya kutaja Majina
Shahidi: Haina sehemu hiyo
Wakili wa Serikali: OBJECTION wakili Kibatala ananyanyuka Nyaraka Juu Maana yake nink
JAJI: kwahiyo tatizo Kunyanyua
Kibatala: Nitaweka Chini basi
Kibatala: Kwa hiyo shahidi Nyaraka hii haina sehemu ya Kujaza Majina
Shahid:i HAKUNA
Kibatala: Hakuna Sehemu Unayotakiwa Kujaza aina Ya Vifaa unavyokabidhiwa?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nyaraka hii pia Inasehemu ya a nafasi ya Kuweka Majina ipo au Haipo
Shahidi: HAIPO
Kibatala: na Sehemu Ya Kujaza Aina ya Mashitaka Kwamba anatuhumiwa kwa Makosa........... IPO HAIPO..?
Shahidi: Haipo
Kibatala: Je katika Hii Hati ya Makabidhiano kuna Mahali inasema Jina la Fulani na mkabidhi Mtu fulani katika Fomu hii
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Inasehemu ya Kuweka Saini
Shahidi: Ipo Nimeweka Force Namba na Saini yangu
Kibatala: Ndiyo Ushahidi Wako huo?
Kibatala nilikusikia sahihi Ujuzi una utalamu wa Kutosha kuhusu Maswala ya Bunduki Nchini Tanzania
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Katika Ushahidi wako wote Uliwahi Kumwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa aina ya Bunduki CZ100 Luger ni Moja wapo ya Bunduki kutoka Jeshi la Wanachi Tanzania
Kibatala: Swali la Mwisho Kwako Kuna Mahala Popote ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuhusu Ulinganifu Kati ya Ofisi ya CO ARUSH na DCI..?
Shahidi: Sikumwambia
Jaji: Re examination
Wakili wa Serikali: Shahidi nitakuuliza Kwa ajili ya ufafanuzi kwa Yale uliyoulizwa Mahakama uweze Kuelewa Ushahidi wako
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Maswali Kwenye Riport Yako Paragraph ya Kwanza inapoanza I have been engaged...Tools na Maganda
Shahidi: Paragraph ya Kwanza Inajielezea Na Inajielezea Uchunguzi Nilikuwa nafanya pale Forensic kwa Miaka 10 nikaweka Bunduki, Risasi(ammunition), Maganda (spent Catridge) Na nikarejea Nimefanya Uchunguzi huu kwa Muda wa Miaka 10
Wakili wa Serikali: Sasa Tools ambayo havikuletwa kwako Vifafanue hapo
Shahidi: Sasa hao hawakuleta Tools, Wakili wa Serikali: sasa Kwanini hukivikufika hapa
Shahidi: Sababu, Ndiyo navichunguza pale Forensic Beaural
Wakili wa Serikali: Kuna Maswali Umeulizwa hapa ukasema Ni Maswala ya Utalii Unakumbuka
Shahidi: Ndiyo, Nilisema Terrorist, spelling nikatamka, Nikasikia Tourism, Tourism ni Maswala ya Kitalii.
Wakili wa Serikali: Lakini kilichopo kwenye Riport yako ni Kitu gani
Shahidi: ni Terrorist
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Ukasema Hapa Firing Pin, Barrow na Ukaulizwa ulionyesha Mahakama Jinsi hivyo Vitu vinavyofanya kazi
Shahidi: Nilionyesha
Wakili Mallya: OBJECTION Mheshimiwa Jaji Sikuuliza Swali la namna hiyo
Wakili wa Serikali: Nauliza na wenzangu
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Nimeulizana na Wenzangu Jibu ni kuwa Sikuonyesha, ipo katika Riport Yangu
Wakili wa Serikali: Shahidi Kwanini sasa Hukuweka
Shahidi: Nilichoweka nilichoombwa na Mteja tu
Wakili wa Serikali: Sasa Ulichoombwa ni nini
Shahidi: Kuchunguza Pistol, Risasi na Maganda ya Risasi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Ukasema Kwenye Riport Yako hakuna Neno Luger, Ieleze Mahakama Kwanini hukuweka
Shahidi: Bunduki ni Serial Namba
Wakili wa Serikali: Kwanini Unasema Bunduki ni Serial Namba
Shahidi: Serial Namba ni Unique
Wakili Malya: OBJECTION Hiyo ni New Fact Kwa sababu Hakueleza Kuwa Serial Namba ni Unique
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tukumbushwe
JAJI: Ndiyo, Kibatala alimuuliza Kwamba Je serial Namba haiwezi Kuonekana kwenye Bunduki Nyingine yoyote
Wakili wa Serikali: Hukueleza Mahakama Kwanini Luger hukuweka Kwenye Riport
Kibatala: OBJECTION tuliuliza Luger ipo au Haipo, Jibu likasema Haipo, akijibu Lolote ni New Fact labda turuhusiwe tena Kumuhoji wakimaliza.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji sisi tunataka atoe Sababu Kwanini Haipo
JAJI: hiyo itatupeleka kwenye New facts na Sababu watatakiwa warudi pia Kumuhoji upya
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunashukru
Wakili wa Serikali: ulimaanisha Nini Kusema Vielelezo Haipo Mahakamani
Shahidi: Nilikuwa namaanisha Kuwa havipo Kwa sababu Nimevitumia Kupiga Katika Ile Bastola
Wakili wa Serikali: Ilifuatiwa na Swali Hukumwambia Mheshimiwa Jaji Kuhusu Kutoleta hivyo Vielelezo
Shahidi: Mimi nilifuata Maelekezo ya Barua, Kwamba Natakiwa Kupiga, nikapiga
Jaji: Swali lilikuwa linahusu nini na Alichokujibu ndiyo ulichouliza
Wakili wa Serikali: Kajibu Tofauti
Wakili wa Serikali: Nilikuwa nataka Kujua Shahidi Ulikuwa unamaanisha Nini Kusema Hukuwa na Idhini
Shahidi: Kimyaaaaaaaaa
Wakili wa Serikali: Naomba Nitoke hapo Mheshimiwa Kuokoa Muda wa Mahakama
Wakili wa Serikali: Katika Ushahidi wako Unasema ulipokea Kielelezo Cha kumpokea 9mm lakini kwenye Barua Hakuna
Shahidi: Kwa sababu Wale ni Layman hawawezi Kujua ni Silaha ya namna gani, Mimi Ndiyo Mtaalamu nikajua ni Pistol Calliber 9mm
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba Mwenzangu aendelee
Wakili wa Serikali Katuga: Shahidi Uliulizwa Kama Uliomba Idhini Kwa Kiongozi wako ili utumie Risasi hizo hizo, Hebu eleza Ni kwanini Hukuomba Idhini Wakili Peter
Kibatala: OBJECTION tunarudi Kulekule kama alitoa Sababu itakuwa Mpya, Anaalika Shahidi atoe Sababu
Jaji: Swali linasema
Wakili wa Serikali: Kwanini hakuomba Idhini
Wakili Peter Kibatala: Itakuwa New Fact akijibu
Wakili wa Serikali: Tunaomba tupewe Nafasi wao Ndiyo walifanya Cross Examination
JAJI: Ngoja aendelee
Shahidi: Kwanza ni Mambo ya Kiofisi siwezi Kueleza Hapa Mahakamani, miye naangalia Barua siwezi Kuuliza Afande.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali ni kwanini hukutumia Risasi zilizokwepo Maabara kwa Uchunguzi wako badala yake Ukatumia zilezile zilizoletwa na wao
Shahidi: Kutokana na Barua Yao walitaka Kujua ni Nzima.? ndiyo Maana nikatoa nikapiga kwenye Bunduki
Wakili wa Serikali: Uliletewa Kielelezo Ukatakiwa Usome Nyuma ya maganda, Ukasema ni Tofauti Elezea Maana yake ni nini Wakili
Peter Kibatala: OBJECTION Huko wanakoenda Kupya
Jaji: Naona Kuna problem
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Jaji Nita rephrase
Shahidi: Hakuna nipoombwa Kufafanua Kwenye Barua
Wakili wa Serikali: Kwani wewe Uliomba Kufanya nini
Shahidi: Waliniomba Kufanya Uchunguzi wa Pistol na Risasi, ni Nzima?
Wakili wa Serikali: Katika Uchunguzi wako hakuna Sehemu Umetumia Neno Luger Ukasema ni Kweli Hakuna ulipo tumia, Sasa Uliandika kwa utambulisho Upi
Shahidi: Kwa Serial Namba yake A5340 callibre 9mm, Cz100.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali Kuhusiana na Tarehe 21 November 2020 Vielelezo Kwa ajili ya uchunguzi, Swali Lilikuwa Hukumtaja Ofisa aliyekuwa Hammery ni Ofisa yupi, kwanini hukusema
Shahidi: Sikusema Kwa sababu hayo Mambo ni ya Kiofisi
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba Katika Ushahidi wako wote hujataja Jina la Silaha aliyekamatwa nazo, Kwanini hukutaja
Shahidi: Kwanza sijui Adamoo
JAJI: mmeleta Kitu Kipya
Wakili wa Serikali: Asante
Wakili wa Serikali: Endelea na Kitu cha Pili
Shahidi: Barua hakutaja Majina
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kuhusu D/C Goodluck kwamba anatoka Ofisi ya DCI na Baadae CID Ofisi Arusha
Wakili Peter Kibatala: we Musta OBJECT sisi tulifika Mbali tukamuuliza kama alifafanua Utofauti wa DCI na CID Arusha, Anachotaka ni Maelezo Mapya
Wakili wa Serikali: Basi Naondoa Swali Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Swali Kwamba Barua haikuwa na Maelezo ya silaha
Shahidi: Mimi Ndiyo Nitaeleza Kitaalamu wala siyo wewe Mteja
Wakili wa Serikali: Hafidhi Uliulizwa kuhusu Bastola ambayo Kibatala alitaja CZ 100 kama Ulisema ni Standard ya JWTZ, kwanini sasa Hukusema
Shahidi: Sijui, Miye sijui
Wakili wa Serikali: Hafidh Uliulizwa swali Moja kuwa kwenye Ushahidi wako Hakuna Mahala Popote ulipozungumzia kama Silaha ilikuwa imepigwa kabla ya Kuleta Forensic Beaural
Shahidi: Hawakuomba Kufanya Uchunguzi wa Gun Powder Resolution
Wakili wa Serikali: ambayo ni Kitu gani
Shahidi: Gun Powder Ni Baruti
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali na Wakili Msomi Malya kama Bastola ile iliwahi Kuwa Mbovu na Baadae Ikatengenezwa
Shahidi: Sikuweza Kujua Kama Ingekuwa Mbovu na Vilevile Sikuombwa nifanye
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali pia kuhusiana na Grooves zinazotoka kwenye Bullets kama Zinalinganishwa kutoka kwenye Mtutu Ukasema Hapana, kwanini Hakuwezi kulinganisha
Shahidi: Grooves unaweza kulinganisha endapo Zinakuja Mbili Unachua Specimen Side A na Side B Kufanya Mlinganisho
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu, Hatuna Maswali Mengine
Jaji: Shahidi Tunashukuru kwa Ushahidi wako na Unaweza kwenda
Jaji: upande wa Jamhuri
Wakili wa Serikali: Robert Kidando Tunaomba ahirisho la Shauri hili Mpaka Jumatatu Tarehe 01 November 2021 Tuweze kuendelea na Usikilizwaji
Wakili Peter Kibatala: Hatuna Objection Mheshimiwa
Jaji: Ombi la Kuhairishwa limekubaliwa Mpka Jumatatu Tarehe 01 November 2021
Jaji: Washitakiwa wataendelea Kuwa chini ya Magereza Mpaka tarehe Hiyo
Jaji anatoka
😀😃😃Bora angetafsiri maana yake nimechumbiwa
KabisaHii kesi ni ya kimkakati, ya kumvua nguo "mtu fulani', ambaye hayupo kwa sasa, wa kuelewa na aelewe
Huyo astaafie hapo hapo kwenye ukoplo wasimuongezee matatizo mengine huko maabaraHuyu Njagu kasoma mpaka Botswana huko lakini bado ni koplo wengine form four harafu duala ila wana nyota inakuaje..
kumbuka yuko mahakaman akitoa ushahidi wa kile alichokiandika, sasa kama hujui ulichokiandika unaenda kutoa ushahidi wa kitu gan? mahakaman sio bar ujueKutokujua kiingereza haikufanyi ukawa mjinga mkuu. Mbona Wachina, Warusi, Wakorea n.k. hawajui kiingereza lakini ni wagunduzi wa mambo mengi tu hapa duniani.
Wanapima sijui kitako,mara mm...sijui Bore nini nini huko..Inakera.. Kesi ya Kipuuzi kama Polisi wenyewe walivyo wapuuzi..Polisi wanasema wamemkuta nayo, yeye anasema wamemuwekea. Sasa hapo Nani anasema ukweri?? Na kwanini polisi hawakuchukua finger print ili wapati kidhibiti kisichokua na Shaka?
Refa kuibeba timu yenye uwezo duni ni kazi kubwa Sana, aidha ajitoe au akubali kupopolewa.Ndo maana wanajitoa... Huyu Jaji wa sa hivi naye atajitoa very soon!
Mtu timamu hawezi kusikiliza na kusimamia maagizo toka juu ya kipuuzi kiasi kile!
Ushiriki wa jina la Sabaya na uwepo wa mashahidi waongo kwenye hii kesi ni uthibitisho kuwa:
✓Tuhuma zote ni haramu!
✓Mbowe na wenzake si magaidi!
✓Shahidi namba 2 ni mhujumu uchumi aende aliko Sabaya!
✓Mashahidi toka PT ni zero brainers!
Tofautisha kukosea na kutokujua....msijifiche kwenye kivuli cha kukosea.Hivi mtu akikosea kiingereza anakuwa mjinga kumbe!!? Nilikuwa sijui mkuu.
Askari polisi anaejiita mtaalamu wa sikaha hajui kutofautisha kati ya tourist na terroristHii nchi hakika viongozi wala wasimamizi wa mahakama huwa hawapati akili, kama hawa ma Judge wa hii kesi (Aliejitoa na Huyu Alikuwepo Sasa).
1) Wanasahau kwamba maisha hubadilika. Leo unaemkandamiza pengine kesho mungu anaweza akampa mamlaka juu yako.
2) Kuna maisha baada ya vyeo.
3) Kuna kudharaulika na kuharibu sifa zao za kazi waliozifanyia juhudi kwa miaka mingi, pengine maisha yao yote.
4) Mungu yupo, anaona na anajua kila kinachofanyika.